Wandugu, nataka kukodi kwa ajili ya harusi. Je, yanapatikana wapi? Na bei yake kwa siku ni shilingi ngapi?
Yapo kwa kina Janguo, sheikh Yahaya na hata car rentals! SERIOUSLY!!! Bei maelewano, mjini hapa, ukiingia kichwa kichwa unapigwaa! Kuyapata ingia Harusi yangu blog then kuna directory mule ucheki kama bado wapo listed. Ila hao watu maarufu kuwapata sio shida kabisa!!!
Kijana taratibu tafuta hata noah itakufaa, usije ukakodi hiyo limousine kwa ghalama kubwa halafu baada ya mwezi mmoja ukaishiwa. ni kweli kila mtu anapenda harusi yake iwe ya mfano but am telling you kama hela zipo kodi hata ndege ikupeleke visiwa vya Caribbean lkn kama ndo izo za kuunga unga angalia usitoke honeymoon na kuanza kupiga mizinga watu
Wazo zuri sana ndugu. Ila kuna jamaa amejitolea kama mchango wake. Ni vigumu sana kumwambia anipe pesa alafu mimi nikafanya makaratee mengine.