Wapendwa kuweni macho...nilikua pale Total nje ya mcity nikaenda kutoa hela NBC nikakuta machine haitoi hela since ni master card nitaenda atm ya CRDB..mule ndani alikuepo mdada mdogo kwa umbo looks naive..
Nikamuuliza hutoki? Akajibu endelea tu natoa hela nyingi so nitawachelewesha so endelea...akaendelea kuongea hlf dada utoe card taratibu hii Atm ina tabia ya kukwaruza card..nikajibu sawa..
Nimefanya muamala card ilivyotoka huku machine inahesabu hela akasogea akawa anaivuta card yangu.. Madai yake anaitoa taratibu isikwaruzike (kumbe alinibadilishia card na alishakariri password yangu)
Nikatoa hela nikapokea card toka kwake nikaondoka... Nikawaza tu hajatoka coz Atm inatoa elfu 5 5 so note 40 ni laki 2 labda anatoa milioni coz alikua anahesabu pale...sikumjali
nikaondoka.
Kesho yake nilisafiri kikazi Dodoma, stayed for 2 wiks hapo cjui km nilibadilishiwa card since siku access Atm...
Basi nimerudi Dar naenda kutoa hela kila nikiweka password Naambiwa nakosea card ikamezwa.. Nikaingia ndani bank kunitolea card iliyomezwa nikawaambia sio hyo wakasema hii pekee ndio imekutwa kuicheck sio yangu.. Nikawatajia acc # kuangalia miamala kibao imeshafanywa wameiba 8m kumbe kila siku walikua wanatoa..
Nikawasimulia incidence ya yule binti wakaniambia yule dada wanamtafuta sana ameshaibia watu wengi kwa style ya kubadilisha card akishakariri password..na hakuna namna watanerefund coz ukiwa ndani ya ATM unatakiwa uwe peke yako nilipaswa nimwambie atoke..
So thts it dears.. Nna maumivu apa mchaga 8m usawa huu Uuuuwii
Hii imekaa kidramadrama, ngumu sana kuiamini maana inajenga maswali badala ya kuacha majibu.
We unaingia ATM kuchukua pesa bila ya kuwa na taadhari hata chembe tena mji wenyewe dar?
Badala ya kuchukua pesa unaanza kupiga story na mtu usiye mjua ndani ya atm? na unakubali kusaidiwa kutoa kadi kwa atmkwa ugumu gani we usiweze?
Unaingiza password yako openly bila ya kuweka japo kigingi?
Pesa uibiwe kwa uzembe wako via atm card afu eti benki wawajibike kukurefund wewe kwa uzembe wako?
Mpaka kadi inamezwa na unaingiza namba ya siri, kwani screen ya atm mashine ilikuwa haionyeshi jina la mwenye kadi?
Uibiwe hata polisi usiende kweli?
Umesafiri mpaka dodoma in two weeks kwa laki mbili tu wakati una 8m bak?
We acha majigambo eti 8m wakati umeweka bank pesa ya mgao wa vikoba. Unafaham 8m wewe?
Hongera, ukujaribu tena utakuwa mtunzi mzuri wa hadithi.