nexus white
JF-Expert Member
- Oct 14, 2011
- 210
- 81
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kusababisha watu kushangaa ni pale usalama wa taifa kutaka kufanya mambo yaliyoshindwa kuzuilika kwa wanachuo na wananchi wengine wa kawaida waliohudhuria mdahalo chuoni hapo. Na hii ni baada ya mgeni mwalikwa ambaye ni naibu waziri January Makamba kusema kwamba hoja katika mdahalo huo zitakuwa ni ni muundo wa serikali na hoja nyingine ni mambo yahusuyo sayansi na teknolojia
Ndipo wanachuo wakaanza kuongea kwa kutoa vielelezo thabiti ili kutetea hoja zao, ndipo mkuu wa mkoa Bi Fatuma Mwassa alipoona wanachuo wanatoa hoja za kupinga serikali mbili na zikiwa zimeshiba kwa uthibitisho wao na kwenda kinyume na matarajio yao(mkuu wa mkoa, usalama wa taifa na makamba) ikabidi watake kuwaongoza na ndipo vijana wakakataa na usalama wa taifa kutaka kuwakamata ambapo wanachuo walisema hakuna aliyefanya vurugu wala kutukana hivyo hakamatwi wala kuonewa mtu. Kwa busara za January Makamba ndipo hali ikatulia baada ya kusema hii ni demokrasia na kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake na hapo mkuu wa mkoa na usalama wakawa wapole
katika mdahalo huo pia walikuwepo TBC1 na TBC taifa lakini nashangaa kutokuitoa habari hii
MY TAKE: Huu mjadala wa katiba ni mjadala wa kitaifa hivyo viongozi acheni watu wazungumze ya moyoni cha muhimu wasivunje sheria tu, vyombo vya dola mpo kwa ajili ya usalama na si kuwafundisha watu waseme nini na pia TBC1 acheni kubagua habari
Nitasema kweli daima uongo kwangu mwiko
Nawasilisha
Source: Mimi mwenyewe nilihudhuria
Ndipo wanachuo wakaanza kuongea kwa kutoa vielelezo thabiti ili kutetea hoja zao, ndipo mkuu wa mkoa Bi Fatuma Mwassa alipoona wanachuo wanatoa hoja za kupinga serikali mbili na zikiwa zimeshiba kwa uthibitisho wao na kwenda kinyume na matarajio yao(mkuu wa mkoa, usalama wa taifa na makamba) ikabidi watake kuwaongoza na ndipo vijana wakakataa na usalama wa taifa kutaka kuwakamata ambapo wanachuo walisema hakuna aliyefanya vurugu wala kutukana hivyo hakamatwi wala kuonewa mtu. Kwa busara za January Makamba ndipo hali ikatulia baada ya kusema hii ni demokrasia na kila mtu ana uhuru wa kutoa maoni yake na hapo mkuu wa mkoa na usalama wakawa wapole
katika mdahalo huo pia walikuwepo TBC1 na TBC taifa lakini nashangaa kutokuitoa habari hii
MY TAKE: Huu mjadala wa katiba ni mjadala wa kitaifa hivyo viongozi acheni watu wazungumze ya moyoni cha muhimu wasivunje sheria tu, vyombo vya dola mpo kwa ajili ya usalama na si kuwafundisha watu waseme nini na pia TBC1 acheni kubagua habari
Nitasema kweli daima uongo kwangu mwiko
Nawasilisha
Source: Mimi mwenyewe nilihudhuria