Ya Manumba Ni Zaidi Ya Malaria!

Ya Manumba Ni Zaidi Ya Malaria!

Kiungani

JF-Expert Member
Joined
Feb 2, 2007
Posts
274
Reaction score
71
Habari zinazozunguka kichinichini Magogoni na Central ni kuwa kuugua kwa ghafla kwa Manumba kuna ukaribu mkubwa na masuala aidha ya madawa ya kulevya, meno ya tembo/vifaru au Ulimboka. Nyepesi zinasema kuwa kabla hajaugua ghafla (Malaria ya siku mbili hadi ICU), alipitia baadhi ya taarifa zinazogusa upelelezi wa siri (status updates) wa masuala hayo.

Inasemekana kuwa mmoja wa vijana wake kikazi naye ana wasi wasi maana alim-feed Mzee updates fulani fulani.

Niliulizwa nishawahi kuona malaria ikampelekeka mtu ICU Aga Khan halafu haelekei kutoka?

Napotelea kwetu kiungani, mjini hatari.
 
Wakubwa wana kila kitu at their disposal..pesa..protection hata na privilage ya kwenda kutibiwa nje..sasa malaria ya kumpeleka icu...
 
hivi mkubwa yeyote akiugua au akifa kwanini watu wanahusisha na hujuma? Kwani hawa watu hawatakiwi kufa au kuugua!

nakumbuka majungu yaliyotokea baada ya kamanda barlow kupigwa risasi.
1. Mapenzi,-ameiba dem wa mtu
2. Visasi-kala hela za watu lakini kawatosa hajawatetea
3. Uwezekano wa yeye kuchaguliwa kuwa ijp-kwani ni mchapakazi, anakubalika
4. Ameingia mkononi mwa wanyan'ganyi-majambazi. Ya mwisho ndo ilithibitika. Hivyo na manumba watasema mengi tu
 
Au ni ile ishu ya madawa ya kulevya ya mtoto wa kigogo iliyotokea China? Pia najiuliza, kwa jinsi Manumba alivyojibu suala la Mwakyembe, usafi wake uko wapi hadi kuhusianishwa na kuingilia dili za wakubwa? Alishindwaje kumtetea Mwakyembe na leo azuie mambo ya watu? Ni dhana tu hizi lakini
 

Kujadili na kuhukumu vitu visivyo na uthibitisho ni "UPUUZI" Lakini kutokujadili tetesi kwa lengo la kupata uthibitisho, pia ni "UPUUZI".


-
ingawa ukitaka kuwa mwongo uwe na kumbukumbu nzuri usichanganye madawa.
 
Dhambi zinawatafuna wooote walijihusisha kudodimiza haki za wazee madocta na walimu achilia mbali sala za cdm hapo bado wengine watamfuata soon....!!!!
 
Unashanga Malaria kumpeleka mtu ICU?? Kwa nini usishanhae ndio ugonjwa unaoonguuza kwa kusababisha vifo?
 
Habari zinazozunguka kichinichini Magogoni na Central ni kuwa kuugua kwa ghafla kwa Manumba kuna ukaribu mkubwa na masuala aidha ya madawa ya kulevya, meno ya tembo/vifaru au Ulimboka. Nyepesi zinasema kuwa kabla hajaugua ghafla (Malaria ya siku mbili hadi ICU), alipitia baadhi ya taarifa zinazogusa upelelezi wa siri (status updates) wa masuala hayo.

Inasemekana kuwa mmoja wa vijana wake kikazi naye ana wasi wasi maana alim-feed Mzee updates fulani fulani.

Niliulizwa nishawahi kuona malaria ikampelekeka mtu ICU Aga Khan halafu haelekei kutoka?

Napotelea kwetu kiungani, mjini hatari.

Mkuu, heshima yako.

Nafikiri hujawahi kukumbwa na ugonjwa huu wa malaria kisawasawa.

Mimi nakumbuka nikiwa kijana mdogo nilipatwa na ugonjwa huu kisawasawa na joto la mwili wangu likafikia 40 na ilikuwa ni patashika kwamba ndio naondoka au vingine lakini kwa msaada wa madaktari na maji ya drip za dawa, nikaanza ,kupata nafuu ndani ya wiki moja nikiwa ICU ya Agha Khan.

Ni moja hospitali nzuri sana kwa kutoa huduma ya kuzingatia hali ya mgonjwa na nakumbuka niliweza kuanza kula na kusikia ladha yake kwa kuanzia kwa ugali na mchicha na kipande cha samaki.

Sasa tatizo a kuugua malaria ni pale inapogongana na ugonjwa mwingine na ndio hali inapokuwa tete kwani inabidi ulazwe ICU na upone malaria halafu uangaliwe ule ugonjwa mwingine.

Hivyo kwa madai yako inawezekana huyu mheshimiwa amekuwa "arrested" na ugonjwa zaidi ya mmoja kamavile BP, na kiharusi.
 
Malaria kali ikizidi wadudu 300 lazima upelekwe ICU, ila muda wa kutoka huko ndo ina tegemea kinga ya mwili.
 

Kujadili na kuhukumu
vitu visivyo na uthibitisho ni "UPUUZI" Lakini kutokujadili tetesi kwa
lengo la kupata uthibitisho, pia ni "UPUUZI".



-
ingawa ukitaka kuwa mwongo uwe na kumbukumbu
nzuri usichanganye madawa.

Naona umerudi... Karibu!
 
Malaria na Hasa Celebral malaria unakwenda ICU bila shaka , na hasa hawa wazee wa bia , maana bia huwa inaahirisha ugonjwa , Balaa ni pale ugonjwa unakufumukia , Noma !
 
Back
Top Bottom