Mr. Django
JF-Expert Member
- Jul 25, 2014
- 1,830
- 2,424
Kumbe lengo lenu la kibwege kiasi hicho! Yaani kumwondoa JPM kwenye headlines za vyombo vya habari!!! Ha aha ahaaaaa...WanaJF.
Tumeona jinsi serikali ya CCM na Jeshi la Polisi walivyohangaika kwa kipindi cha maandalizi ya UKUTA. Ni wazi kwamba kwa kusogeza mbele operesheni hii kutaendelea kuwashughulisha sana mapolisi na maccm kwa kipindi kingine.
Kwa kifupi kufikia hapa tulipo UKUTA imefanikiwa sana sana. Kila siku magazeti yote yalikuwa yanazungumzia UKUTA. Kwa kiasi kikubwa tumeweza kumwondoa JPM kwenye headlines na watanzania wengi wamepata ukweli juu ya hali halisi ya Udikteta na dalili zake alizozionyesha JPM.
Nina uhakika kuruhusu viongozi wa dini na Taasisi mbalimbali za ndani na za kimataifa kujaribu kukutanisha pande hizi mbili kutafungua zaidi uelewa wa watanzania juu ya UKUTA. Na kwa upande wa Pili nia ovu ya kuliingiza Taifa kwenye machafuko inayoonyeshwa na serikali ya awamu ya tano.
Kwa wapenda amani wote duniani wataunga mkono uamuzi huu wa viongozi wetu ambao umedhihirisha nia yetu ya ndani ya ya kulindaa amani ya nchi yetu .
[HASHTAG]#UKUTA[/HASHTAG] ni operesheni endelevu hata sasa tunaendelea nayo. Tutaendelea kujipanga na kufanya maboresho ya mikakati yetu ili mwisho wa yote katiba ya nchi yetu iheshimiwe na kila mtu.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu ibariki CHADEMA.
Mungu ibariki operasheni [HASHTAG]#UKUTA[/HASHTAG].