Labani og
JF-Expert Member
- Sep 15, 2020
- 15,774
- 24,209
SIKU moja tu tangu Kamati ya Kusimamia na Kuendesha Ligi ya Bodi ya Ligi (TPLB) kutangaza kumfungia kiungo wa Yanga, Khalid Aucho kwa mechi tatu na kumlima faini ya Tsh 500,000 kwa kosa la utovu wa nidhamu, mabosi wa klabu hiyo wapo kwenye mchakato wa kukata rufaa.
Akizungumza na Mwanaspoti, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rodgers Gumbo alisema uongozi haujakubaliana na uamuzi huo wa kamati hiyo ya bodi ukiona kiungo huyo amehukumiwa mara mbili.
Gumbo alisema wanalazimika kutaka rufaa kutokana na kuwa waliwahi kuiandikia Bodi ya Ligi siku za nyuma juu ya beki wa Simba, Henock Inonga aliyefanya kosa kama hilo, lakini walijibiwa mwamuzi alishachukua hatua ndani mchezo kwa kuonyeshwa kadi ya njano, ila safari hii Aucho hilo limesahaulika.
NB hawajamaliza Wana Yanga ......mlete aucho
Akizungumza na Mwanaspoti, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rodgers Gumbo alisema uongozi haujakubaliana na uamuzi huo wa kamati hiyo ya bodi ukiona kiungo huyo amehukumiwa mara mbili.
Gumbo alisema wanalazimika kutaka rufaa kutokana na kuwa waliwahi kuiandikia Bodi ya Ligi siku za nyuma juu ya beki wa Simba, Henock Inonga aliyefanya kosa kama hilo, lakini walijibiwa mwamuzi alishachukua hatua ndani mchezo kwa kuonyeshwa kadi ya njano, ila safari hii Aucho hilo limesahaulika.
NB hawajamaliza Wana Yanga ......mlete aucho