Ya CHADEMA mpe Mungu na ya Kaisari mpe CCM

Ya CHADEMA mpe Mungu na ya Kaisari mpe CCM

Huu ni ujumbe kwa wapiga kura na watanzania wanaotafuta vyama vya kujiunga navyo baina ya CHADEMA na CCM.

Ukichagua ufisadi,wizi,ubadhirifu,uonevu,mauaji ya rai,kutozwa kodi za line ya simu,PAYE kandamizi, n.k basi rafiki yako ni Kaisari anaefanana na CCM na hivyo unapaswa kuchagua CCM.

Lakini kama wewe ni mtu wa kutetea wanyonge,kupinga dhuluma,uonevu,wizi,ufisadi na hata kupinga kodi ambazo ni mzigo kwa mwananchi hakika wewe ni kipenzi cha mungu na hivyo unastahili kuwa upande wa CHADEMA.

Tafakari ndugu!

hasante sana mkuu na maneno hayo yatumike popote pale kabla ya kuanza mkutano ifikapo 2015 naomba namba zako za simu
 
Vipi kuhusu kumwagia watu tindikali, kulisha watu sumu, kujilipua mabomu na kulegeza nati za tairi za magari ya watu??

Je,vipi kuhusu hizi sera zisizo rasimi za magamba

1.Kulindana

2.Ufisadi,wizi na ubadhirifu

3.Kung'oa watu kucha na meno

4.Kuiba kura

5.Kuzima na kuzuia maandamano

6.kuua rai ovyo kwa kutumia dola

7.Kufungia magazeti

8.Kuhamisha watendaji wabovu badala ya kuwafukuza

9.Kusaini mikataba usiku na tena isiyo na tija kwa taifa

10.Mikataba kufanywa siri

11.Kubeba wawekezaji na kunyanyasa wazawa

12.Ni mwiko kujiuzulu isipokuwa kwa shinikizo la bunge

13.Ukitaka kuchaguliwa toa rushwa a.k.a takrima.

14.Mwenyekiti wa chama taifa is untouchable!

Hebu fanya tafakuru alafu uone kama nimewasingizia au laa!
 
hasante sana mkuu na maneno hayo yatumike popote pale kabla ya kuanza mkutano ifikapo 2015 naomba namba zako za simu

Mkuu nashukuru sana ila kuhusu namba za simu najiuliza usije ukawa ni member wa TISS.Hawa jamaa si wa kucheka nao hata kidogo.
 
Ruzuku tu inawashinda kuweka wazi Mahesabu yake,mutaweza kuongoza nchi.
 
Back
Top Bottom