Daaah kaka shukrani sana umeongea fact nyingi za msingi nitafanyia kazi ushauri wako ubarikiwe sana mkuu
Ishi humo usipende kupendwa na wanawake,,
Ishi na mmoja tu wala usipende kugonga gonga hovyo wanawake,,
Maana kila uchi una miiko yake.
Uliye nae akizingua achana nae tu tafuta mwingine chungulia kama anaweza akafaa kwenye ufalme wako au atauangamiza hapo baadae.
Pambania kuwa mkubwa bila kutaka watu wengine wakusifu.
Ukiona umeanza kusifiwa kaa macho,, na uwaepuke hao wanaokusifu muda wote.
Usiwe na rafiki wa kudumu kabisa kwenye maisha yako.
Hapa namaanisha ni mwiko kuwa na mtu anaepajua Kazini kwako au Biashara zako na muda huo huo nyumbani kwako anapajua..
Weka mipaka watu unaofahamiana nao kwenye utafutaji wa riziki wasiweze kuyasogelea maisha yako ya nyumbani.
Ni marufuku na ni mwiko kuwatuma vijana uliowaajiri kwenye biashara zako kwenda nyumbani kwako.
Marufuku mkeo kwenda kwenye biashara zako bila mpangilio
Maana adui atajishikiza kwa mkeo na kukumaliza kabisa.
Wanawake wanatumaliza maana hutoa siri zetu kwa maadui bila wao kujua
Wakidhani kuwa wanachonga profile nzuri mbele za wanawake wengine kumbe ndio wanauza maisha yetu.
Kumbuka hayo mafanikio ni ya kwako wewe, wengine wote watanufaika nayo ikiwa tu watakubali kuendelea kubaki kwenye circle ya maisha yako.
Mtunze na kumficha sana mkeo kuliko kitu chochote kile kwasababu uhai wako unaanzia kwake,,
Mpende na umjali kwa wakati uwapo nyumbani.
Papendezeshe nyumbani kwako na uweke majibwa ya hatari kwaajili ya heshima ya nyumbani kwako,,
Mbwa huweka mipaka na kuwazuia maadui wa kike kufika nyumbani kwako.
Funga kamera za siri.
Uweke mji wako kiganjani mwako muda wote.
Ishi maisha yako bila presha simamia ndoto zako usiache kanuni hizo.
Idhibiti vyema nguvu ya pesa juu yako na mengine yote hatma itayaelekeza kuja kwako.
Tunza Afya yako, Tunza mkeo, Kula vizuri utibu mwili kwa maji ya baridi hasa nyakati za juakali kwa kuuloweka muda mwingi kwenye bwawa huku ukiyaangalia mawingu, hii inakufanya uvune nishati nyingi sana hapa ulimwenguni.
Tembea peku muda mwingi uwapo nyumbani usipende kuvaa kandambili.
Ongea na mbwa wako maana ndio marafiki zako wa kweli.
Mwisho kabisa wakumbuke wale wanaohitaji chakula unaweza ukawa na ratiba ya kuwalisha kila siku tatu za wiki kama bado kipato hakikidhi.
Ila kama unamudu wapatie chakula kila siku jioni.
Wale chakula washukuru uvune nishati ya riziki kutoka kwao.
Mwisho kabisa ukumbuke kuwa duniani tunapita hivyo yatupasa kuacha alama na kumbukumbu nzuri kwa watu kwa faida ya watu wetu tunaowaacha hapa duniani kama watoto na wajukuu wetu.
Maana sisi tutapita tu siku moja.
Kuna siku Dunia itaamka haina hata mtu mmoja aliezaliwa kuanzia 1980 hadi 2000. Enzi zinapita na tunasahaulika pia.
Kila la kheri ewe kijana mwenzangu.
BY SONKO BIBO.
The Author.