nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,860
- 5,803
Thursday, 04 April 2013 17:33Written by Mwandishi wetu
Mchoro wa Uwanja wa kisasa wa Klabu ya
Yanga
Mchoro wa Uwanja wa Kaunda utakavyo kuwa ndani
Dar es Salaam
WAKATI viongozi wa Simba wakiendelea kurumbana wanachama wa klabu hiyo juu ya nani anastahili kuwa kiongozi halali bila kujali kuwa hali hiyo inasababisha maendelea mabovu ya timu hiyo,Watani wao wajadi Yanga wameanza kuonyesha mikakati dhabidi ya ujenzi wa uwanja wa kisasa.
Yanga ambayo ni Mabingwa Kombe la Kagame na vinara wa Ligi Kuu Tanzania Bara imefikia hatua hiyo baada ya Kampuni ya Beinjing Cosntruction Engineering Group (BCEG) kutoka nchini China, ambayo mwishoni mwa mwaka jana ilisaini makubaliano ya upembuzi yakinifu juu ya ujenzi wa uwanja wa mpira wa miguu (Kaunda stadium) leo imewasilisha michoro na makadirio ya bajeti ya ujenzi wa Uwanja mpya eneo la Jangwani (Kaunda Stadium).
Kaimu meneja wa kampuni ya BCEG Zhang Chengwei David amesema upembuzi yakinifu umekamilika kuhusiana na suala la ujenzi wa uwanja wa mpya wa klabu ya Yanga eneo la jangwani ambapo taratibu za makadirio na michoro imekamilika tayari na leo kuwasilishwa kwa uongozi wa klabu ya Yanga.
Zhang alisema kwamba kampuni yao BCEG wana uzoefu wa ujenzi wa viwanja sehemu mbali mbali duniani, na mfano mzuri ni ujenzi wa uwanja mpya wa Taifa jijini Dar es salaam ambao ulikua mkubwa kuliko viwanja vyote barani Afrika kabla ya kujengwa kwa uwanja mpya wa nchini Afrika Kusini (Soccer city) uliotumika kwa ajili ya fainali za kombe la dunia 2010.
Aidha Zhang aliendelea kusema pia kwa sasa wanajenga uwanja wa Uhuru Stadium (jirani na uwanja wa Taifa ) ambapo ujenzi wake ulianza mwaka jana mwezi Aprili na wanatarajia kuukamilisha mapema mwaka huu, huku ukiboreshwa kwa kufunikwa uwanja mzima na kuweka viti ambayo vitaweza kubeba watazamaji 20,000 na utaanza Julai mwaka huu.
Kwa mujibu wa makubaliano ya kampuni ya BCEG na klabu ya Yanga ujenzi wa uwanja mpya wa Kaunda stadium utachukua muda wa miaka miwili, kuanzia utakapoanza ujenzi wake ambapo unatazamiwa kuanza mwezi wa Julai 2013 kulingana na kukamilika kwa taratibu za ujenzi kwa kampuni hiyo.
Kaunda stadium utakuwa na uwezo wa kuchukua watazamaji 40,000, waliokaa kwenye viti, huku ukiwa na sehemu za maegesho ya magari, sehemu ya watu maarufu (VIP) hostipali, hoteli na hosteli, eneo la waandishi wa habari, eneo la walemavu na huduma zote muhimu zinazopatikana katika viwanja vya michezo.