Gurudumu
JF-Expert Member
- Feb 5, 2008
- 2,349
- 261
Kuna hili bango la wizara ya afya ambalo limekuwa pale ocean road takriban miezi miwili sasa. Ni wazi linampigia JK kampeni, na tume haikutoa amri ya kuliondoa. Tukumbuke rais wetu mteule Slaa ana sera za kimapinduzi kwa wizara hii. Watendaji wake ndio hao bado wanajipendekeza kwa JK hadi wakati huu ambao upepo umeshabadilika dhahiri.
labda swali la msingi, (tukianza kujipanga kutoa huduma za afya bure), ni kwamba bango hili linagharimu shillingi ngapi kwa siku na ni kiasi gani kwa miezi miwili ambayo limetundikwa hapo? matumizi ya aina hii ya pesa yanachangiaje ukosefu wa dawa, vitanda na vifaa katika hospitali zetu?