Yajue haya kuhusu nchi ya Marekani

Yajue haya kuhusu nchi ya Marekani

KUna mtu kasema mleta mada yupo hukohuko usa
Niakiangalia kiswahili chake ninawasiwasi naye nikama yupo musoma vijiji vya ndani ndani kule
ha ha ha ha ha
hiii ndio tz banaaa
Sheria inasema lazima uwe na bima lakini wengi tu huendesha bila ya bima, angalia P.D Friday utanifahamu. Mtandao wa craigslist au black page.


Ndukiiiii 🏃‍♂️🏃‍♂️🏃‍♂️
Kuna vtu unatakiwa uviepuke kama hvyo ndugu siku yakikukuta utajizika mzina
 
Habari za huko? Mi hakunifai huko,ahsante kwa tips
Nalog off
 
Yeah Jimmie, hafadhali umenena.
Namba 4 hyo sheria mbona hata huku ipo so usiwaone marekan ndio wa kwanza hata huku ni kosa kupiga muziki kwa sauti kubwa maeneo ya makazi... na ukitoa taarifa polisi hufika na kutoa onyo au kukamata kabisa (na wanavyopenda hela)

namba 7 umedanganya.... kumbuka kule kuna state laws na kuna federal laws.....

unaweza kuendelea kuwa safe from mikono ya sheria kama ulifanya kosa ambalo ni kosa under this state law na sio kosa under that state law kwa kuhamia kwenye hyo state

hautakuwa safe ndani ya marekani nzima if only kosa ulilofanya linaangukia under federal law

kama unaishi kweli marekani utakuwa umeelewa na kujua umekosea wapi katika uandishi wako

Namba 14 sio tu marekani hata hapa bongo kuna mitandao ya escort service kama EXOTIC TANZANIA ni hela yako tu unaingia unachagua unayemtaka mnakubaliana bei anakuja hadi kwako/sehemu mliyokubaliana so usishangae ukafikir ni marekan pekee

Namba 18 pia umedanganya a legal age for driving in USA avarage ni 16 yrs ..

lakini south dakota pekee ndio ni 14 na miezi 6 na kuna majimbo kama new jersey wenyewe wanaanza kuendesha na miaka 17

na bado kuna mijadala mizito kufanya legal age for driving iwe ni 18 ndani ya marekani

sasa sijui ww ndugu yangu miaka 13 umeona wapi wanaendesha magari...

hayo mambo uliyoandika ni mepesi mno next time jaribu kuandika mambo ambayo kweli watu hawayajui

huyo ndugu yako aliyopo USA mwambie aache kukulisha matango poli

Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hello JF MEMBERS jioni ya leo nimeamua kutajia mambo kadha kuhusu marekani.Marekani ni nchi ya kwanza kiuchumi na kijeshi na ya tatu kwa ukubwa duniani
Leo nataka ujue BAADHI ya sheria na utamaduni nchini marekani nitagusia mambo kadhaa ili upime au ulinganishe na nchi yako.

1.marekani mwanafunzi ndo huamua somo atakalosoma kwa kipindi husika na sio kupangiwa na mwalimu na anawezakwenda shuleni kwa muda wowote anaotaka

2.nchini marekani namba za ngari utumika kwa nyuma tu na si lazima huweke na mbele.magari karibia yote yana PLT N nyuma tu.

3.matumizi ya simu utumika kwa mwezi kununua kifurushi unachotaka na ndicho utakachokuwa unalipia kla mwezi ila unaweza kubadilisha kiasi cha pesa na ukaendelea tena kulipia kwa mwezi.

4.kuweka muziki kwa sauti kubwa ndani ya nyumba au unaongea kwa sauti inawezakuwa hata kutembea kwa kishindoni tatizo Jirani yako anaweza kupiga simu police au kumuita police kuwa unapiga kelele.(unaweza hata kufunguliwa mashitaka au kufukuzwa kwenye nyumba,ni bora upige mziki mkubwa kwenye gari)

5.kila raia nchini marekani ana namba ya dharura ya police(police akipigiwa cm dakka tu yupo mlangoni kwako).

6.kitambulisho cha ID kinamuwezesha mgeni kuishi marekani ndani ya mwaka mmoja

7.SOCIAL SECURITY CARD inakutambulisha popote ulipo nchini marekani.(mfano TZ niko mwanza nikifanya kosa nahamia sehemu nyingine basi nakuwa salama.lakini marekani sio hivyo bado unajidanganya,popote ulipo unajulikana).

7.marekani kuna utamaduni wa kumpokea mgeni wako kwa ua(ndugu,rafiki,jamaa una muda hujakutana nae na amekuja marekani utaenda umebeba ua utakalompa.

8.muislam haruhusiwi kuoa zaidi ya mke mmoja licha ya dini kuruhusu wake wanne,(kama wewe ni muislam itabidi tu uwe mpole).

19.awali marekani ilikuwa muungano wa majimbo 13 na ndio mistari 13 ya bendera.

10.ushoga marekani utambulika na wanafunga ndoa kama mume na mke

11.marekani ni taifa lenye watu wenye asili ya nchi mbali mbali ila ni raia wa marekani.

12.unaweza kutembea marekani nzima bila ya kuelekezwa na mtu au kwenda sehemu usihoijua na ukafika mradi tu ujue jina la sehemu unayoenda.(mfano niko msoma nataka niende kumtembelea ndugu yangu dae ntaenda na kufika bila kuelekezwa mpaka mlangoni kwake bila kuelekezwa)

13.africa tunafrika kwamba wazungu ni watu wabaya sana ila nchini marekani ni bora uwe na rafiki wa kizungu kuliko black na black wanajifanya wanajua sana kuliko watu wote na ni wabaya sana.

14.marekani kuna mitandao ya wanawake wanajiuza mtandaoni.ukimtaka mmoja kwa picha unaweza kumpigia simu na kumpa anuani ya nyumbani atakufuata utafanya yako pesa yake unampa anasepa zake.

15.wasichana nchini marekani huwa na .maboyfriend na sio kuwa na swala la mume tofauti na kwetu africa anataka basi umdangae nitakuoa

15.nchini marekani ndege ni kama mwendo kasi na hakuna ushamba wa kupanda ndege.(TZ ndege zinawenyewe ila marekani hilo wamelisahau kabisa)

16.nchi zetu za africa bado tunaangaika vijana kupata ajira ila nchini marekani ajira inaangaika kutafuta wafanyakazi.kwaiyo usishangae nchini marekani mtu akakuambia anafanya kazi 4 kwa siku (swala kama hilo nchini marekani naisi ndomana kila mtu anapenda kuja kufanya kazi marekani.

17.kila gari ina bima na ukiwa barabarani jaribu kuipa nafasi kubwa gari ilioko mbele yako.nchini marekani ukikwaruza kidogo tu gari la mwingine jua bima ya gari lako itausika kumnunulia gari lingine hapo kwako itakuwa ni kilio.(kuna tabia baadhi ya watu wanayo,akiona unamsongelea sana na uko kasi anashika breki fasta ili ukwaruze alafu anakuambia sitaki gari.hapo anamaanisha nyingine inunuliwe)

18.nchi marekani usishangae kuona mtoto wa miaka 13 akiendesha gari au kumilika gari au magari(TZ hayupo kabisa na ukiwa na gari basi inaaminika kuwa una pesa na mademu wa tz wanamshombokea sana mwenye gari ukiwa na gari utawapata wengi)

19.nchi marekani ni vizuri mwanamke akakupenda kuliko wewe kumtongoza maana ukifanya hivyo uweza kujisababishia matatizo,(sio wote) na bora awe mzungu kuliko mweusi.ukiwa unasikia kesi za wanawake kubakwa huwa ni ishu kama hizi alafu kwa takwimu zangu zisizo rasmi wanawake weusi wanaongoza.
Na wanawake nchini marekani akikupenda jua umepndwa kweli na wanawivu wa kuua usiombe akakufumania .(ila sina maana wanaume huwa hawawatamkii wanawake kuwa wanawapenda)

20.marekni unaruhusiwa kumuadhibu mtoto bila kumpiga na unapomuazibu zingatia sheria .(huruhusiwi kumpiga mtoto

N.B: hayo ni baadhi katika mengi sana .na hapo sina maana baadhi hapo africa hazipo inawezakuwepo ila uzingatiaji wake ni mdogo sana na nimetolea mfano kwa tanzania kwasababu tanzania ndo nchi ninayoifaamu sana na nimeishi sana

Swali unaruhusiwa ila kwa ufupi..





Sent using Jamii Forums mobile app
Kwahiyo unaifaham Tanzania zaidi ya unavyoifaham Congo? Naona mifano yote ya kipuuzi umeielekezea kwa nchi hiyo (Tanzania) kam vile kupanda ndege, mtoto mdogo kumiliki au kuendesha gari nk kana kwamba hayo mamb ya kushangaa ndege Congo hayapo
 
Kwahiyo unaifaham Tanzania zaidi ya unavyoifaham Congo? Naona mifano yote ya kipuuzi umeielekezea kwa nchi hiyo (Tanzania) kam vile kupanda ndege, mtoto mdogo kumiliki au kuendesha gari nk kana kwamba hayo mamb ya kushangaa ndege Congo hayapo
Hta ucjskie vibaya

We're the one people and are living in the one world
 
USA Baby...

Ila kuna kamba nyingi sana katika bandiko lako mkuu [emoji16][emoji16][emoji16]. Marekani ina majimbo 50 na kila jimbo linajitegemea kwa sheria zake kamili (japo sheria za shirikisho ndiyo ziko juu ya zingine). Mfano kuna majimbo kama California ni lazima uweke namba za gari kwa mbele pia (kama hawajabadilisha); na uchangudoa (ukiwemo wa mitandaoni) hauruhusiwi isipokuwa Las Vegas Nevada. Ukishikwa unajaribu kununua changudoa unatupwa jela na ni kashfa kubwa sana inayoweza kukufukuzisha kazi. Ni kwa sababu hii FBI huwa wanafunga mitandao ya machangudoa...
Huyo ni newcomer, yan ndo kwanza ana mwaka mmoja Marekani. Kwahiyo mengi hayajui japo anajifanya anajua
 
Bariadi umeishi
Tz nmekaa sana kulko kongo mwanza mmekaa miaka 7,na mikoa yote ya kanda ya ziwa mmekaa,dar pole mmekaa mwenzi mmoja,nna watoto wawili wote mmezaa na wa tz
Kwahiyo tanzania nafahamu kuliko watanzania wngn hasa mwanza pale nyamagana,ilemela na busweru huwezi niambia ktu hadi vichochoro nakupitsha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo ni newcomer, yan ndo kwanza ana mwaka mmoja Marekani. Kwahiyo mengi hayajui japo anajifanya anajua
Marekani saiv nmekaa majimbo matatu tofauti na nmetembea majimbo mengi marekani ni kubwa kuliko tz ila ni dogo sana kuliko tz kwny swala la usafr

Sent using Jamii Forums mobile app
 
SUALI moja to :- kwanini uMarekani hupenda kuvamia nchi zenye Rasilimali tunuku..??????
 
Back
Top Bottom