Kama mdau hapo juu alivyokuambia, Gpu ni muhimu zaidi, na Display port ni nzuri kushinda Hdmi linapokuja suala la monitor.
Port 1 ya display port ina uwezo wa kudrive monitor 4 za Full HD. Kuna monitor maalumu zenye dp in na out unaunganisha na waya wa dp monitor zote toka output moja ya desktop ama laptop.
Na njia hii sio lazima uwe na gpu kali kivile hasa kama software yako sio nzito unayotaka kuitumia kwenye multi monitor. Hata gpu za ndani za laptop zinaweza kamilisha hii kazi, laptop za kazi kama thinkpad utakuta badala ya Hdmi wanakuwekea port ya Mini dp.
Kama upo serious sana ndio utahitaji gpu highend kama hio Rtx 2080 na wengine wanaweka multi gpu, unakuta Gpu 2 zinawekwa pamoja, incase monitor zako ni high resolution kama 4k. Sema hapa jiandae milioni 10 zinaweza kuisha kimasihara tu.