Wizi wa laptop katikati ya jiji

Wizi wa laptop katikati ya jiji

GP

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2009
Posts
2,049
Reaction score
161
wakuu,
siku hizi maeneo ya katikati ya jiji na hasa kule maeneo ya karibu na chuo cha ifm, mtaa wa samora etc. kumezuka WIZI wa laptops kwa kutumia magari hasa TAXI na saloons.
hii ni kutokana na kwamba MABEGI YANAYOBEBA LAPTOPS YANAJULIKANA, HIVYO UNATEMBEA BARABARANI na LAPTOP yako begani unashangaa ghafla IMEKWAPULIWA na mtu toka ndani ya GARI na gari kutokomea.
kuweni makini na mabegi yenye laptops.
 
SENKSI BWANA MKUBWA!
sina komments because ,MEN ARE AT WORK😀
 
Nadhani imefika wakati mbaya pia!!! Sasa si heri na kutemewa mate utakwenda kujikoga uso kuliko kukwapuliwa Laptop ya Milion 2..Na yawezekana kabisa na police wapo pembe wanatazama tu mchezo !!!!
 
Nadhani imefika wakati mbaya pia!!! Sasa si heri na kutemewa mate utakwenda kujikoga uso kuliko kukwapuliwa Laptop ya Milion 2..Na yawezekana kabisa na police wapo pembe wanatazama tu mchezo !!!!
Gharama ya Laptop inaweza isiume sana kuliko documents zilizopo kwenye hiyo laptop maana huzipati tena!!
 
Binamu hawa wakwapuzi wamekariri mabegi ya laptops, sasa hata wanafunzi wa ifm wakipita na bags zinafana na hizo na ndani maskini wameweka madesa, yanakwapuliwa vile vile!!!
 
WIZI WA LAPTOP KATIKATI YA JIJI

Kumekuwa na Wimbi kubwa la wizi wa Laptop maeneo ya Jiji la Dar es salaam kwa siku za karibuni haswa maeneo ya Posta Mtaa wa Samora Kwa kutumia Gari Ndogo za kubebea Abiria Taxi , Hii imekuwa Rahisi kwao kwa sababu begi nyingi za Laptop zinajulikana kwa maumbo na Lebo zilizoko kwenye Mabegi hayo .

Mara nyingi inawakuta watu wanaobeba mabegi hayo mikononi , ghafla gari hiyo inaweza kuja kwa nyuma kukutishia kukugonga Ndio hapo Unaporwa Begi Hilo .

Ingawa Tatizo hili limekwepo kwa kipindi kidogo kwa baadhi ya maeneo , hii tabia imerudi tena kwa kasi ya ajabu kwahiyo mnavyotembea huko mitaa kati kati ya Jiji haswa Samora muwe makini sana .

Hata hivyo Laptop nyingi huwa zinauzwa maeneo ya SAMORA Pembani mwa Duka La Kuuza Vitabu , JAMHURI , MKWEPU , FIRE ,NKURUMAH NA KUNA BAADHI YA MADUKA YA VIFAA VYA KOMPUTA HUWA YANASHIRIKI BIASHARA HII KWA KUNUNUA BIDHAA HIZO

NOTE : HAYO MAELEZO YA MAENEO SIO LAZIMA UKUTE VIFAA VYAKO NI KWA TAARIFA TU
 
Duh, we mkuu ni chiboko!!.
Yani umekopi "aidia" yangu, loh
 
WIZI WA LAPTOP KATIKATI YA JIJI

Kumekuwa na Wimbi kubwa la wizi wa Laptop maeneo ya Jiji la Dar es salaam kwa siku za karibuni haswa maeneo ya Posta Mtaa wa Samora Kwa kutumia Gari Ndogo za kubebea Abiria Taxi , Hii imekuwa Rahisi kwao kwa sababu begi nyingi za Laptop zinajulikana kwa maumbo na Lebo zilizoko kwenye Mabegi hayo .

Mara nyingi inawakuta watu wanaobeba mabegi hayo mikononi , ghafla gari hiyo inaweza kuja kwa nyuma kukutishia kukugonga Ndio hapo Unaporwa Begi Hilo .

Ingawa Tatizo hili limekwepo kwa kipindi kidogo kwa baadhi ya maeneo , hii tabia imerudi tena kwa kasi ya ajabu kwahiyo mnavyotembea huko mitaa kati kati ya Jiji haswa Samora muwe makini sana .

Hata hivyo Laptop nyingi huwa zinauzwa maeneo ya SAMORA Pembani mwa Duka La Kuuza Vitabu , JAMHURI , MKWEPU , FIRE ,NKURUMAH NA KUNA BAADHI YA MADUKA YA VIFAA VYA KOMPUTA HUWA YANASHIRIKI BIASHARA HII KWA KUNUNUA BIDHAA HIZO

NOTE : HAYO MAELEZO YA MAENEO SIO LAZIMA UKUTE VIFAA VYAKO NI KWA TAARIFA TU


Wizi!!
George_Porjie
user_online.gif
Today, 01:30 PM

wakuu,
siku hizi maeneo ya katikati ya jiji na hasa kule maeneo ya karibu na chuo cha ifm, mtaa wa samora etc. kumezuka WIZI wa laptops kwa kutumia magari hasa TAXI na saloons.
hii ni kutokana na kwamba MABEGI YANAYOBEBA LAPTOPS YANAJULIKANA, HIVYO UNATEMBEA BARABARANI na LAPTOP yako begani unashangaa ghafla IMEKWAPULIWA na mtu toka ndani ya GARI na gari kutokomea.
kuweni makini na mabegi yenye laptops.
Mods atafanya kazi yake ya kuziunganisha hizi post! Tatizo ni kupost kitu kabla hujasoma post zilizopo!
 
na nyie mmezidi ushamba mnatembea na laptop za nini?fanya kazi ofisini muda ukiisha nenda home acha kitendea kazi ofisini...acha wawapore bana
 
Biashara hii inashamiri kutokana na sababu nyingi .... moja wapo ni kuwepo kwa soko safi hasa kwa wanafunzi wa vyuo vyetu ambapo wanauhakika wa kuuza. Kuna jamaa alitaka ule laptop nyngi auze lakini akakatishwa tamaa na wadau wake walipomwambia kwamba mtu hawezi kununua laptop (yenye memory na speed ya kuridhisha) kwa laki 4 na nusu hivi KWA SABABU ZIPO LAPTOP NYINGI ZA WIZI KWA BEI CHINI YA HIO.....

haya kumbe ufisadi ni kila eneo...
 
Binamu hawa wakwapuzi wamekariri mabegi ya laptops, sasa hata wanafunzi wa ifm wakipita na bags zinafana na hizo na ndani maskini wameweka madesa, yanakwapuliwa vile vile!!!
ndio maanake,
nadhani mkuu Geoff kawastukia begi lake kama kabeba mtoto mgongOni!.
 
na nyie mmezidi ushamba mnatembea na laptop za nini?fanya kazi ofisini muda ukiisha nenda home acha kitendea kazi ofisini...acha wawapore bana
Sasa kutembea na laptop ni ushamba gani ndugu,hujui kama kuna kazi nyingine huwa pending,hivyo inapaswa kufanywa nyumbani?Acha kuunadi ushamba wewe!!
 
Mi nimeshama katika hivo vibegi 'vya laptop'. Nikibahatika kuja Bongo huwa natumia rucksack
 
ndio maanake,
nadhani mkuu Geoff kawastukia begi lake kama kabeba mtoto mgonogni!.

back pack is safer kwa laptops afu hawashtukii kama umebeba hiyo...mpwa Goeff is very smart
 
Sasa kutembea na laptop ni ushamba gani ndugu,hujui kama kuna kazi nyingine huwa pending,hivyo inapaswa kufanywa nyumbani?Acha kuunadi ushamba wewe!!

wewe ndo mshamba kabisa...eti kufanyia kazi nyumbani??kutwa manashinda kwenye JF mkiwa ofisini kazi hammalizi ikifika jioni mna beba mafaili na hivo mnavoita laptop eti ukafanyie kazi nyumbani kama unaweza kufanya kazi nyumbani si ungekaaa huku huku nyumbani kuliko kwenda ofisini ..we vipi
 
wewe ndo mshamba kabisa...eti kufanyia kazi nyumbani??kutwa manashinda kwenye JF mkiwa ofisini kazi hammalizi ikifika jioni mna beba mafaili na hivo mnavoita laptop eti ukafanyie kazi nyumbani kama unaweza kufanya kazi nyumbani si ungekaaa huku huku nyumbani kuliko kwenda ofisini ..we vipi

Mhh! wakati mwingine ni bora kukaa kimya kuliko kuanika ujinga wako!! Yaani kubeba laptop ni ushamba? Why was the laptop designed to be small and portable in the first place? Si tungebaki na desktop tu? Muda sio mrefu utasema kubeba mobile phones pia ni ushamba!!!
 
Mhh! wakati mwingine ni bora kukaa kimya kuliko kuanika ujinga wako!! Yaani kubeba laptop ni ushamba? Why was the laptop designed to be small and portable in the first place? Si tungebaki na desktop tu? Muda sio mrefu utasema kubeba mobile phones pia ni ushamba!!!

kubeba laptop sio ushamaba, elewa ile imetebgenezwa kwa ajili ya kufacilitate mobility, pia wengine kazi zetu sio za kukaa kwenye meza tangu asubuhi hadi jioni so we have to move so i wish kama ungejua umechemsha kusema laptop ni ushamba,

kwa ushauri ni vizuri kuwa na back up , mimi nina external drive na huwa ninafanya backup kila mwisho wa mwezi au hata mara 2 kwa mwezi. na na kwa wale wanaoweka laptop siti za nyuma za gari ( sallon cars) nairobi wanajivunjia kioo cha nyuma gari likiwa kwenye jam wanaondoka nayo, bestway weka chini ya seat ( unapoweka miguu) ili isimtamanishe alieko nje
 
Back
Top Bottom