Yanga yamwekea pingamizi Rais wa TFF Wallace Karia

Yanga yamwekea pingamizi Rais wa TFF Wallace Karia

ngara23

JF-Expert Member
Joined
Aug 31, 2019
Posts
15,774
Reaction score
35,994
Yanga kama mbabe wa mpira wa Tanzania imedhamiria Kwa dhati kusafisha pale TFF na bodi ya ligi, Sasa nguvu time imehamia Kwa Wallace Karia

CEO wa Yanga Andre Mtine ameandika barua kwenda kamati ya uchaguzi TFF kumwekea pingamizi Wallace Karia

Yanga wameitaka kamati ya uchaguzi TFF kumwondosha Rais Wallace Karia katika mchakato wa uchaguzi wakiwa na hoja kuu 3

1. Matumizi mabaya ya madaraka Kwa kuchukua endorsement 46 kati ya 47.
Sifa ya kukidhinkugombea Urais ni kupata endorsement 5 tu ila Karia amejisanyia endorsement 46 kati ya 47, akijua wazi kufanya hivo ni kuhujumu mchakato wa uchaguzi, maana wagombea wengine watakwama Kwa kukosa endorsement

2 Kuanza kampeni kabla ya wakati.
Karia amekusanya endorsement 46 kabla ya mchakato hii ni dhahiri alizikusanya mapema kabla ya kipenga cha uchaguzi kupulizwa

3 Karia hapaswi kugombea mihula wa mitatu 3
Sera ya michezo nchini imakataza viongozi kukaa madarakani zaidi mihula miwili
 
Klabu Bingwa ya soka nchini Yanga SC imemuwekea pingamizi Rais wa TFF Wallace Karia na pingamizi hilo limewasilishwa ofisi za TFF saa 9:30 Alasiri ya leo likiwa limesainiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wao (CEO) Andre Ntine.

Yanga SC katika pingamizi lao wanaitaka Kamati ya Uchaguzi chini ya Mwenyekiti wake Wakili Kilomoni Kibamba kumuondoa Karia katika kinyang'anyiro cha Uchaguzi wakiwa na hoja Kuu 3

1. Matumizi mabaya ya madaraka kwa kuchukua endorsement 46 Kati ya 47

2. Kuanza kampeni kabla ya muda kwa kukusanya endorsement 46 kabla ya tangazo la Uchaguzi kutolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF.

3. Wanapinga Karia kugombea mara ya 3 wakisema ni kinyume na sera ya michezo nchini ambayo inataka vyama vya michezo viongozi wake kukaa madarakani kwa vipindi 3 vya miaka mitatu mitatu au vipindi 2 vya miaka minne minne.

Bin Kazumari imepata taarifa hizi kutoka kwenye chanzo cha uhakika ndani ya Shirikisho na Kamati ya Uchaguzi.

BIN KAZUMARI MTIPA (The voice of the voiceless)
 
Klabu Bingwa ya soka nchini Yanga SC imemuwekea pingamizi Rais wa TFF Wallace Karia na pingamizi hilo limewasilishwa ofisi za TFF saa 9:30 Alasiri ya leo likiwa limesainiwa na Afisa Mtendaji Mkuu wao (CEO) Andre Ntine.

Yanga SC katika pingamizi lao wanaitaka Kamati ya Uchaguzi chini ya Mwenyekiti wake Wakili Kilomoni Kibamba kumuondoa Karia katika kinyang'anyiro cha Uchaguzi wakiwa na hoja Kuu 3

1. Matumizi mabaya ya madaraka kwa kuchukua endorsement 46 Kati ya 47

2. Kuanza kampeni kabla ya muda kwa kukusanya endorsement 46 kabla ya tangazo la Uchaguzi kutolewa na Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi ya TFF.

3. Wanapinga Karia kugombea mara ya 3 wakisema ni kinyume na sera ya michezo nchini ambayo inataka vyama vya michezo viongozi wake kukaa madarakani kwa vipindi 3 vya miaka mitatu mitatu au vipindi 2 vya miaka minne minne.

Bin Kazumari imepata taarifa hizi kutoka kwenye chanzo cha uhakika ndani ya Shirikisho na Kamati ya Uchaguzi.

BIN KAZUMARI MTIPA (The voice of the voiceless)
Engineer anataka urais nini🤣🤣🤣🤣
 
Karia amefanya mazuri kipindi chake ila ifikie mahali apumzike kwa heshima atakumbukwa akiendelea kung'ang'ania atatoka kwa aibu kama Raisi wa zamani wa CAF issa hayatou au Raisi wa zamani wa FIFA Sepp Blater
Huyu karia acha yanga wamwendeshe watakavyo yote kayataka yeye,mke wake kapewa ajira na gsm ule ulikua mtego mkubwa sana ,karuhusu gsm adhamini timu nane .
Hapo hana ujanja na watadili nae sana .
Safar hii akichomoka na kuupata huu urais nadhan atajifunza kuwakazia yanga vilivyo na kuondoa janja janja za hao jamaa
 
Back
Top Bottom