Ya Mbagala Na Bedui Aliyekojoa Msikitini...

Kweli haya ni maneno makubwa yenye hekima na yanayojenga pia. Hivyo inapaswa kujiangalia sana tusije tukaaibisha na kupaka matope dini kwa vitendo kama vile vya Mbagala, bokoharam, elshabaab na misimamo mingine mikali inayojaribu kufuatilia mambo madodo madogo wakati makubwa ya kuanzia na sisi wenyewe tukiwa na upofu nayo. Tusioshe kikombe nje tu na wakati ndani ni kichafu. Kama maji ni kidogo bora tuanze kuosha ndanikuliko nje.

Haya mamisimamo makali kama kweli watu wangechukulia kwa uzito huohuo katika kulea watoto wao, wao wenyewe, kujiadibisha wao wenyewe kwa kufuata miongozo ya dini basi kusingekuwa na na makosa ya jinai, dunia ingejaa upendo na watu wote (kama sio wengi wengekuwa machapakazi na sio kukaakaa kwenye vigenge na kuchokonoana masikio kwa hadithi zenye kejeli, wongo, upuuzi na uzushi.

Dini inaanza kwa mtu kujisafisha kwanza yeye mwenyewe na sio kuangalia kadoa kadogo kwa mwenzake na kusahau kuoga matope yaliyojaa mwilini mwake.
 


Wewe ina maana hukuelewa majid anazungumzia kitu gani? issue hapa ni suala zima la subira kwa nini nyie waislamu( si wote) mnakuwa watumwa wa hasira? Ni kweli sasa hivi utandawazi umesababisha watu wengi kuiga tabia za raia wa mataifa mengine(vurugu na maandamano katika baadhi ya nchi) hivi tuwavumilie mpaka lini,si ndio nyie mnataka viongozi wateuliwe kqwa uwiano wa kidini,huo ndio udini wenyewe sasa kwani Tanzania haikujengwa kwa misingi hiyo,kwa kuwa sasa mmeamka basi mbambaneni kielimu zaidi na si kulalamikalalamika. Kuweni wastaarabu bwana.
 

Mshangao wa kwanza nilioupata katika maisha yangu ni pale rais wa nchi alipotangaza kuwa udini umekolea sana Tanzania. Nilishangaa maana nina jirani yangu Muislamu, wakai wa Idd huleta pilau kwenye hotpot. Wakati wa krismass napeleka. Wakati woote ni rafiki yetu. Hapa kazini, tunamchanganyiko wa waislamu na wakristu tunaishi kwa amani sana. Mwenzetu akipata shida au furaha ya mtoto Idara yote twaenda kwake.
Hivi mnafikiri nguvu na kiburi cha Ponda kinatoka kwa nani kama siyo kwa mkuu wa kaya ambaye alitumia mbinu hizo kulalalisha ushindi wake?
Na tushukuru wale waliochomewa na kuibiwa vitu vyao kwa mgongo wa waislamu hawakutaka kulipa kisasi, au walivaa busara za 'mtume' kwa bedui aliyeenda kukojoa msikitini, vinginevyo JK asingekuwa anakula pepo huko Oman.
 
Tuache mafundisho ya uogo hayata tusaidia, watoto wanajaribu mafundisho yetu je yapo sawa? kumbuka kila fundisho litajaribiwa na kizazi hiki hivyo tuwe makini na mafundisho yetu. je huyu mtoto mkristo aliitoa wapi qurani?
 
Naungana na wewe 100% huu uliofanyika Mbagala ni uhuni wa hali ya juu na ni kweli inaonyesha kuwa vijana wengi hawana kazi na wapo tayari kufanya lolote saa yoyote.

Hili ni janga la Taifa tujitafakali upya!
 

Kwani ni uongo ni makasatasi? C Quran tu hata Biblia usipoijua ni karatasi dini au kitabu cha dini ni ndani ya moyo wa mtu na c physical thing kama ww unavyoita divai whisky pia Quran ni makaratasi tu na yaweza fungia mihogo kama gazeti la kiarabu linavyofungia mihogo na vitumbua.
Ulichofunzwa ww kuhusu Quran sicho ninachokijua mm na nininachojua mm kuhusu Bible sicho ujuacho ww, wala hukiamini so tuvumiliane Mungu ndie anaejua nani ni nani.
 
Ningependa nikusahihishe kama ifuatavyo;

*Kijana aliyekojolea Quran tukufu inaelezwa alikuwa ana umri wa miaka 12 kwa mujibu wa report ya polisi, vyombo vya habari na mahakama.

*Hakuna mahali popote kwenye uislam panapofundisha kuwa mtu akiidhalilisha Quran tukufu atageuka mnyama, kufa au kuwa kichaa.(Yule mtoto wa kiislam alikuwa anapotosha na kusema uongo kwa kumuhusisha Mwenyezi Mungu na jambo ambalo Mwenyezi Mungu hajalisema, kiislam huu ni sawa na ushirikina)

*Uislam haufundishi watu kufanya mizaha, kuthubutisha au kufanya majaribio kwenye Quran tukufu.
(Yule mtoto wa kiislam alipaswa kuadhibiwa kisawasawa na waislam kwani tunaamini anayajua hayo na alipaswa kuepusha yasitokee, na yule kijana wa kikristo alipaswa kufundishwa na kuonywa maana tunajua hajui nini maana ya Quran tukufu na mafundisho ya uislam kwa usahihi wake)

*Si sahihi kabisa kabisa kwa waislam kutaka kuamsha ghasia siku za leo kupitia matukio yoyote kwa kisa cha kudai waliwahi kuonewa siku za nyuma.(Kufanya hivyo hakuwezi hata sikumoja kuujenga uislam wa kweli, zaidi kutaleta uadui mkubwa na visasi)

MY TAKE
1/Wale watu wote waliofanya ghasia mbagala sio waislam sahihi, kwa kuwa uislam ni dini ya amani na masikilizano.

2/Hakuna mahali popote kwenye uislam panapotamka kuwa maadui wa waislam ni wakristo.
 
Mdondoaji,

Nimejaribu kufuatlia hoja yako lakini nimeshindwa kuelewa una maanisha ni nini! Kwa hiyo, wewe kwa mtazamo wako, unadhani kwa kuwa kijana ana miaka 14 basi ni sawa kwa hao waumini kureact kwa kuchoma makanisa? Kweli akili ni nywele...

Mkuu,

Hujanielewa kweli kwanza nilikuwa namuambia Maggid angelitumia mfano mwengine na sio huo wa bedui kwasababu huyo bedui alikuwa katika hali tofuati na yule kijana wa miaka 14. Ni afadhali angelitoa mfano wa mke wa abulahab aliyekuwa akimwekea miba mtume kila siku nyumbani kwake na miba ile ilikuwa ikimchoma mtume na kumuumiza na siku alipoiona haipo mtume alimfata yule mama nyumba kwake kumuuliza hali kwasababu alikuwa ni jamaa yake na hivyo alipoona miba haipo akajua huyo mama leo anajambo limemfanya asifanye kazi yake ya kila siku. But huyu mama alikuwa hajalewa, mtu mwenye akili timamu na alikuwa akifanya hali ya kuwa anafahamu ni kosa. Ila mtume alitumia busara kuliendelea jambo hilo.


Tukirudi katika kosa la huyu kijana nakubaliana na mawazo ya maggid kuwa busara itumike. Kwani sidhani makanisa au misikiti inahusika na matendo ya wanaadamu. Vile vile serikali iende mbali zaidi kushughulikia grievance za waislamu kwani yanayotokea Nigeria hayakuanza leo wala jana bali ya muda mrefu. Kinawashinda nini kuanzisha committee hiyo na ikawayasikiliza manunguniko ya waislamu na ikayasikiliza manunguniko ya wakristo then wakawaomba watanzania watoe mashauriano ili ipatikane solution kusudi tuishi kwa amani? Hivi wewe unadhani hali hii kutumia vitisho na mikwala ndio solution? Kuwakamata na kuwafunga watu ndio solution just think yourself utafahamu kuwa ninachokisema kina mantiki.
 

Naomba nikusahihishe,

Nimesoma kwenye gazeti moja na kwa mujibu wa watu walioko huko huyo kijana alikuwa ana miaka 14. Hata kama ana miaka 12 ni umri ambao vijana wengi wanakuwa washabaleghe na hivyo anajua fika anachokifanya.

Pili unaposema yule mtoto wa kiislamu anavyosema kuwa akiichezea Quran atageuka kuwa kichaa binafsi naona huyu nae ana kosa but haliko sawa na kukojolea Quran. Labda angelikuwa huyu kijana amekojolea biblia ningelikubaliana na wewe maana huwezi kuwa imani thabiti ya uislamu hadi uamini vitabu vyote vinne na biblia na quran ni mojawapo ya vitabu hivyo. Hivyo sikubaliani na wewe waadhibiwe sawa kwani mmoja amefanya mzaha na Quran na mwengine amekashifu Quran. Hawa wana adhabu mbili tofauti.

Kuhusu ghasia ninachokiona mie siamini hawa waislamu wanaoandamana au kufanya wengi ni waislamu bali ni wahuni na wasio na ustaarabu. Hata hivyo inawezekana baadhi yao ni waislamu na ukiangalia zaidi ni ufukara na chuki ya muda mrefu dhidi ya ndugu zetu wakristo ndio imepelekea hivi. Kwani wasichome masinagogi ya wahindi kule Temeke? Kwanini wasiharibu miti ya ibada ya wapagani bali wameenda makanisani? Haujiulizi why?
 
Ni kweli Mjengwa. Hakika Muislam safi hawezi kufanya kilichotokea Mbagala. Wale si Waislam ni wahuni.
 

Kwenye red text, Kwani uongo??? Mbona usikalie ujikute umefika Makkah au Newyork?? Vivyo hivyo biblia. Ni makaratasi tu. Kuna zaidi ndani ya hayo makaratasi ambayo nyie wahuni na ponda wenu hamkijui. Nuna, pasuka, jiue. Huo ndo ukweli.

 
Dini zinatumika kama kisingizio tu!

vijana wanatumika kisiasa... ukosefu ya ajira tanzania nao unachangia hili ..
 
Mjengwa, mfano huu unaujua tangu utoto wako au umeusikia lini? Kama kuna hadithi nzuri kama hizi ambazo ndugu zetu huwa mnazinukuu inakuwaje kunakuwa na Waislam wapumbavu wasioweza kupima haya? Hiyo subra inayohubiriwa miskitini kwenu inwaunisha nini nyie watu? Mbona hamna subra?

Tunaomba Maggid uwe Sheikh basi labda utawabadilisha hawa ndugu zako?!! Mimi katika Waislam wote namheshimu sana Sheikh wa Mkoa wa Dar-Es-Salaam (Sheikh Musa Salim, kama sijakosea), huyu kaka ana busara isiyo kifani maana ukimsikia anavyozungumza tu unajua hapo kwenye kichwa kuna busara!! Siyo hawa wengine sijui wamesoma wapi??
 
Dini zinatumika kama kisingizio tu!

vijana wanatumika kisiasa... ukosefu ya ajira tanzania nao unachangia hili ..


Viper,

You are absolutely correct Viper. Ukosefu wa ajira, umaskini na chuki vinachangia hili. Tuna mikakati mingi kama MKUKUTA, MKURABITA but inabakia kuwa miradi ya kutajirisha watu na watanzania wanazidi kuwa maskini na mafukara. Nilishawahi kusema unemployment among youth is more than 70% (according to the survey done by ILO na Wizara ya vijana). Hawa wote wanaishia kuingia kwenye ajira zisizo rasmi na huko ni kugumu. Baadhi ndio huishia kwenye bongo flava, drugs, wizi na kadhalika.
 


Ni kweli machafuko ya kidini yakitokea hakuna atakayepona kwa dini zote tuwe makini sana na wavumilivu pia tuombe
kwaajili ya amani ya nchi kila mtu kwa imani yake.
 
I like the christians wanapenda amani bila kujali madhehebu yao japokuwa wana madhehebu meengi!
 
BLUE:mkuu Mohamedi Mtoi plizzz reservve that words untill mbagalla issues,ponda issues,zanzibar issues are over and forgotten u cant even convince a very little child of 2yrs that is true about thee sayings ,but now we hope that to be but its not that way,nakiri ni taswira mbaya sana inajengeka pindi watoto wadogo wanapoona what islams do and you will agreed with me u cant change red to be white ,

ushauri:
Mohamedi Mto ninawiwa pia kutoa changamoto hii kwa dini ya kiislam kuwa wakati wakuchagua viongozi wa misikiti vigezo hivi hawa ndio watu wanaoweza kuaibisha au kuonyesha dini inaheshima gani ndugu yangu
1.elimu dunia
2.hekima
3.utashi
hii ndio vigezo vinavyowacost kwa sasa wanaiharibu dini ya mtume.kwa kweli ukiingia kwenye kila kimoja wapo kwa undani ungeona how its so simple to contol those as you have mentioned,hayo madhehebu mengine wanadil san na hivo vitu vitatu ,juzi nimeshuhudia waumini wa kianglikana wamempeleka mchungaji wao chuo kikuu kusoma ,elimu dunia is valuable
angalizo: sifungamani na upande wowote wa dini hizi za merikebu
 
Asante Majig Mjengwa kwa kuipenda nchi yako.

Tunajidanganya, ni nani anasema dunia ikibaki na waislamu au wakristo pekee ndipo itakuwa salama!!!!
 

Majjid you are very right Watu wavumiliane kama alivyosema mtume
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…