Yanga anafungwa leo

Huyu aliyesema yanga anafungwa tafadhali niachieni Mimi Nina kazi nae
 
Wakuu simba sc anamfunga mtani wake leo, sina maneno mengi 1-2 ft

Mengine yanayobaki ni ya nje ya uwanja labda kama yanaweza leta shida. Ila ndani ya uwanja, simba nampa benefit of doubt kuliko chama langu Yanga
 
Mechi ya leo imenifundisha vitu vingi sana kuhusu football. Kwakifupi Simba iliimarika kwa ujio wa Anicet Oura na Libase Gueye ukiachilia mbali udhaifu wa YANGA round ya pili ligi iliyomalizika. Ukiweza kuwadhibiti hao jamaa wawili basii umemalizana Simba. Game ya Chama na Mpanzu inategemea zaidi hao jamaa wawili wameamkaje ndo maana Mpanzu alikuepo toka mwanzo lakini bado Simba walipasuka sana kwa Yanga adi inaonekana Mpanzu kama kiwango kimeshuka. Kuanzia January ubora wa Simba kwa % kubwa uliamuliwa zaidi na hao jamaa wawili hapo Oura na Libase. Leo wamechezewa sana undava na Yanga walikua wanafanya sana pressing kila jamaa wakikamata mpira tofauti na ukiwachia sana nafasi za kutembea lazima wakudhuru. Anyways Simba bado ni bora hata ni matokeo ya mechi moja tu. Azam pia kasajili. Ila Yanga timu ikipata muunganiko patakua pa moto sana. Nje ya mada kidogo, kuna kitu nimekiona toka mechi ya Yanga Day ni kama Alan Okelo anafukuzwa kimya kimya pale YANGA nini shida kwa bwanamdogo mbona kama ni mapema sana? Otherwise YANGA BINGWA πŸ’ͺπŸ”₯
 
Otherwise YANGA BINGWA πŸ’ͺπŸ”₯
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…