Wizi makazini umaskini unachangia?

Wizi makazini umaskini unachangia?

Babu Ubwete

Senior Member
Joined
Jan 26, 2008
Posts
169
Reaction score
31
Kuna wimbi kubwa la wizi katika kampuni za mjini Vodacom,Barclays, Stanbic,Tigo etc ambazo nyingi zimeajiri vijana waliosoma walau first degree. Swali kwanini wizi huu umeibuka nyakati hizi kijana kamaliza tu mzumbe au udsm kapewa kazi ya uhasibu unasikia kaiba million 700, kuna mtu baclays kapiga billion 3. Tatizo ni nini?
 
Ni kushuka ama kupotea kwa maadili ya Taifa. Na pia hatujawa makini katika kushughulikia wizi, ufisadi na kila baya. Manake kila fisadi ama mwizi anajipa moyo kuwa akiiba atatumia hizo fedha alizoiba kuhonga na kumaliza kesi yake. Lakini tutakapofikia kuwa kama China katika kuwashughulikia mafisadi, wezi, watoa rushwa nk kutakuwa na woga fulani.
 
Kuna wimbi kubwa la wizi katika kampuni za mjini Vodacom,Barclays, Stanbic,Tigo etc ambazo nyingi zimeajiri vijana waliosoma walau first degree. Swali kwanini wizi huu umeibuka nyakati hizi kijana kamaliza tu mzumbe au udsm kapewa kazi ya uhasibu unasikia kaiba million 700, kuna mtu baclays kapiga billion 3. Tatizo ni nini?

Tatizo si umasikini hasa.

Mimi nionavyo, kwa mtu aliyetoka Chuo, akaajiriwa, na ndani ya mwaka 1au 2 kaiba, hiyo ni shida yake binafsi, zaidi tamaa.Vitu vizuri vimekuwa viingi, na bei zake ni za juu, hivyo ni lazima shortcut zitumike.

Na makampuni uliyoyataja nadhani mishahara yao si haba sana ukilinganisha na sekta zingine kama kwenye viwanda vya akina Kanjibhai.

Lakini shida ambayo siyo rasmi sana, ni mfumo uliojengeka katika jamii yetu kwa sasa ambapo wizi unaonekana kama njia ya fasta ya kujisongesha mbele! Inafikia mahali mwibaji kama huyo anaonekana kidume, na anatanua mtaa wa 2!

Viongozi wetu ndo kabisaaa, wanaiba mchana kweupe na kusababisha watu wengine kukesha wakipanga mbinu za "kutoka"!
 
Back
Top Bottom