Salary Slip
Platinum Member
- Apr 3, 2012
- 52,200
- 162,758
Unajua kuna jambo ambalo watu wengi hawajaligundua na pengine ndio kitu kinachomtesa JK katika kufanya maamuzi.
Kama tujuavyo,mh.Mhungo awali hakuwa mwanasiasa bali ni JK mwenyewe alimuitaji kisha akampa ubunge na baadae uwaziri.
Kwa sababu hiyo,kama Muhongo kuacha kazi yake ya awali,basi JK ndio sababu au kwa lugha nyingine,Kikwete ndio kamponza kwa kumuingiza katika siasa na leo hii akisema anamfukuza,basi lazima ahakikishe ana pa kumpeleka na si kumtupa tu.
Ugumu zaidi ni endapo Ikulu ilihusika katika sakata hili kama inavyotuhumiwa, kwani kama ni kumponza, basi hapo atakuwa kamponza mara mbili.Yaani mtu umemfanya ache kazi yake ya awali kwa kumpa kazi nyingine alafu kupitia kazi hiyo unamuingiza katika matatizo na kisha unatakiwa kumfukuza.
Hili jambo kibinadamu ni gumu sana,unless JK si sehemu ya uchafu huu na Muhongo alitumia ofisi vibaya kwa tamaa zake mwenyewe basi hapo Kikwete hatakuwa na lawama na itakuwa raisi hata kumwajibisha ila tofauti na hapo,Kikwete ana kibarua kigumu sana.
Unajua hata kama umelamba mabilioni,ila kuachishwa kazi kwa tuhuma za wizi kwa mtu kama Muhongo,ni pigo na aibu kubwa.Hawa watu hata wakiachwa kazi teyari wana mahela mengi ila hapa wanachopigania ni kujisafisha tu mbele ya jamii ingawa sidhani kama wanasafishika.
Hiki ndio kiini cha "kigugumizi" cha JK na huenda akampa cheo kingine hata kwa kutumikia nafasi hiyo mpya atakayompa nje ya nchi.
Najua ubunge wake bado upo utakuwa pale pale lakini kwa jinsi alivyokuwa na kazi nzuri na pengine ndio maana alikuwa na dharau,huo ubunge tu bado haumtoshi na hakuteuliwa ili awe mbunge tu.
Kama tujuavyo,mh.Mhungo awali hakuwa mwanasiasa bali ni JK mwenyewe alimuitaji kisha akampa ubunge na baadae uwaziri.
Kwa sababu hiyo,kama Muhongo kuacha kazi yake ya awali,basi JK ndio sababu au kwa lugha nyingine,Kikwete ndio kamponza kwa kumuingiza katika siasa na leo hii akisema anamfukuza,basi lazima ahakikishe ana pa kumpeleka na si kumtupa tu.
Ugumu zaidi ni endapo Ikulu ilihusika katika sakata hili kama inavyotuhumiwa, kwani kama ni kumponza, basi hapo atakuwa kamponza mara mbili.Yaani mtu umemfanya ache kazi yake ya awali kwa kumpa kazi nyingine alafu kupitia kazi hiyo unamuingiza katika matatizo na kisha unatakiwa kumfukuza.
Hili jambo kibinadamu ni gumu sana,unless JK si sehemu ya uchafu huu na Muhongo alitumia ofisi vibaya kwa tamaa zake mwenyewe basi hapo Kikwete hatakuwa na lawama na itakuwa raisi hata kumwajibisha ila tofauti na hapo,Kikwete ana kibarua kigumu sana.
Unajua hata kama umelamba mabilioni,ila kuachishwa kazi kwa tuhuma za wizi kwa mtu kama Muhongo,ni pigo na aibu kubwa.Hawa watu hata wakiachwa kazi teyari wana mahela mengi ila hapa wanachopigania ni kujisafisha tu mbele ya jamii ingawa sidhani kama wanasafishika.
Hiki ndio kiini cha "kigugumizi" cha JK na huenda akampa cheo kingine hata kwa kutumikia nafasi hiyo mpya atakayompa nje ya nchi.
Najua ubunge wake bado upo utakuwa pale pale lakini kwa jinsi alivyokuwa na kazi nzuri na pengine ndio maana alikuwa na dharau,huo ubunge tu bado haumtoshi na hakuteuliwa ili awe mbunge tu.