Wizi uliofanyika kwenye nyumba ya Mengi wakati wa msiba una somo la kujifunza

Freddie Matuja

JF-Expert Member
Jul 21, 2018
1,466
2,860
Wasalaam wandugu wapendwa,
Nimesoma kupitia vyombo vya habari kuwa vibaka/wezi wameiba mikufu ya dhahabu, fedha na laptop nyumbani kwa Mengi.
Polisi wanafanya kazi yao, ila kuna mambo kama Taifa na familia ya Tanzania tuna jukumu la kujiuliza kwa sauti na ikiwezekana kuchukua hatua za muda mfupi, muda wa kati na muda mrefu ili mambo ya wizi kama huu wakati wa msiba huko mbele yasitokee tena.

Kabla ya kutoa hoja ya nini kifanyike, pengine nije na swali;
Msiba huu ungetokea "Masaki au Oyesterbay" na wakahudhuria wakazi wa mitaa hiyo, bila shaka hata wizi usingefanyika;
Msiba huo wangehudhuria hukohuko Machame, wazee na watoto wao wa kishua, bila shaka wizi usingetokea.
Ila msiba ambao unatokea na kila mmoja anahudhuria kama zilivyo tamaduni zetu, msibani kila mmoja anakuja. Inapoteka kuna watu wana njaa, hawana tumaini la kupata fedha kwa kazi za mikono yao, na mara wanaingia kwenye kasri kama la mzee Mengi na huenda hawajawahi kuingia na wanajua mle ndani kuna "shekels", kuna vito vya thamani na laptop; ushawishi wa kuiba ni mkubwa.
Cha ajabu wanaiba sio kuhifadhi, wanaiba ila wakauze na kupata hela ya kula ili ndani ya siku 2 au 3 hana hata mia.

Iko haja kutengeneza mfumo jumuishi ambao watu wengi waweze kufanya kazi endelevu hata kama ni kukata nyasi alishe ng'ombe, kuku, kupalilia au kufyaka; cha msingi ana uhakika kuwa kila asb kuna pahala pa kutumia nguvu na akili yake kufanya kazi.
Inapotokea kuna gap kubwa sana kati ya walala hoi wengi na walala heri wachache, aibu ya uporaji kama huo haitaisha.

Serikali ni baba na mama wa Watanzania; iko haja kuja na programu na project jumuishi ili kupunguza nguvu kazi ambayo iko idle kitaa. Wengi tunafahamu, maeneo ya watu walio idle hata ukipaki gari ukazubaa hutakuta taa, mlango umevunjwa wameiba laptop au vitu vingine.

ila kuna maeneo bongo hapa hapa unaweza kupaki gari au kutembea usiku, hutaibiwa wala kukabwa. Maeneo yenye umasikini rate ya uhalifu iko juu. Hata tukiongeza vituo vya polisi bila kupunguza rate ya unemployment, tunakuwa hatujatenda haki kwetu kama watu wazima, hali kadhalika kwa vijana ambao ndiyo nguvu kazi, akina baba na mama wa kesho ambako taasisi za familia zinaundwa ili kuleta malezi ya watoto katika jamii ambayo kwa ujumla inajenga taifa.

Tunao wajubu wa kufanya kwa pamoja. Hatukubaliani na uhalifu hata kidogo. Ila tuna wajibu wa kudhubiti uhalifu usitokee na vitendo kama hivyo kwa kuunda mifumo endelevu ya vijana wetu kufanya kazi kwa kadri ya nguvu zao na elimu yao pia.

Jumapili njema wakuu
 
Nashukuru kwa taarifa yako nzuri na ushauri wako Mkuu.

Ila umesoma hiyo habari katika chombo gani cha habari? Naomba uthibitishe maandishi yako kwa ushahidi Mkuu.
 
Nashukuru kwa taarifa yako nzuri na ushauri wako Mkuu.

Ila umesoma hiyo habari katika chombo gani cha habari? Naomba uthibitishe maandishi yako kwa ushahidi Mkuu.
Kama uko Tanzania hii, leo vyombo vingi vya habari hususan magazeti yametoa taarifa hiii.
Pitia hii link hapa chini utapata details na mpaka taarifa ya RPC wa Kilimanjaro ipo...Anyway jihabarishe boss wangu
 
Hoja ipo hapa, tatizo uwasilishaji sasa. Ni kweli kuwa unemployment rate iko juu sana nchi hii,na ndiyo sababu watu wanapata nafasi ya kuzika kila mtu,hata kama hawahusu.

Hoja ya msingi ni hizi demokrasia mfu zilizojaa akili zetu. Hapo mkipigwa operesheni nguvu kazi mtaanza kusema mmevunjiwa haki za binadamu.

Hivi kweli mtu mzima, mtanzania anaweza kukosa kazi??? Fursa kibao nchi hii.
 
Hoja ipo hapa, tatizo uwasilishaji sasa. Ni kweli kuwa unemployment rate iko juu sana nchi hii,na ndiyo sababu watu wanapata nafasi ya kuzika kila mtu,hata kama hawahusu.

Hoja ya msingi ni hizi demokrasia mfu zilizojaa akili zetu. Hapo mkipigwa operesheni nguvu kazi mtaanza kusema mmevunjiwa haki za binadamu.

Hivi kweli mtu mzima, mtanzania anaweza kukosa kazi??? Fursa kibao nchi hii.
Boss wangu, Nchi za GCC UAE, Kuwait, Bahrain, Saudia, Qatar na Oman; hamna demokrasia hata chembe; ila wanatumia vyema rasilimali zao na wako njema kwelikweli kiuchumi.

Hii demokrasia ni mifumo tu ambayo sometimes tunabishana in the name of wengi wape na kuna wakati hao wengi wanaweza kuwa very shortsighted whenever it comes to deal with real issues.
Suala la msiba wa mzee mengi ni sehemu tu ya kuonesha kuna tatizo sio macheme, bali pahala pengi katika nchi yetu
 
Boss wangu, Nchi za GCC UAE, Kuwait, Bahrain, Saudia, Qatar na Oman; hamna demokrasia hata chembe; ila wanatumia vyema rasilimali zao na wako njema kwelikweli kiuchumi.

Hii demokrasia ni mifumo tu ambayo sometimes tunabishana in the name of wengi wape na kuna wakati hao wengi wanaweza kuwa very shortsighted whenever it comes to deal with real issues.
Suala la msiba wa mzee mengi ni sehemu tu ya kuonesha kuna tatizo sio macheme, bali pahala pengi katika nchi yetu
Mzee baba!punda kaka punda !! Bila mjeledi haendi ng'o. Hili ni swala mtambuka sana mkuu.
Kuna ongezeko la watu mijini,kuna hii feeling ya kusema mimi ni msomi sifanyi kazi hiyo,kuna hii tabia ya vijana kuganda home kwa wazazi. Lakini ukifuatilia hao wazazi walianzia maisha kwenye chumba kimoja kisicho na umeme wala maji.
Nionavyo mimi ni tubadili mitizamo kabisa.
 
Mzee baba!punda kaka punda !! Bila mjeledi haendi ng'o. Hili ni swala mtambuka sana mkuu.
Kuna ongezeko la watu mijini,kuna hii feeling ya kusema mimi ni msomi sifanyi kazi hiyo,kuna hii tabia ya vijana kuganda home kwa wazazi. Lakini ukifuatilia hao wazazi walianzia maisha kwenye chumba kimoja kisicho na umeme wala maji.
Nionavyo mimi ni tubadili mitizamo kabisa.
Boss wangu, iko hivi ili tupate matokeo tarajiwa lazima tutengeneze mifumo ya practical training, orientation na absorption ya hao watu wanakwenda wapi in an organized pattern.
Jeshini iwe polisi, Usalama, magereza, JWTZ;
Madaktari, nursing na wadau wengi wa taaluma ya tiba;
Michezo kama mbio, mpira wa miguu, netball, basket ball
wote hawa wanajifunza kwa vitendo. Knowledge in class in followed by practical training.

Kuna wakati mmoja ujinga ulifanyika sayansi ikafundishwa kwa kitu inaitwa alternative to practical... hapo ndipo failure ilianza kuzaliwa.

Wazungu wanakuja na mifumo ya kutudanganya tujengeane uwezo in the name of lifeskills kwa kupigana "sound"... hapa wanaotoka ni mmoja mmoja tena ni kama zali.
Unless we create an organized system iwe kwenye kilimo, ufugaji, biashara... tutaweza kuwa na mfumo endelevu wa kuwafanya watu wafanye kazi, wajijenge kijamii, wakue kimahusino kazini na kwenye jamii; kwa mfumo huo tutafika kule tupokwenda.
Ila kama watu wanasoma mpaka form 4; baada ya hapo hakuna mfumo rasmi kujua hawa watu wanakwenda wapi na kufanya nini; wanaishia kushinda kwenye betting venues maana hawana cha kufanya...
something must be done kwa vijana wetu kwa kizazi cha sasa na vizazi vijavyo ili tuwe na kizazi na jamii yenye afya miaka 100 ijayo... It begins with vision and mission how do every Tanzania fits in our motherland vision. Kama ipo namna gani watu wote tunafit in as family?

Wayahudi wana msemo: All Israel is responsible for one another... sisi kwenye context yetu... tukoje tukoje???
 
Duh!

Harusi za Marekani

Walioalikwa :100
Wanaohudhuria kanisani :80
Wanaohudhuria ukumbini :70
Wanaotoa Zawadi:65
Vitu vilivyopotea : 0

Harusi za Uingereza

Walioalikwa :50
Wanaohudhuria kanisani :50
Wanaohudhuria ukumbini :40
Wanaotoa Zawadi:40
Vitu vilivyopotea : 0

Tanzania sasa

Walioalikwa :500
Wanaohudhuria kanisani :38
Wanaohudhuria ukumbini :1300
Wanaotoa Zawadi:70
Vitu vilivyopotea : simu 20,vijiko 300,visu vya kukatia keki 15, camera 1,chupa 2 Za wine, mdada kutongozwa na kudate na Mgeni mmoja wapo, wavulana kutafuta demu mpya, zawadi kuibwa, viti vilivyovunjika 50,meza zilizovunjika 5,watu kuondoka na mapambo, wamama kuondoka na misosi na nyama kwenye mikoba sijui huwa tunakwama wapi.


Kwenye misiba na harusi kuna watu huiba zawadi za maharusi na vitu vya waombolezaji na vya mwenye nyumba, ni kawaida.
 
zikeni kama waislamu mtuanafariki anazikwa siku hiyo hiyo na sanda tu mazishi yanaishia kaburini baada ya kuzika hakuna story tena . lakini nyinyi ndugu zangu mtu mmoja kumzika inachukua mda siku tatu mnamuweka marehemu mnaanza kumsiifu weeee mpaka ina boa. ndio maana wengine hawapendi kwenda kwenye mazishi yenu maana sio mila yao mtamlaumu MO bure
 
Back
Top Bottom