PostGE2025 Yaliyotokea Oktoba 29 tusingependa yajirudie tena. Tuweke hoja mezani

Conversations and stories after Tanzania's 2025 General Elections

Home tutor Dar

Senior Member
Joined
Feb 23, 2025
Posts
114
Reaction score
139
Watanzania wenzangu,
Tukio la Oktoba 29 lilileta maumivu, sintofahamu na migawanyiko ambayo hatutamani ijirudie kamwe. Amani ya nchi yetu ni hazina kubwa, na kama taifa, tunapaswa kutafuta njia mbadala, zenye hekima na utulivu ili kufikia makubaliano kwa hoja, si chokochoko.

Ndugu zangu, hebu tukusanye hoja zetu.

Je, ni mambo gani wananchi tungependa serikali iyafanyie kazi?
πŸ‘‰ Elimu?
πŸ‘‰ Ajira?
πŸ‘‰ Afya?
πŸ‘‰ Haki na usawa mbele ya sheria?
πŸ‘‰ Hali ya uchumi na maisha?
πŸ‘‰ Uhuru wa mawazo na kujieleza?
πŸ‘‰ Maendeleo ya vijana na wanawake?
πŸ‘‰ Uwajibikaji wa viongozi?

Tafadhali changia hoja yako kwa heshima.
Huenda kwa namna moja au nyingine zikawa mwanzo wa maridhiano na mageuzi chanya.

Tukumbuke: Nchi ni yetu sote.Maridhiano ni hatua ya hekima. Tufike mahali tunajenga badala ya kubomoa.

✍🏽 Karibu kwenye mjadala wa busara.
 
Hayo yote yatawezekana kuzungumzika Endapo Serikali Haramu na Batili ikijiuzuru!

Hii Serikali haijachaguliwa na Wananchi,Imewaua wananchi wake Ili ijimilikishe madaraka!
 
M-tag kwanza bibi mashavu hapa chini ili tumfikishie ujumbe
 
Hakuna mazungumzo yoyote mezani ,Wauaji wakiwa MADARAKANI.

Kama umetumwa kupima upepo, kawaambie, Kila kitu kimekamilika, Dec 9 wasithubutu hata mara Moja kupiga Risasi hata sisimizi.


Dec 9 Risasi yoyote Kwa Mwandamanaji italipwa Kwa Risasi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…