Yaliyojiri katika M4C Operation Pamoja Daima jijini Arusha

Yaliyojiri katika M4C Operation Pamoja Daima jijini Arusha

Mungi

JF Gold Member
Joined
Sep 23, 2010
Posts
16,975
Reaction score
9,580
Mkutano umeanza muda, ambapo kabla ya mkutano kuhusu OPD Tundu Lissu na Heche walizungumzia uchaguzi wa Sombetini.

Hivi Sasa anazungumza Lissu, anasema Madini ya Tanzanite yapo Arusha lakini siyo ya watanzania, bali ya wamarekani, Gesi ipo Tanzania lakini siyo ya watanzania, Tuna wanyama wengi vivutio lakini siyo mali ya watanzania, mitandao ya mawasiliano ipo Tanzania lakini siyo ya kwetu. Amesema nchi imeuzwa na ccm. Akauliza wananchi kama kila kitu wamepewa wageni tumebakiwa na nini? wananchi wakasema Virobaaaa!!!!

Anaendelea kuzungumza kuwa watanzania tujifunze kusoma alama za nyakati.

attachment.php

Ngusero.jpg
 
Anazungumzia Operation Tokomeza, anasema kabla ya hapo kulikuwa na Operesheni kimbunga, ambapo ilianzishwa na Kikwete baada ya kugombana na Kagame wa Rwanda, hivyo operation kimbunga ilikuwa inawakamata watu wenye asili ya kinyarwanda.
 
tunashukuru kwa updates kamanda, tupia na vipicha ili watu waone tofauti ya OPT na M4C-OPD
 
Operation Tokomeza ilianzishwa baada ya raia kuchoshwa na watawala, wakaona raia wameasi watawala, ndiyo maana rais ametangaza operesheni ya kijeshi.

Jeshi limekatazwa kuingia kwenye shughuli za raia kwasababu wamefundishwa kuua. Unapotumia jeshi kwenye operation Tokomeza unawaambia jeshi kwenda kuua, unapowaambia jeshi waende kwenye operesheni mtwara unawaambia waende wakawaue raia
 
Wewe mungi weka picha ndio uje na hizo hekaya mkuu. Hivi hivi kadaanganye watoto
 
...


....Hii nyomi iliyofurika hapa itasababisha watu wafe kwa pressure !!!!!
 
Miaka ya nyuma wakati wa utawala wa marais waliotangulia hatujawahi kusikia bomu limerushwa makanisani, lakini chini ya utawala huu uliofitinika tumeshuhudia bomu linarushwa kanisani, viongozi wa makanisa wameuawa kanisani. Watu wameuawa makanisani na kwenye mikutano ya kampeni serikali ipo kimya, watu wameuawa soweto, hakuna aliyetoa hata pole, Kamuhanda alitoa amri Daudi Mwangosi auawe halafu akapandishwa cheo, serikali ya aina gani ipo kimya tu.

Yule polisi aliyemwua Daudi Mwangosi alipelekwa mahakamani mara mbili sasahivi yupo Ukerewe anafanya kazi yake ya uaskari
 
Katiba yetu ukiisoma inasema Rais wetu ni amiri jeshi mkuu wa ulinzi na usalama, ukiisoma katiba ya zanzibar inasema rais wa zanzibar ni mkuu wa majeshi..... sasa tuna amiri jeshi wakuu wangapi?
 
Wazanzibar hawataki Muungano na ukweli ndiyo huu.
wiki iliyopita ccm ya upande wa kiteto iliwashawishi wafugaji wakawaue wakulima kwasababu wamevamia ardhi yetu, huku akina ndugai wanawashawishi wakulima wakawaue wafugaji..... ccm wamechoka hawana fikra, wamebaki kututengenezea vita kwakuwa nchi imewashinda, tusome alama za nyakati
 
Ccm washatambua kuwa hawana chao, wakweka mikutano wananchi hawaendi wala hawana mpango wa kusikiliza ngonjera zao, ndio maana wanafanya kama wanavyotaka bila kujali, sababu wanajua kitumbua kimeingia mchanga.
 
Wewe mungi weka picha ndio uje na hizo hekaya mkuu. Hivi hivi kadaanganye watoto

Duu wewe milango 6, kumbe bado unaipenda chadema eeh...ama kweli chadema ni kama maji...usipoyaoga utayanywa dah.
 
Amezungumzia suala la Zitto Kabwe, kwamba chadema walishamalizana na Zitto Kabwe, anasema anabaki tu kama mwanachama wa chadema kupitia mahakama.
 
Amezungumzia suala la Zitto Kabwe, kwamba chadema walishamalizana na Zitto Kabwe, anasema anabaki tu kama mwanachama wa chadema kupitia mahakama.
Hiyo ndio demokrasia? Akumbuke kuwa kadi yake alikabidhiwa na zitto
 
Back
Top Bottom