Yajue Madhara ya Vipodozi vyenye Kemikali na Vipodozi Vilivyopigwa Marufuku

EMT

Platinum Member
Jan 13, 2010
14,483
15,308


Zaidi ya asilimia 52 ya wanawake hutumia vipodozi vyenye sumu ambavyo huwasababishia matatizo mbalimbali ikiwamo kansa ya ngozi, figo pamoja na kuharibika kwa mimba kwa mama mjamzito. Aidha katika utafiti uliofanywa na Asasi isiyokuwa ya kiserikali Envirocare mwaka jana inaonyesha mikoa ambayo imeathirika zaidi na matumizi ya vipondozi hivyo ambayo ni Tanga, Dar es Salaam, Mwanza, Dodoma, Arusha, Mbeya na Kilimanjaro.

Meneja wa Mradi huo, Elfansia Shayo, alisema Envirocare imeandaa kampeni kwaajili ya kupinga matumizi ya vibodozi hivyo itakayofanyika leo jijini Dar es Salaam. "Envirocare kwa kushirikiana na Mamlaka ya Chakula na Dawa Tanzania (TFDA) imefanya utafiti ulionyesha zaidi ya asilimia 52 ya watumiaji wa vipodozi hivyo ni wanawake na baadhi yao wanajua madhara yake," alisema.

Mkurugenzi Mtendaji wa Asasi hiyo, Loyce Lema, alisema kampeni hiyo inahusu kutoa elimu kwa jamii kuhusu matumizi ya vipodozi hivyo na ambazo viambato hivi husababisha madhara kwa watumiaji na mazingira. Alisema pamoja na TFDA kuweka mfumo thabiti wa udhibiti wa vipodozi ambao unatumia njia mbalimbali ikiwamo usajili wa vipodozi, utoaji wa vibali vya biashara, na ukaguzi wa maduka bado mfumo huo unachangamoto kwani vipodozi vimekuwa vikiingizwa nchini kwa kutumia njia zisizo rasmi.






 
VIPODOZI VYENYE VIAMBATA VYENYE SUMU

Viambata vifuatavyo havitakiwi kuwepo kwenye bidhaa za vipodozi (Vimepigwa Marufuku kwa Matumizi ya Binadamu)

1. Bithionol
2.Hexachlorophene
3. Mercury compounds
4. Vinyl chloride
5. Zirconium – containing complexes in aerosol products
6. Halogenated salicylanilides (di-, tri- metabromsalan and tetrachlorosalicynilide)
7. Chloroquinone and its derivatives
8. Steroids in any proportions
9. Chloroform
10. Chlofluorocarbon propellants (fully halogenated chlorofluoroalkanes) in cosmetic aerosol products
11. Methyelene chloride

Tunapenda kutaarifu jamii kwa ujumla na wadau wote wanaojishughulisha na maswala ya vipodozi kuwa vipdozi vifutavvo vimepigwa marufuku

(ORODHA YA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU) LIST OF BANNED COSMETICS (2004-2005)

(vipodozi vyenye hydrokwinoni) "Cream" and "lotions" containing "Hydroquinone"

1. Mekako Cream.
2. Rico Complexion Cream
3. Princess Cream
4. Butone Cream
5. Extra Clear Cream
6. Mic Cream
7. Viva Super Lemon Cream
8. Ultra Skin Tone Cream
9. Fade - Out Cream
10. Palmer`s Skin Success (pack) Cream
11. Fair & white Active Lightening Cream
12. Fair & White Whitening Cream
13. Fair & White Strong Bleaching
Treatment Cream
14. Fair & white Body Clearing milk –tight Cream
15. Maxi – Tone fade Cream
16. Nadinola Fade Cream
17. Clear Essence Medicated fade Cream
18. Peau Claire Body Lotion
19. Reine Clair Rico Super Body Lotion
20. Immediat Claire Maxi – Beuty lotion
21. Tura Lotion
22. Ikb Medicated Cream
23. Crusader Skin Toning Cream
24. Tura Bright & Even Cream
25. Claire Cream
26. Miki Beauty Cream
27. Peau Claire Crème Eclaircissante
28. Sivoclair lightening Body Lotion
29. Extra Clair lightening Body Lotion
30. Precieux Treatment Beauty Lotion
31. Clear Essence Skin Beautifying Milk
32. Tura Skin Toning Cream
33. Madonna Medicated Beauty Cream
34. Mrembo Medicated Beauty Cream
35. Shirley Cream
36. Kiss – Medicated Beauty Cream
37. UNO21 Cream
38. Princess Patra Luxury Complexion Cream
39. Envi Skin Toner - Cream
40. Zarina Medicated Skin Lightener - Cream
41. Ambi Special Complexion - Cream
42. Lolane Cream
43. Glotone Complexion Cream
44. Nindola Cream
45. Tonight Night Beauty Cream
46. Fulani Cream Eclaircissante
47. Clere Lemon Cream
48. Clere Extra Cream
49. Binti Jambo Cream
50. Malaika Medicated Beauty Cream
51. Dear Heart with Hydroquinone Cream
52. Nish Medicated Cream
53. Island Beauty Skin Fade Cream
54. Malibu Medicated Cream
55. Care plus Fairness Cream
56. Topiclear Cream
57. Carekako Medicated Cream
58. Body Clear Cream
59. A3 Skin Lightening Cream
60. Ambi American Formula Cream
61. Dream Successful Cream
62. Symba crème Skin Lite ‘N' Smooth Cream
63. Cleartone Skin Toning Cream
64. Ambi Extra Complexion Cream for men
65. Cleartone Extra Skin Toning Cream
66. O`Nyi Skin Crème
67. A3 Tripple action Cream Pearl Light
68. Elegance Skin Lightening Cream
69. Mr. Clere Cream
70. Clear Touch Cream
71. Crusader Ultra Brand Cream
72. Ultime Skin Lightening Cream
73. Rico Skin Tone Cream
74. Baraka Skin Lightening Cream
75. Fairlady Skin Lightening Cream
76. Immediat Claire Lightening Body Cream
77. Skin Lightening Lotions Containing
Hydroquinone
78. Jaribu Skin Lightening Lotion
79. Amira Skin Lightening lotion
80. A3 Cleartouch Complexion Lotion
81. A3 Lemon Skin Lightening Lotion
82. Kiss Lotion
83. Princess Lotion
84. Clear Touch Lotion
85. Super Max – Tone Lotion
86 No Mark Cream

Gel with "Hydroquinone"

1. Body Clear
2. Topi Clear
3. Ultra Clear

Lotion containing "Hydroquinone"

1. Peau Claire Lightening Body Oil

Soaps containing "Hydroquinone"

1. Body Clear Medicated Antiseptic Soap
2. Blackstar Soap
3. Cherie Claire Body Beauty Lightening & Treating Soap
4. Immediate Clair Lightening Beauty Soap
5. Lady Claire Soap
6. M.G.C Extra Clear Soap
7. Topi Clear Beauty Complexion Soap
8. Ultra Clear Soap

Soaps containing Mercury and its compounds

1. Movate Soap
2. Miki Soap
3. Jaribu Soap
4. Binti Jambo Soap
5. Amira Soap
6. Mekako Soap
7. Rico Soap
8. Tura Soap
9. Acura Soap
10. Fair Lady Soap
11. Elegance Soap

Cream containing Mercury and its Compounds

1. Pimplex Medicated Cream
2. New Shirley Medicated Cream

Cream containing (hormones in steroids)

1. Amira Cream
2. Jaribu Cream
3. Fair & Lovely Super Cream
4. Neu Clear Cream Plus (spot Remover)
5. Age renewal Cream
6. Visible Difference Cream (Neu Clear – Spots Remover)
7. Body Clear Cream
8. Sivo Clair Fade Cream
9. Skin Balance Lemon Cream
10. Peau Claire Cream
11. Skin Success Cream
12. M & C DynamiClair Cream
13. Skin Success Fade Cream
14. Fairly White Cream
15. Clear Essence Cream
16. Miss Caroline Cream
17. Lemonvate Cream
18. Movate Cream
19. Soft & Beautiful Cream
20. Mediven Cream
21. Body treat Cream (spot remover)
22. Dark & Lovely Cream
23. SivoClair Cream
24. Musk – Clear Cream
25. Fair & Beautiful Cream
26. Beautiful Beginning Cream
27. Diproson Cream
28. Dermovate Cream
29. Top Lemon Plus
30. Lemon Cream
31. Beta Lemon Cream
32. Tenovate
33. Unic Clear Super Cream
34. Topiflam Cream
35. First Class Lady Cream

Gel containing steroids

1. Fashion Fair Gel Plus
2. Hot Movate Gel
3. Hyprogel
4. Mova Gel Plus
5. Secret Gel Cream
6. Peau Claire Gel Plus
7. Hot Proson Gel
8. Skin Success Gel Plus
9. Skin Clear Gel Plus
10. Soft & Beautiful Gel
11. Skin Fade Gel Plus
12. Ultra – Gel Plus
13. Zarina Plus Top Gel
14. Action Dermovate Gel Plus
15. Prosone Gel
16. Skin Balance Gel Wrinkle Remover
17. TCB Gel plus
18. Demo – Gel Plus
19. Regge Lemon Gel
20. Ultimate Lady Gel
21. Topifram Gel Plus
22. Clair & Lovely Gel

(ORODHA YA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU) LIST OF BANNED COSMETICS (2005-2006)

Cosmetics containing "Hydroquinone"
1. Body White Lotion
2. Bio Claire Cream
3. Forever Aloe MSM Gel
4. Kroyons baby oil

Cosmetics containing drug ingredients
1. Blue cap spray
2. Blue cap cream
3. Blue cap Shampoo
4. Marhaba Anti- Dandruff hair Cream

Hair cosmetic containing prohibited extract from "Apocynum Cannabium root extract"
1. African Gold Super Gro

Cosmetic containing potential carcinogenic extract from "Tussilago
farfara"
1. Sofn` Free Hair Food


(ORODHA YA VIPODOZI VILIVYOPIGWA MARUFUKU) LIST OF BANNED COSMETICS (2007-2008)

(vipodozi vyenye hydrokwinoni na steroid) Cosmetics containing "Hydroquinone & Steroid"

1. Clear Essence skin beautifying milk for sensitive skin
2. Fair & White Clarifiance fade cream
3. Fair & White Exclusive Whitenizer body lotion
4. Fair & White exclusive whitenizer cream gel
5. Fair & White Maxitone Lightening Lotion sun block
6. Fair & White So White Skin Perfector Gel

(vipodozi vyenye hydrokwinoni pekee) Cosmetics containing "Hydroquinone"

1. Fair & White Powder (Exclusive whitenizer & Serum)
2. New Youth Tinted Vanishing Cream
3. Skin Success Fade Cream Regular
4. Teint Clair Clear Complexion Body Lotion
5. Mareme Cream
6. Si Claire Plus Cream
7. Clair & White Body Cream

(vipodozi vyenye steroid pekee) Cosmetics containing "Steroid"

1. Fair & White serum exclusive Whitenizer
2. Maxi White Lightening Body Milk
3. Maxitone Cleansing Milk
4. Avoderm Cream
5. Niomre Cream
6. Niomre Lotion
7. Nyala Lightening Body Cream
8. Si Claire Cream
9. Cute Press White Beauty Lotion
10. White SPA Rose Lotion
11. White SPA UV Lightening Cream

Cosmetic containing extract from "Arctostaphylos UVA URSI (bearberry extract)"Plant containing "Hydroquinone" na "Arbutin".

1. Bio Light Cream
2. Salon DermaPlex Amazon Clay Normal to Dry Skin
3. Beauty Secrets Body Cream
4. Swiss Soft N White Lightening Gel
5. Whitening Complex Mask

Cosmetic containing potential carcinogenic extract from "Tussilago farfara"

1. Elasta-QP- (DPR-11) Hair Conditioner
2. Fanrasia- Pure Tea Gro for Hair

(vipodozi vyenye kiasi kikubwa cha madini ya zinki pyrithione, zaidi ya 1%) Cosmetic containing high concentration of Zinc Pyrithione 48% instead of Zinc Pyrithione 1%

1. Venus Solutions Soothing Scalp Treatment

Cosmetics containing Tin Oxide ingredient that associate with irritation when used around the area of the eye.


1. Eye Shadow Gel 10
2. Eye Shadow Gel 02 (Pearl Brown Gel with chaaracterisric odor)
3. Eye Shadow Gel 07 (Pearl Pink gel with characteristic odor)
4. Eye Shadow Gel 08 (Pearl Dark Red gel with characteristic odor)
5. Eye Shadow Gel 09 (Purple Dark Red gel with characteristic odor)
6. Eye Shadow Gel

Cosmetics containing malic acid and tartric acid that have property of peeling out skin cells causing whitening effect

1. AHA Whitening Cream


Source:TANZANIA FOOD AND DRUGS AUTHORITY
 
Asante sana Baba Mtu!!Kinachonishangaza mbona bado vipo madukani!!kweli ufisadi kila kona cjui itakuwaje,Kibaya zaidi vipodozi vilivyokatazwa mijini vinauzwa vijijini kwa bei poa kabisa,nilikuwa kwenye research nikayaona haya!!Who will save us jaman these people are killing women!!!
 
Actually it is suggested people use natural or herbal products; the above ones and perhaps many more could lead to skin cancer in a long run. Eating vegetables and drinking a lot of water is good for one's skin....lets avoid chemicals friends, ladies and gentlemen?
 

Kinachotakiwa ni kutoa taarifa tfda(mamlaka ya chakula na dawa tanzania). Vile kuwaelimisha akina mama na akina dada juu ya madhara ya kutumia vipodozi hivi. Kulikuwa na thread moja hapa jf ikitueleza jinsi dada yetu alivyoharibiwa ngozi yake na dawa/vipodozi.
 
Wengi wa wanaosoma hapa utakuta hawatumii ila wale dada zetu wa mtaani....
Na TFDA wanaweka kwenye website badala ya kukazania kutoa elimu kwa umma juu ya madhara ya vipodozi hivyo. Kibaya zaidi vimejaa tele Kariakoo, Ilala, Sinza na mtaani kwetu.
 
Duh!!! Hadi Clear Essence ndani tumekwisha halafu alomst vipodozi vyote bado viko dukani na watu wataendelea kununua kama kawa
 
Wanawake nchini wametakiwa kubadilika kwa kuacha kutumia vipodozi vyenye madhara mwilini na kuachana na dhana kuwa ukiwa mweupe au kuwa na mapaja manene unapendwa zaidi. Hayo yamesemwa na Kaimu Meneja wa Mamlaka ya Chakula na Dawa (TFDA), Kanda ya Kati, Florent Kyomo.

Kyomo amesema kuwa, asilimia kubwa ya waathirika wa vipodozi ni wanawake hasa wale wenye uelewa mdogo ambao hawataki kubadilika kwa kudhani kuwa weupe ni moja ya mafanikio na kupendwa zaidi na wanaume.

Ameongeza kuwa, changamoto kubwa wanayokabiliana nayo ni uelewa wa wananchi juu ya matumizi ya vipodozi vyenye madhara ambapo wengi wao wanashindwa kuacha kutumia kutokana na kutumia madawa hayo kwa muda mrefu na kufafanua kuwa, hata hivyo kuwa wataendelea na mikakati ya kutoa elimu zaidi ili watu wengi wajue madhara na kuwa na dhamira ya kuacha kutumia vipodozi hivyo.
 
KWELI kabisa mtu unatakiwa ujikubali jinsi MUNGU alivyokuumba na sio kujikoboa koboa
 
teh hata wanaume siku hz wanajichubua tena sana tu, so siyo vizur kusema ni wanawake tu, cha msingi ni kuwa hili jambo lina madhara na wahusike wanapaswa kushauriwa waache kujichubua, na wahusika wenyewe ni wanawake na wanaume wanaotumia hyo mivipodozi na siyo wanawake peke yao.
 
mimi napingana na kauli ya uelewa mdogo. Kuna wasomi kibao na wengine ni doctors na wanajichubua. Pia ni kweli kuna wanaume wengi tu siku hizi wanajichubua.
 
mimi napingana na kauli ya uelewa mdogo. Kuna wasomi kibao na wengine ni doctors na wanajichubua. Pia ni kweli kuna wanaume wengi tu siku hizi wanajichubua.

Unaweza ukawa msomi ila ukawa haujajitambua, suala la msingi wapewe elimu ya kujitambua ili waweze kujikubali jinsi walivyo!!
 
ila tuache maskhara bwana MWANAMKE MWENYE MAPAJA MANENE(figure bomba) NA MWEUPE anavutia wakuu..hasa for single night affair
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…