Habar za wakati wana jamvi.
Ninapenda kushare nanyi malalamiko ya watu wengi kuhusu Taxify na madereva wao kwa wizi wanaowafanyia watumia huduma.
Tukianza na Taxify wenyenye
Juzi nimesafir KM 7 kwa dk 13 na price ilikuwa 4000tsh
Nikachajiwa 10,000tsh safari ilikuwa ni ya kwenda. Cha ajabu kwenye risit inaonyesha nimetembea km 22 na ni sehem ambayo kila siku nasafir kwenda uko.
Wakati na rudi nimechajiwa sh 9000tsh kwa distance hiyo hiyo ya km 7 huku risit yao inaonyesha km 18.
Ni hii sio mara ya kwanza kutokea overcharging
Nikajirubu kupata mawasiliano yao kwa njia ya email
Wakanijibu ni GPS problem, nikawauliza kama hili tatizo mnalijua maana imekuwa hili ndo jibu lenu kila shida hii ikitokea mmechukua hatua gani lisitokee tena, nikapewa majibu mengine mepesi, ila wakaniambia wamesolve, nikasafir baada ya siku mbili KM 2 wakanichage 6000tsh na kunipa risit ya km 12. Nilienda offisin kwao nikakitana na dada mmoja akanijibu kirahis kwamba sim ya dereva ilikuwa ina shida ya GPS
My take kama mtanzania mmoja naweza kuibiwa sh 5000 kwa safari moja ni watanzania wangapi wengine wanaibiwa?
Jinsi madereva wa taxify wanavyoiba.
Kuna njia mbili ambazo nimezibain kutokana na experience yangu na huu usafir..
Ya kwanza, ukifika destination yako anakuonyesha screenshot ya bei kubwa kama una haraka unalipa af unaondoka af anaendelea na trip ya uber so distances inaendelea kusoma ilk baadae aki end bei iwe sawa au ikaribiane na aliyokucharge.
Pili inatokea sana ukifanya request kwajili ya mtu akifika anamwonyesha bei, af end trip kama amepata abiria wa uber anaendeleanae anakuja ku end baadae...
Pia kama kuna mtu mwenye utaalam wa sheria ni hatua gani zinaweza kuchukuliwa na wizi wa aina hii ili kuwatetea watanzania wanaoibiwa.
Asanteni.
Sent using
Jamii Forums mobile app