ong'wafaza
JF-Expert Member
- Apr 30, 2012
- 243
- 100
Mimi mtanisamehe maana bado ni muumini wa Baba wa Taifa Hayati Mwl. Jk Nyerere.
Nakumbuka enzi za uhai wake aliwahi kutaja mambo manne muhimu ambayo yeye binafsi aliamini tulitakiwa (na mimi bado naamini) kuyazingatia katika kusaka maendeleo yetu.
Ili tuendlee kama Taifa na hata kwa mtu mmoja mmoja tunatakiwa tuwe na Watu,Ardhi ,Siasa safi na Uongozi bora.
Kwa mkutadha wa mada hii,leo sitaongelea Watu na Ardhi japo navyo vinahitaji mjadala.
Leo nitajikita kwenye masuala ya Siasa safi na Uongozi bora.
Na haya ndio mambo ya msingi ambayo Wateule wanatakiwa kuyazingatia.
Kwa muda mrefu sasa Watanzania tumekuwa tukiendesha nchi yetu chini ya mfumo wa siasa ya demokrasia ya vyama vingi .
Aina hii ya siasa kwa kweli haijafanikiwa sana katika kuleta utulivu kwa nchi, kwani kumekuwa na makandokando mengi yaliyosababisha hata utekelezaji wa majukumu ya wanasiasa (viongozi) wenyewe kutoelewana vizuri.
Kadhalika, upatikanaji wa viongozi bora umekuwa na changamoto nyingi zilizosababishwa, kwa kiasi kikubwa, na mfumo mbaya wa namna ya upatikanaji wa viongozi katika ngazi mbali mbali.
Yote haya, kama hayatawekwa sawa,tutashindwa kuendelea kwa kasi inayotakiwa.
Nichukue nafasi hii kuwaasa Wateule hawa kuyaishi maono haya ya Mwalimu kwa kusimamia kupatikana kwa mifumo sahihi ya kuendesha nchi (siasa safi) na namna bora ya kupatikana viongozi bora.
Nachelea kusema kuwa, suala la upatikanaji wa Katiba mpya haliepukiki.
Pengine mchakato wa kupata Katiba mpya iliyo bora unaweza kuchukua muda mrefu.
Lakini jambo la kutengeneza mfumo bora wa namna ya kupata. Viongozi bora likiwemo swala la upatikanaji wa Tume huru ya uchaguzi linaweza lisichukue muda mrefu.
Ni matumaini yangu kwamba, , Wateule watakubalina na mimi kwamba, pamoja na mambo mengine, kazi kubwa waliyonayo ni kuwaletea maendeleo ya kweli Watanzania.
Juhudi zote watakazofanya, wanapaswa kufahamu kwamba bila SIASA SAFI na UONGOZI bora maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana.
Au ninasema uongo ndugu zangu?
Nakumbuka enzi za uhai wake aliwahi kutaja mambo manne muhimu ambayo yeye binafsi aliamini tulitakiwa (na mimi bado naamini) kuyazingatia katika kusaka maendeleo yetu.
Ili tuendlee kama Taifa na hata kwa mtu mmoja mmoja tunatakiwa tuwe na Watu,Ardhi ,Siasa safi na Uongozi bora.
Kwa mkutadha wa mada hii,leo sitaongelea Watu na Ardhi japo navyo vinahitaji mjadala.
Leo nitajikita kwenye masuala ya Siasa safi na Uongozi bora.
Na haya ndio mambo ya msingi ambayo Wateule wanatakiwa kuyazingatia.
Kwa muda mrefu sasa Watanzania tumekuwa tukiendesha nchi yetu chini ya mfumo wa siasa ya demokrasia ya vyama vingi .
Aina hii ya siasa kwa kweli haijafanikiwa sana katika kuleta utulivu kwa nchi, kwani kumekuwa na makandokando mengi yaliyosababisha hata utekelezaji wa majukumu ya wanasiasa (viongozi) wenyewe kutoelewana vizuri.
Kadhalika, upatikanaji wa viongozi bora umekuwa na changamoto nyingi zilizosababishwa, kwa kiasi kikubwa, na mfumo mbaya wa namna ya upatikanaji wa viongozi katika ngazi mbali mbali.
Yote haya, kama hayatawekwa sawa,tutashindwa kuendelea kwa kasi inayotakiwa.
Nichukue nafasi hii kuwaasa Wateule hawa kuyaishi maono haya ya Mwalimu kwa kusimamia kupatikana kwa mifumo sahihi ya kuendesha nchi (siasa safi) na namna bora ya kupatikana viongozi bora.
Nachelea kusema kuwa, suala la upatikanaji wa Katiba mpya haliepukiki.
Pengine mchakato wa kupata Katiba mpya iliyo bora unaweza kuchukua muda mrefu.
Lakini jambo la kutengeneza mfumo bora wa namna ya kupata. Viongozi bora likiwemo swala la upatikanaji wa Tume huru ya uchaguzi linaweza lisichukue muda mrefu.
Ni matumaini yangu kwamba, , Wateule watakubalina na mimi kwamba, pamoja na mambo mengine, kazi kubwa waliyonayo ni kuwaletea maendeleo ya kweli Watanzania.
Juhudi zote watakazofanya, wanapaswa kufahamu kwamba bila SIASA SAFI na UONGOZI bora maendeleo ya kweli hayawezi kupatikana.
Au ninasema uongo ndugu zangu?