Wizara ya Elimu mnakwama wapi?

Wizara ya Elimu mnakwama wapi?

pombe kali

JF-Expert Member
Joined
Jun 28, 2014
Posts
312
Reaction score
614
Hii Wizara ishakuwa kidonda ndugu, ubora wa elimu unashuka kila kukicha wahitimu tunaozalisha hawakidhi vigezo vya soko la ajira.

Shule zetu za umma uwiano wa wanafunzi kwa Mwalimu hauendani na uhalisia watoto wetu kila siku wanadaiwa hela na maelezo sahihi mwanangu wa Darasa la pili kila siku anatakiwa apeleke 500 bila hivyo anachapwa na kufelishwa inasikitisha.

Shule za binafsi ada haishikiki shule za umma elimu haikidhi, mashuleni hawaimbi tena nyimbo za taifa na za kizalendo badala yake wanawekewa nyimbo za kizazi kipya hata watoto wa kiume.

Hii sio sawa ikizingatiwa Wizara hii inaongozwa na msomi mwenye hadhi ya Uprofesa.
 
Hii Wizara ishakuwa kidonda ndugu, ubora wa elimu unashuka kila kukicha wahitimu tunaozalisha hawakidhi vigezo vya soko la ajira.

Shule zetu za umma uwiano wa wanafunzi kwa Mwalimu hauendani na uhalisia watoto wetu kila siku wanadaiwa hela na maelezo sahihi mwanangu wa Darasa la pili kila siku anatakiwa apeleke 500 bila hivyo anachapwa na kufelishwa inasikitisha.

Shule za binafsi ada haishikiki shule za umma elimu haikidhi, mashuleni hawaimbi tena nyimbo za taifa na za kizalendo badala yake wanawekewa nyimbo za kizazi kipya hata watoto wa kiume.

Hii sio sawa ikizingatiwa Wizara hii inaongozwa na msomi mwenye hadhi ya Uprofesa.
Pole sana mdau, kwakweli kuna mambo ambayo yanahitaji sana tathmini na ufuatiliaji na Wizara hawawezi kukwepa hili.

Lakini nadhani wanaingia na kuona malalamiko yetu, pia kwa ushauri wangu kwa kuwa shule ni nyingi sana na huenda tatizo sio shule zote ni baadhi. Basi ungeweka na jina la shule husika ambayo/ambazo unazilalamikia. Kwa uelewa wangu uendeshaji wa shule upo Tamisemi kupitia ngazi za Halmashauri (decentralization), hivyo kupata consistency ya utekelezaji wa miongozo sio jambo rahisi.

Walipue tu hao wanaofanya hivyo na naamini Wizara watadeal nao kama kuna hayo mambo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Elimu nzuri ni gharama....

Nimempeleka mtoto kwa iterview last week
.. Kabbla ya tarehe 5 Jan malipo laki sita sabini hukoo... Bado Nauli..

Niko hapa kinyonge nawaza. Shule za uma hizo ndo majanga. Watoto wanaenda kukua.

Shida Ipo.
 
Back
Top Bottom