mwangalingimungu
JF-Expert Member
- Jul 29, 2013
- 1,301
- 733
Ushabiki, unazi na siasa tuweke kando, kisha tujiulize: (1) Ukatibu Mkuu Yanga unahitaji kwanza uanachama? Kama jawabu ni ndio, na mwajiriwa si mwanachama, hapo kuna kasoro. (2) kwa mujibu wa katiba ya Yanga, nani ana jukumu la kuajiri? Kama walioajiri hawana mamlaka hayo kikatiba, hapo kuna kasoro (3) kwa mujibu wa taratibu za uajiri wa klabu ya Yanga, kuna ulazima wa nafasi kutangazwa? Kama ulazima huo upo na haikutangazwa, hapo kuna kasoro (4) uzoefu wa ujazaji nafasi kama hizo ndani ya Yanga unaelekeaje, kwa kuangalia na akina Sendeu na Mwalusako. Taratibu hizo zilifuatwa? Kama hazikufuatwa, wazee na wanachama walilalamika? (5) wakati wote wa kujadili mada hii muhimu ni kuzingatia kwamba kinachopingwa si kuajiriwa Mkenya, bali iwapo taratibu zilifuatwa.