cnjona
JF-Expert Member
- Mar 24, 2014
- 1,027
- 239
YANGA SC ipo katika mazungumzo na klabu tofauti za Asia na Ulaya ambazo zinataka kununua wachezaji wake watatu, beki Mtogo Vincent Bossou, kiungo Mbrazil Andrey Coutinho na mshambuliaji Mzimbabwe, Donald Ngoma.
BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE inafahamu Yanga SC ipo kwenye mazungumzo na klabu mbili za Malaysia ambazo zinawataka Bossou na Coutinho.
Aidha, klabu moja nchini Denmark imeonyesha nia ya dhati ya kumnunua mshambuliaji Ngoma na mazungumzo yanaendelea na klabu yake.
Baada ya mazungumzo ya awali, Yanga SC wameziagiza klabu zote hizo ziandike barua rasmi za ofa za kuwataka wachezaji hao.
BIN ZUBEIRY SPORTS- ONLINE inafahamu Yanga SC ipo kwenye mazungumzo na klabu mbili za Malaysia ambazo zinawataka Bossou na Coutinho.
Aidha, klabu moja nchini Denmark imeonyesha nia ya dhati ya kumnunua mshambuliaji Ngoma na mazungumzo yanaendelea na klabu yake.
Baada ya mazungumzo ya awali, Yanga SC wameziagiza klabu zote hizo ziandike barua rasmi za ofa za kuwataka wachezaji hao.