Yanga na Simba (Sunderland) HAZIKUPIGANIA Uhuru

Yanga na Simba (Sunderland) HAZIKUPIGANIA Uhuru

Mohamed Said

JF-Expert Member
Joined
Nov 2, 2008
Posts
22,454
Reaction score
32,980

View: https://youtu.be/msgve8ZwfHE?si=U_4RF703Qpe3nSpU

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake.

Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika.

Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion.

Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie.

Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000.

Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa.

Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama.

Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo.

Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7, Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Faiz Mafungo kadi nambari 24; Iddi Tosiri kadi nambari 25.

Hizi kadi za TANU kwa kuwa zilikuwa za rangi ya kijani washabiki wa Yanga wakajinasibisha na TANU wakidai TANU ni Yanga na ni chama chao.

Bahati mbaya Sunderland wao wakivaa rangi nyekundu na rangi nyekundu ni rangi ya bendera ya Uingereza.

Club ya mpira iliyopigania uhuru wa Tanganyika ni Young New Strong Football Club kutoka Tabora.

Juhudi za kuihuisha TANU zilikuja mwaka 1955 mwaka mmoja baadae kupitia Young New Strong Football Club - kilabu ya kandanda iliyoanzishwa miaka mingi nyuma ambayo ilikuwa maarufu pale mjini.

Wanachama wa kilabu hiyo baadhi yao ndiyo walikuwa waasisi wa African Association mwaka wa 1945, mashuhuri miongoni mwao walikuwa Fundi Mhindi na Maulidi Kivuruga.

Mwenyekiti wa kilabu hiyo alikuwa Juma Mrisho, mcheza kandanda mashuhuri kwa siku zile.

Shaaban Mohamed Silabu na Bilali Rehani Waikela walikuwa Katibu na Naibu Katibu.

Mzee Waikela ndiye aliyenisomesha historia hii.
 
huyu ; Dome Okochi ni nani mzee wangu? maana wajaluo wa tanzania ni wachache sana na kwa kipindi hicho sifikirii kama kulikuwa na wajaluo wa hapa tanganyika walioweza kutoka Mara kuja dar kupambana na waingereza
 
huyu ; Dome Okochi ni nani mzee wangu? maana wajaluo wa tanzania ni wachache sana na kwa kipindi hicho sifikirii kama kulikuwa na wajaluo wa hapa tanganyika walioweza kutoka Mara kuja dar kupambana na waingereza
DOME OKOCHI BUDOHI "MAU MAU" NDANI YA TANU?

Kadi ya TANU ya Dome Budohi ni no. 6.

Dome Budohi alikuwa Mluya kutoka Kenya lakini alikuwa mwanachama na kiongozi wa TAA na hivi ndivyo alivyoweza kupata kadi hiyo no. 6.

Mimi nikimfahamu katika utoto wangu kwa jina la Dickson alipokuwa akija kwetu na kuingiliana sana na wazee wangu.

Pamoja na yeye walikuwa Wakenya wawili ambao wote niliwafahamu kwa majina yao ya kwanza tu, Maxwell na Martin.

Haukupita muda mrefu toka TANU iundwe Dome Budohi alikamatwa pamoja na Wakikuyu wengi waliokuwa Tanganyika kwa tuhuma za kuhusishwa na Mau Mau.

Wengi wa hawa Wakikuyu waliotiwa mbaroni walikuwa wafanya biashara Mwanza na sehemu nyingine ya Kanda ya Ziwa.

Martin alirudi Kenya lakini Maxwell alibaki Tanzania na mimi nilikuwa nikikutananae hadi katika miaka ya 1980.

Mara ya mwisho tulionana Mtaa wa Mafia na tulipiga picha pamoja.

Picha yangu na Mzee Maxwell hiyo hapo chini.

Ilikuwa Maxwell ndiye aliyefanya juhudi ya kunikutanisha na Dome Budohi Nairobi mwaka wa 1972 alipoona nataka sana kujua yale yaliyokuwapo Mtaa wa Kipata katika miaka ile ya kupigania uhuru.

Maxwell akiniambia kuwa Dome Budohi alikuwa mstari wa mbele katika TANU hadi mwaka wa 1955 aliposalitiwa na Martin kupitia barua iliyotoka Kenya kuja kwa Budohi barua ambayo ilimuhusisha na Mau Mau.

Budohi alikuwa akifanya kazi katika duka la muziki la Assanand lililokuwa Ring Street (sasa Mtaa wa Jamhuri) na alikuwa mmoja wa vijana wanamuziki akipiga drums katika Skylarks Band iliyokuwa ikiongozwa na Ally Sykes.

Martin alikuwa akipiga trumpet katika bendi hiyo iliyokuwa maarufu kwa vijana katika miaka ile ya 1950.

Budohi pia alikuwa muigizaji wa senema na aliigiza senema moja, "Mgeni Mwema," pamoja na Rashid Mfaume Kawawa.

Juu ya haya yote hawa vijana pamoja ya kuwa walikuwa hawapunguki katika kumbi mbili maarufu za Dar es Salaam ya wakati ule, Alexander na Arnautoglo walikuwa wapigania uhuru.

Nakumbuka kama.jana vile mazungumzo yangu na Dome Budohi nyumbani kwake Ruiru na kisha Ngei Estate alipohamia baadae.

Aliniambia kuwa alikitahidi sana kutafuta kuonana na Julius Nyerere wakumbushane enzi zao kila alipokuwa akienda Nairobi lakini hakufanikiwa.

Dome Budohi hakurudi tena Dar es Salaam hadi alipofariki.

Nimeshindwa kabisa kujua kwa uhakika kama Martin alikuwa kachero katika Special Branch au vipi.

Lakini itoshe tu kuwa katika kipindi hiki tunachokizungumza ilikuja kunidhihirikia baadae sana baada ya uhuru kuwa Ali Mwinyi Tambwe Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na mtu karibu sana na Abdul Sykes Secretary wa TAA alikuwa kachero wa Special Branch pamoja na Alexander Tobias.

Alexander Tobias alikuwa ameajiriwa na TAA mwaka wa 1950 kama Executive Secretary.

Picha: Kambi ya Mau Mau Kenya.

Itaendelea...
 

View: https://youtu.be/msgve8ZwfHE?si=U_4RF703Qpe3nSpU

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake.

Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika.

Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion.

Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie.

Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000.

Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa.

Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama.

Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo.

Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7, Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Faiz Mafungo kadi nambari 24; Iddi Tosiri kadi nambari 25.

Hizi kadi za TANU kwa kuwa zilikuwa za rangi ya kijani washabiki wa Yanga wakajinasibisha na TANU wakidai TANU ni Yanga na ni chama chao.

Bahati mbaya Sunderland wao wakivaa rangi nyekundu na rangi nyekundu ni rangi ya bendera ya Uingereza.

Club ya mpira iliyopigania uhuru wa Tanganyika ni Young New Strong Football Club kutoka Tabora.

Juhudi za kuihuisha TANU zilikuja mwaka 1955 mwaka mmoja baadae kupitia Young New Strong Football Club - kilabu ya kandanda iliyoanzishwa miaka mingi nyuma ambayo ilikuwa maarufu pale mjini.

Wanachama wa kilabu hiyo baadhi yao ndiyo walikuwa waasisi wa African Association mwaka wa 1945, mashuhuri miongoni mwao walikuwa Fundi Mhindi na Maulidi Kivuruga.

Mwenyekiti wa kilabu hiyo alikuwa Juma Mrisho, mcheza kandanda mashuhuri kwa siku zile.

Shaaban Mohamed Silabu na Bilali Rehani Waikela walikuwa Katibu na Naibu Katibu.

Mzee Waikela ndiye aliyenisomesha historia hii.

Mzee nilifurahi sana siku ulipoandika kuhusu Etohola Yao Kwasy JESHI na Pacome Zouzoua PEDOU.Mlikuwa mmekutana airport ulikosindikizwa na kijana wako.Hii ilikuwa baada ya KOLO kula kono la nyani. Nakushukuru sana.
 
Mzee nilifurahi sana siku ulipoandika kuhusu Etohola Yao Kwasy JESHI na Pacome Zouzoua PEDOU.Mlikuwa mmekutana airport ulikosindikizwa na kijana wako.Hii ilikuwa baada ya KOLO kula kono la nyani. Nakushukuru sana.
Bali...
Ahsante.
Mimi ndiye nikisindikiza.
 
Wakina sykes wamekula mema sana ya nchi hii

Ova
 

View: https://youtu.be/msgve8ZwfHE?si=U_4RF703Qpe3nSpU

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake.

Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika.

Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion.

Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie.

Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000.

Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa.

Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama.

Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo.

Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7, Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Faiz Mafungo kadi nambari 24; Iddi Tosiri kadi nambari 25.

Hizi kadi za TANU kwa kuwa zilikuwa za rangi ya kijani washabiki wa Yanga wakajinasibisha na TANU wakidai TANU ni Yanga na ni chama chao.

Bahati mbaya Sunderland wao wakivaa rangi nyekundu na rangi nyekundu ni rangi ya bendera ya Uingereza.

Club ya mpira iliyopigania uhuru wa Tanganyika ni Young New Strong Football Club kutoka Tabora.

Juhudi za kuihuisha TANU zilikuja mwaka 1955 mwaka mmoja baadae kupitia Young New Strong Football Club - kilabu ya kandanda iliyoanzishwa miaka mingi nyuma ambayo ilikuwa maarufu pale mjini.

Wanachama wa kilabu hiyo baadhi yao ndiyo walikuwa waasisi wa African Association mwaka wa 1945, mashuhuri miongoni mwao walikuwa Fundi Mhindi na Maulidi Kivuruga.

Mwenyekiti wa kilabu hiyo alikuwa Juma Mrisho, mcheza kandanda mashuhuri kwa siku zile.

Shaaban Mohamed Silabu na Bilali Rehani Waikela walikuwa Katibu na Naibu Katibu.

Mzee Waikela ndiye aliyenisomesha historia hii.

Assalamu alaykum sheikh!Kwa maana hiyo ni kwamba Yanga hii ya leo ilitokana na hiyo Young New Strong Football Club ya Tabora?.
 

View: https://youtu.be/msgve8ZwfHE?si=U_4RF703Qpe3nSpU

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake.

Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika.

Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion.

Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie.

Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000.

Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa.

Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama.

Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo.

Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7, Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Faiz Mafungo kadi nambari 24; Iddi Tosiri kadi nambari 25.

Hizi kadi za TANU kwa kuwa zilikuwa za rangi ya kijani washabiki wa Yanga wakajinasibisha na TANU wakidai TANU ni Yanga na ni chama chao.

Bahati mbaya Sunderland wao wakivaa rangi nyekundu na rangi nyekundu ni rangi ya bendera ya Uingereza.

Club ya mpira iliyopigania uhuru wa Tanganyika ni Young New Strong Football Club kutoka Tabora.

Juhudi za kuihuisha TANU zilikuja mwaka 1955 mwaka mmoja baadae kupitia Young New Strong Football Club - kilabu ya kandanda iliyoanzishwa miaka mingi nyuma ambayo ilikuwa maarufu pale mjini.

Wanachama wa kilabu hiyo baadhi yao ndiyo walikuwa waasisi wa African Association mwaka wa 1945, mashuhuri miongoni mwao walikuwa Fundi Mhindi na Maulidi Kivuruga.

Mwenyekiti wa kilabu hiyo alikuwa Juma Mrisho, mcheza kandanda mashuhuri kwa siku zile.

Shaaban Mohamed Silabu na Bilali Rehani Waikela walikuwa Katibu na Naibu Katibu.

Mzee Waikela ndiye aliyenisomesha historia hii.

This has something to do with the fact that wewe ni kolo. Ubaya ubwela
 
DOME OKOCHI BUDOHI "MAU MAU" NDANI YA TANU?

Kadi ya TANU ya Dome Budohi ni no. 6.

Dome Budohi alikuwa Mluya kutoka Kenya lakini alikuwa mwanachama na kiongozi wa TAA na hivi ndivyo alivyoweza kupata kadi hiyo no. 6.

Mimi nikimfahamu katika utoto wangu kwa jina la Dickson alipokuwa akija kwetu na kuingiliana sana na wazee wangu.

Pamoja na yeye walikuwa Wakenya wawili ambao wote niliwafahamu kwa majina yao ya kwanza tu, Maxwell na Martin.

Haukupita muda mrefu toka TANU iundwe Dome Budohi alikamatwa pamoja na Wakikuyu wengi waliokuwa Tanganyika kwa tuhuma za kuhusishwa na Mau Mau.

Wengi wa hawa Wakikuyu waliotiwa mbaroni walikuwa wafanya biashara Mwanza na sehemu nyingine ya Kanda ya Ziwa.

Martin alirudi Kenya lakini Maxwell alibaki Tanzania na mimi nilikuwa nikikutananae hadi katika miaka ya 1980.

Mara ya mwisho tulionana Mtaa wa Mafia na tulipiga picha pamoja.

Picha yangu na Mzee Maxwell hiyo hapo chini.

Ilikuwa Maxwell ndiye aliyefanya juhudi ya kunikutanisha na Dome Budohi Nairobi mwaka wa 1972 alipoona nataka sana kujua yale yaliyokuwapo Mtaa wa Kipata katika miaka ile ya kupigania uhuru.

Maxwell akiniambia kuwa Dome Budohi alikuwa mstari wa mbele katika TANU hadi mwaka wa 1955 aliposalitiwa na Martin kupitia barua iliyotoka Kenya kuja kwa Budohi barua ambayo ilimuhusisha na Mau Mau.

Budohi alikuwa akifanya kazi katika duka la muziki la Assanand lililokuwa Ring Street (sasa Mtaa wa Jamhuri) na alikuwa mmoja wa vijana wanamuziki akipiga drums katika Skylarks Band iliyokuwa ikiongozwa na Ally Sykes.

Martin alikuwa akipiga trumpet katika bendi hiyo iliyokuwa maarufu kwa vijana katika miaka ile ya 1950.

Budohi pia alikuwa muigizaji wa senema na aliigiza senema moja, "Mgeni Mwema," pamoja na Rashid Mfaume Kawawa.

Juu ya haya yote hawa vijana pamoja ya kuwa walikuwa hawapunguki katika kumbi mbili maarufu za Dar es Salaam ya wakati ule, Alexander na Arnautoglo walikuwa wapigania uhuru.

Nakumbuka kama.jana vile mazungumzo yangu na Dome Budohi nyumbani kwake Ruiru na kisha Ngei Estate alipohamia baadae.

Aliniambia kuwa alikitahidi sana kutafuta kuonana na Julius Nyerere wakumbushane enzi zao kila alipokuwa akienda Nairobi lakini hakufanikiwa.

Dome Budohi hakurudi tena Dar es Salaam hadi alipofariki.

Nimeshindwa kabisa kujua kwa uhakika kama Martin alikuwa kachero katika Special Branch au vipi.

Lakini itoshe tu kuwa katika kipindi hiki tunachokizungumza ilikuja kunidhihirikia baadae sana baada ya uhuru kuwa Ali Mwinyi Tambwe Katibu wa Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika na mtu karibu sana na Abdul Sykes Secretary wa TAA alikuwa kachero wa Special Branch pamoja na Alexander Tobias.

Alexander Tobias alikuwa ameajiriwa na TAA mwaka wa 1950 kama Executive Secretary.

Picha: Kambi ya Mau Mau Kenya.

Itaendelea...
Mzee tumsifu Yesu Kristo hakuna picha uliyoweka
 
Mzee tumsifu Yesu Kristo hakuna picha uliyoweka
1752771259434.jpeg
 
Hakika najifunza mambo mengi ya Historia yetu kupitia kwako Mzee wangu namuomba Mwenyezi Mungu akuzidishie badala na Umri mrefu ili uendelee kutupa Elimu sisi vijana wako
 
Hakika najifunza mambo mengi ya Historia yetu kupitia kwako Mzee wangu namuomba Mwenyezi Mungu akuzidishie badala na Umri mrefu ili uendelee kutupa Elimu sisi vijana wako
Wa Ukae,
Amin kwa sote.
 
Walikuwa njema,kizazi,watoto zao walibweteka wakajisahau kama unavyoona familia za kina rupia nao

Ova
Mrangi,
Tuanze na Abbas Sykes:
ABBAS SYKES (1929 - 2021) SEHEMU YA TATU: KING'S COLLEGE BUDO SHULE MOJA NA KABAKA EDWARD MUTESA WA UGANDA 1940s
Siku moja katika mazungumzo na Balozi Sykes akaniambia kuwa yeye baba yake alimtoa Kitchwelle Boys Government School na kumpeleka Kampala Uganda kwa ajili ya kupata elimu.

Balozi anasema yeye hakuwa anajua ni shule gani baba yake alikuwa anataka kumpeleka lakini walipokuwa Nairobi wakiwa pale hotelini wakisubiri safari ya kwenda Kampala baba yake akakutana na jamaa wa Kinubi na katika maongezi baba yake akawaeleza kuwa alikuwa katika safari anaelekea Uganda kumpeleka kijana wake shule.

Basi mmoja wao katika wale jamaa wa Kinubi akamwambia Kleist kuwa shule nzuri sana ni King's College Budo kama ana uwezo na itakuwa vyema kama atampeleka mtoto wake shule hiyo.

Hapo King's |College Budo ndipo Abbas Sykes ailipokuja kusoma na Freddie Mutesa ambae baadae akajakuwa Kabaka wa Buganda na Rais wa Uganda mwaka 1962 Uganda ilipopata uhuru.

Balozi Sykes anakumbuka kumuona mama yake Freddie Mutesa akiwa kavaa yale magauni ya Kiganda akija shule kumtembelea mwanae na jinsi shule nzima ilivyokuwa ikitetemeka kwa ujio wa bi. mkubwa yule kwani Freddie ndiye aliyekuwa akitegemewa kuwa Kabaka wa Uganda.

Wote Abbas Sykes na Freddie Mutesa katika utawala wa kikoloni wakahusika kikamilifu katika kupigania uhuru wa nchi zao.

Inasikitisha kuwa kutoka miaka ile ya 1940 wazalendo hawa hawakupata tena kuonana wakati nchi zao washazikombboa kutoka kwa Muingereza na labda kwa kuwa Kabaka Mutesa alipunduliwa mwaka wa 1966 na kwenda kuishi uhamishoni Uingereza ambako alifariki mwaka wa 1969.

Miaka hiyo Abbas Sykes tayari alikuwa kwenye ubalozi wa Tanzania Ufaransa na Canada.

Hii shule King's College Budo ina sifa ya pekee katika shule za Afrika ya Mashariki kwani viongozi wengi na watu mashuhuri wamesoma hapo kutoka Uganda kwenyewe, Kenya hadi Nyasaland na wenyewe wanajiita Budoians.

Hii ni ''club,'' pekee ya wasomi kama Yusuf Lule, Godfrey Binaisa na Charles Njonjo kwa kutaja majina maarufu katika siasa za Afrika ya Mashariki.

Balozi Sykes anamkumbuka baba yake kwa mapenzi makubwa sana.

Balozi mara nyingi akinambia kuwa, ''Sisi baba yetu alitujengea msingi mzuri sana wa maisha na alipofariki aliacha jina kubwa la ukoo wetu.

Hakuna mahali ambako baba yetu hakuacha alama yake kuanzia kwenye siasa, biashara na katika dini ya Kiislam hasa katika kuwasomesha watoto wa Kiislam wake kwa waume.

Yeye na wenzake akina Ali Jumbe Kiro walijenga ile shule ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.

Mungu akajaalia kuwa Bwana Abdul baada ya kifo cha baba yetu mwaka wa 1949 yeye akavaa viatu vya baba yake na vikamuenea vizuri sana ndani ya TAA hadi kuasisi TANU mwaka wa 1954.

Hapa ikawa tumekuwapo katika African Association mwaka wa 1929 na tukawepo katika kuunda TANU mwaka wa 1954.

Balozi akipenda sana kunitania kwa kuniita, ''Yaa Mohamed, unaiona Sykes dynasty?''

Nakumbuka siku nilipomtembelea baada ya Kleist Abdul Sykes kuchaguliwa kuwa Mayor wa Dar es Salaam.

''Unajua Mohamed somo yake alikuwa Mwafrika wa pili kuchaguliwa katika board ya Dar es Salaam Municipal Council kwa hiyo Kleist kafuata nyayo za babu yake,'' Balozi aliniambia kwa furaha.

Mwafrika wa kwanza kuchaguliwa katika board hiyo alikuwa Juma Mwindadi.

1752791385934.png

Mahojiano na Balozi Sykes nyumbani kwake Sea View kwa ajili ya kipindi cha TV 2012

1752791043578.png

Juma Mwindadi
 

View: https://youtu.be/msgve8ZwfHE?si=U_4RF703Qpe3nSpU

Ally Sykes ndiye aliyechora kadi ya TANU na kuchagua rangi na nembo yake.

Rangi alizochagua zilikuwa, nyeusi kuwakilisha taifa la Kiafrika na kijani ardhi ya Tanganyika.

Mfano wa kadi ya TANU ulitokana na kadi yake ya Tanganyika Legion.

Baada ya kumaliza kuichora ile kadi, aliwaendea Tanganyika Standard Newspapers ili wamchapishie.

Kutoka mfukoni mwake mwenyewe alichapisha kadi 1000 za kwanza na akitumia fedha za TAGSA alichapisha kadi nyingine 2000.

Kadi nambari 1 ilitolewa na Ally Sykes kwa rais wa TANU, Julius Kambarage Nyerere na Ally aliweka sahihi yake kama afisa aliyeitoa.

Ilipendekezwa kwamba kadi chache za mwanzo lazima zipigwe mnada na fedha zitakazokusanywa zitiwe kwenye hazina ya chama.

Abdulwahid, Ally, Dossa Aziz, Rupia na wengine walipanda dau kununua kadi hizo.

Ally alimshinda kaka yake Abdulwahid kwa bei akapata kadi ya TANU nambari 2; Abdulwahid alipewa kadi nambari 3; Dossa Aziz kadi nambari 4; Phombeah kadi nambari 5; Dome Okochi, mmoja wa wale wazalendo kutoka Kenya katika TANU alipata kadi nambari 6 na Rupia kadi nambari 7, Bibi Titi kadi nambari 16; Iddi Faiz Mafungo kadi nambari 24; Iddi Tosiri kadi nambari 25.

Hizi kadi za TANU kwa kuwa zilikuwa za rangi ya kijani washabiki wa Yanga wakajinasibisha na TANU wakidai TANU ni Yanga na ni chama chao.

Bahati mbaya Sunderland wao wakivaa rangi nyekundu na rangi nyekundu ni rangi ya bendera ya Uingereza.

Club ya mpira iliyopigania uhuru wa Tanganyika ni Young New Strong Football Club kutoka Tabora.

Juhudi za kuihuisha TANU zilikuja mwaka 1955 mwaka mmoja baadae kupitia Young New Strong Football Club - kilabu ya kandanda iliyoanzishwa miaka mingi nyuma ambayo ilikuwa maarufu pale mjini.

Wanachama wa kilabu hiyo baadhi yao ndiyo walikuwa waasisi wa African Association mwaka wa 1945, mashuhuri miongoni mwao walikuwa Fundi Mhindi na Maulidi Kivuruga.

Mwenyekiti wa kilabu hiyo alikuwa Juma Mrisho, mcheza kandanda mashuhuri kwa siku zile.

Shaaban Mohamed Silabu na Bilali Rehani Waikela walikuwa Katibu na Naibu Katibu.

Mzee Waikela ndiye aliyenisomesha historia hii.

Haya matimu kumbe utapeli yalianza zamani sana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom