Wimbo wa Gaidi

LEGE

JF-Expert Member
Oct 14, 2011
5,123
9,168
1913551_482137365323486_6568961958810323386_n.jpg





AYA: Wimbo wa Gaidi

MTUNZI: Hussein Tuwa

UTANGULIZI

Ni miaka mitatu tangu kuuawa kwa Osama bin Laden nchini Pakistan. Wanamgambo wa Al-Qaida wamesambaratika. Wengi miongoni mwao wameuawa, wengine wamekamatwa na majeshi ya marekani nchini Pakistani…na kikundi cha wachache wengine kimefanikiwa kutoroka na kukimbilia eneo la Waziristan lililo kaskazini mwa Pakistan, hususan kwenye kitongoji cha Miramshah kinachodhibitiwa na wapiganaji wa Taleban, ambao walikuwa ni washirika wao wakuu na huko wakapata hifadhi baada ya kifo kile kichungu cha kiongozi wao.
Na tangu wakati huo, hali ya wakaazi wa kijiji kilichokuwa kiasi cha kilomita saba kutoka kwenye ile ngome ya wa-Taleban iliyowahifadhi wale wanamgambo wachache wa Al-Qaida, imekuwa ni ya mashaka makubwa. Njaa ilikuwa imetawala, mahitaji yote muhimu yametoweka, maradhi hayakuwa na wa kuyatibu, ilhali magonjwa ya mlipuko na yatokanayo na lishe duni yakishamiri…na roho za wanakijiji kile zikiwa sio mikononi mwao tena, bali mikononi mwa wapiganaji wa taleban waliokidhibiti kijiji kile.
Kwa nini?
Kwa kuwa Osama Bin Laden alikuwa ameuawa na wamarekani…na taarifa ziliwafikia wa-Taleban kuwa tabibu aliyefika mahala ambapo Osama alikuwa amejificha kwa ajili ya kumtibu binti wa mpiganaji yule mwenye msimamo mkali ndiye aliyetoa siri ya mahala Osama alipokuwa, kwani wamarekani walivamia eneo lile siku mbili tu baada ya tabibu yule aliyeaminika kuwa alikuwa akiiunga mkono Al-Qaida kufika eneo lile. Kwa kuwa Al-Qaida ilisambaratika kwa muda baada ya kifo cha Osama, Taleban wakachukua jukumu la kulipiza kisasi kifo cha mshirika wao mkubwa kwa niaba ya Al-Qaida.
Hivyo basi, pale binti wa Osama aliyekuwa akishikiliwa na wanajeshi wa Pakistani kabla ya kukabidhiwa kwa wamarekani, alipofanikiwa kupenyeza taarifa kwa watalebani kupitia kwa mmoja wa watendaji wa jeshi la Pakistani aliyekuwa akiiunga mkono Al-Qaida kwa siri, kuwa tabibu huyo alikuwa akiongea kwa lugha ya ki-pashtuni, lakini kwa lafudhi ya watu watokao kwenye kijiji kile, ilitosha sana kuwajulisha watalebani kuwa dakitari aliyemchomea utambi Osama kwa wamarekani hadi akauawa, alikuwa ametokea kwenye kijiji kile kilichokuwa kiasi cha kilometa saba tu kutoka pale kwenye ngome yao.
Kilichofuatia kilikuwa ni kizazaa kikubwa pale kijijini.
Mauaji, mateso, na utekaji nyara viliwaandama wanakijiji, ikitafutwa familia ya tabibu aliyemchoma Osama kwa wamarekani. Msako wa nyumba hadi nyumba uliondeshwa ukazaa matunda. Familia ya tabibu aliyehusika kumchomea utambi Osama ilipowekwa kizuizini kwa wiki nzima na kuwekwa kwenye wakati wa mateso na vitisho visivyosemeka ikiwamo kubakwa, kupigwa mijeledi na baadhi yao wakiuawa huku wengine wote wakishuhudia, siri ikabidi itolewe. Tabibu wa Osama akatajwa na wanafamilia wake mwenyewe, wakati huo yeye akiwa jijini Islamabad.
Wataleban wakamfuata huko huko kwa lengo la kumuua. Lakini sio kabla ya kumtesa na kumhoji kikatili. Tabibu akakiri kuwa hakuwa peke yake…alikuwa na mwenzake kutokea kwenye kijiji kile kile ambaye alikuwa ni miongoni mwa wapiganaji wa Al-Qaida waliokimbilia kule kwa Wataleban na kuhifadhiwa.
Hah!
Wateleban wakahamanika. Ni nani huyo?
Tabibu akafa na siri yake kwa kujitia kumpora silaha mmoja wa watesaji wake ili awateketekeze.Wakamuwahi na kummiminia risasi. Kifo cha Osama kikalipizwa… miezi mitatu tu baada ya kifo chake. Lakini sasa wataleban wakabakiwa na kitendawili kikubwa. Ni nani miongoni mwa wale maswahiba wao wa Al-Qaida waliowahifadhi kule kwenye ngome yao jirani na kile kijiji walichokibatiza jina “kijiji cha wasaliti”, aliyekuwa akishirikiana na yule tabibu msaliti?
Sasa huyu ndiye alikuwa anasakwa na kijiji kile kikawekwa chini ya karantini kabambe na watalebani.
Na mpaka msaliti huyo na wengine kama yeye watakapobainishwa na kuuawa, hakuna atakayetoka wala kuingia kwenye kijiji kile.
Kijiji kikawa kimetengwa na dunia.
Jitihada za majeshi ya Pakistani kukiokoa kijiji kile hazikufua dafu asilani, kwani Waziristan ilikuwa ni ngome kuu ya wataleban, na hakukuwa na namna ya kuiangusha isipokuwa kwa kuipenya kijasusi kama jinsi alivyopenyezwa yule tabibu mzaliwa wa kijiji kile ndani ya kundi la Al-Qaida.
Na hilo lilikuwa haliwezekanin tena sasa. Watalebani wlaikuwa wkimshuku kila aliyewaendea na kila waliyemuona kuwa si miongoni mwao.
Na sasa hali ilikuwa imefikia pabaya.
Wapiganaji wote wa Al-Qaida waliokuwa wamehifadhiwa kwenye nyumba salama ya uongozi wa wa-Taleban. Miongoni mwao alikuwamo msaliti. Talebani walidhamiria kumtia mikononi na kumuangamiza. Ilikuwa ni mahojiano ya mara kwa mara, mitihani ya hapa na pale kwa wale Al-Qaida waliokimbilia mikononi mwa washirika wao wa ki-Taleban.
Amani ikapotea. Ndani nan je ya nghome ile kubwa ya watalebani.
Jumuia ya kimataifa ilifanya bidii za kila namna kuwaokoa wakaazia wa kijiji kile bila mafanikio yoyote. Serikali ya Pakistani pamoja na kulaani kwake kuuawa kwa Osama ndani ya nchi yake bila ya wao wenyewe kushirikishwa, haikufua dafu, kwani Taleban siku zote wamekuwa wakiamini kuwa serikali ya Pakistani ilikuwa ni kibaraka wa wamarekani.
Marekani ikatoa tamko. Talebani iwaachie huru wana kijiji wale waondoke kijijini pale na kwenda kwenye kambi za wakimbizi nje ya kitongoji kile cha Waziristan, na iwasalimishe wapiganaji wote wa Al-Qaida iliowahifadhi, ama si hivyo ndege za maangamizi zinazoruka bila ya rubani, yaani “drones”, zitatumwa kuisambaratisha ngome yao.
Taleban wakagoma.
Na wao wakatoa tamko.
Wamarekani wakituma hizo ndege ijue pia itaua raia wa kijiji wasio na hatia…na watalebani watakuwa wanaua kila mmarekana watakayemuona, popote pale duniani.
Ngoma nzito…

______________

SEHEMU YA KWANZA

Kijiji cha Dargah Mandi, kilomita saba magharibi mwa kitongoji cha Miramshah, Waziristan ya Kaskazini, Pakistan.

Ni saa saba za usiku. Baridi kali ilikuwa ikipambana na mashuka mazito yaliyokuwa yakijaribu kuihifadhi miili ya wanakijiji waliorundikana upande mmoja wa eneo pana la tambarare lililokuwa mpakani kabisa mwa kijiji kile kilichojaa madhila makubwa na mashaka mazito.
Ni kijiji cha Dargah Mandi kilichokuwa ndani ya kitongoji cha Waziristan ya Kaskazini, ambayo ilikuwa ni ngome kuu ya wapiganaji wa Taleban, nchini Pakistani.
Wanakijiji walikuwa wamejikunyata wakisubiri msaada waliokuwa wameutarajia kwa muda mrefu bila matumaini ya kuupata. Wapiganaji wa Taleban wenye silaha walikuwa wamewazingira wanakijiji wale kutoka pande zote za eneo lile, nao wakiusubiri msaada ule ambao kwa hakika na wao walikuwa wakiuhitaji, maana hali kijini Dargah Mandi ilikuwa tete kila upande.
Mbele yao, kiasi cha kama mita mia tatu hivi kutoka pale ambapo wale wanakijiji walikuwa wamejikunyata huku wakiwa wamewekewa mitutu ya bunduki za wapiganaji wale wenye roho zisizosita kutekeleza mauaji, kulikuwa kuna uwanja mpana wa wazi wenye majani mafupi, na kwenye maeneo sita tofauti ya uwanja ule, kulikuwa kuna mioto iliyokuwa ikiwaka kutokana na marundo ya kuni zilizowashwa kwa kusudio maalum, ikitupa miale yake hewani na kuleta mwanaga kiasi eneo lile na wakati huo huo ikiacha baadhi ya maeneo ya uwanja ule kuwa na kiza kizito.
Dakika zilisonga na baada ya muda ulioonekana kuwa ni mrefu kuliko uhalisia wa muda wenyewe, miungurumo ya ndege ilisikika ikitokea angani upande wa mwisho kabisa wa eneo lile la wazi lililowekewe mioto, eneo ambalo liliiishia kwenye korongo refu sana lililoanguka umbali wa mita zipatazo mia nne kwenda chini, ambako kulikuwa kuna mto mkubwa sana uliokuwa ukipeleka maji kwa ghadhabu isiyosemekana hadi kwenye bahari ya Arabia (Arabian Sea), kilometa nyingi kusini mwa Pakistani.
Dargah Mandi haikuweza kabisa kuingilika kutokea upande ule hatari, ambapo hakuna binadamu ambaye angeweza kukiingia kijiji kile kwa kulikwea korongo lile kutokea kule chini kwenye mto ule mkali.
Na ni kutokana na uhatari wa eneo lile ndipo watalebani waliojaa hila na shuku zisizo ukomo, walipoelekeza kuwa ndege zile za misaada ziangushie marobota makubwa ya chakula na madawa kwenye eneo lile, kisha ndege zitakazoangusha misaada ile zigeuzie huko huko angani na kwenda zake. Hakukuwa na ruhusa kabisa kutua pale kijijini wala sehemu yoyote ya eneo walilolidhibiti vilivyo, la Waziristan ya Kaskazini.
Ndege ya kwanza ikatokeza kutokea nyuma ya milima mingi iliyolizunguka eneo lile, na mining’ono ya viherehere ikazagaa miongoni mwa wanakijiji. Ndege ikazidi kukurubia na ikazidi kushuka. Watalebani wengi wa shuku wakajiweka makini kwa bunduki na makombora yao…

***MNH! Tuwa ndo kaanza hivi?? Haya NJOO TUSOME zaidi hapo kesho muda kama wa leo.
 
RIWAYA: Wimbo wa Gaidi

MTUNZI: Hussein Tuwa

SEHEMU YA PILI

Na ni kutokana na uhatari wa eneo lile ndipo watalebani waliojaa hila na shuku zisizo ukomo, walipoelekeza kuwa ndege zile za misaada ziangushie marobota makubwa ya chakula na madawa kwenye eneo lile, kisha ndege zitakazoangusha misaada ile zigeuzie huko huko angani na kwenda zake. Hakukuwa na ruhusa kabisa kutua pale kijijini wala sehemu yoyote ya eneo lile walilolidhibiti vilivyo, la Waziristan ya Kaskazini.
Ndege ya kwanza ilitokeza kutokea nyuma ya milima mingi iliyolizunguka eneo lile, na minong’ono ya viherehere ikazagaa miongoni mwa wanakijiji. Ndege ikazidi kukurubia huku ikizidi kushuka. Watalebani wengi wa shuku wakajizatiti kwa silaha makini wakiwa miongoni mwa wanakijiji ambao sasa waliwakusanya kuwafanya kama ngao zao dhidi ya shambulizi lolote kutoka kwenye ndege ile. Na hata pale walipoanza kujizatiti namna ile, ndege nyingine tatu zilioneka kutokeza juu ya vilele vya milima iliyolizunguka eneo lile, na dakika kumi baadaye marobota makubwa yalionekana kuanguka kutoka angani. Mayowe yalizagaa, wanakijiji wakazidi kujirudisha nyuma ili kuwa mbali na eneo lile la wazi lililokuwa likimulikwa kwa ile mioto kutoka pembe sita tofauti. Lakini muda si muda, maparashuti yakafunuka kutoka kwenye marobota yale makubwa, nayo yakaanza kushuka taratibu huku yakinesanesa hewani kwenye anga ile ya usiku. Wanakijiji na watalebani walijitahidi kwa kadiri walivyoweza kufuatilia ushukaji wake kwenye kiza cha usiku ule wenye mbalamwezi hafifu, lakini haikuwa rahisi. Marobota yalizidi kushuka, kila moja kwa uelekeo wake…kila moja likiwa na shehena muhimu kwa wanakijiji wa Dargar Mandi ndani yake…lakini pia juu ya kila mgongo wa robota la vyakula vile, kulikuwa kuna siri kubwa….

________________

Makomando wanne walishuka kwa maparashuti wakiwa wamelala juu ya migongo ya yale marobota makubwa ya chakula cha msaada yaliyokuwa yakiangushwa na ndege za msalaba mwekundu kwenye kile kijiji cha Dargar Mandi. Wote wanne walikuwa wamevaa nguo maalum za kuzamia mbizi majini bila ya kulowa.
Lengo lao lilikuwa ni moja tu. Kumkomboa mtanzania aliyenaswa ndani ya kijiji kile, akiwa ni mmoja wa wapiganaji wa Al-Qaeda aliyetajwa kutafutwa na FBI baada ya shambulizi la kutisha kwenye ubalozi wa Marekani jijini Dar mnamo mwaka 1998. Sasa ngome iliyosalia ya Taleban ilikuwa inawahifadhi baadhi ya wapiganaji wa Al-Qaeda waliobakia, yeye akiwemo, ilikuwa imezingirwa na majeshi ya ushirika wa Marekani na Pakistani. Upinzani wa Taleban ulikuwa unaelekea kushindwa, na wamarekani wakiingia ndani ya ngome ile hakutakuwa na garantii ya mtanzania yule kunusurika.
Isipokuwa kama atatolewa mle ngomeni kabla majeshi ya washirika hayajavamia.
Lakini kivipi?
Ndipo nafasi ilipojitokeza pale Taleban walipokubali wanakijiji waletewe vyakula vya msaada kwa njia ile.
Marobota yanatua kwa vishindo ardhini na kuviringika shaghala baghala, kila moja upande wake. Makomando wanagaragazwa vibaya na yale marobota makubwa, lakini kwa kuwa walikuwa mahiri kwenye kazi zao na kwa kuwa walishalifanyia mazoezi mara kadhaa tukio lile kabla ya siku ile, kila mmoja alifanikiwa kujirusha pembeni na kubaki akiwa amejilaza kimya kwenye majani mafupi ya eneo lile, macho yao yakitafuta uelekeo ambao kila mmoja aliamini kuwa ni kusini ya pale walipoangukia, wakiyaacha yale marobota makubwa kabisa yakiendelea kubingirika huku yakijizonga na yale maparashuti yaliyoyashusha.
Kule kwa wanakijiji wenye njaa, watalebani walikuwa wakiyafuatilia yale marobota kwa umakini kwa kadiri walivyoweza. Kwa namna fulani ambayo sio bahati mbaya, marubani waliokuwa wakiyadondosha yale marobota waliyaangusha mbali na ile mioto mikubwa iliyowashwa kuwaelekeza ni wapi yale marobota yaangushwe, na hii iliwapa nafasi makomando walioshuka na marobota yale kuweza kutumia kiza kilichopo, mbali na ile mioto, ili kijiweka mbali na marobota yale na kwenda kwenye jukumu lililokuwa mbele yao. Jukumu kubwa na la hatari sana…wenyewe waliliita ni jukumu la kujitoa muhanga…suicide mission. Kwa ajili ya mtu mmoja ambaye hata hivyo hawakuwa wakimjua kiukaribu wowote zaidi ya kuwa alikuwa akihitajika sana na nchi kubwa duniani, na kwamba malipo yao kwa kujitoa kwao kwenye kulitekeleza jukumu lile, yalikuwa ni makubwa sana kiasi cha kuhalalisha lolote ambalo wangekutana nalo ndani ya eneo lile lililoshindikana kabisa hata kwa mataifa makubwa yenye uwezo mkubwa wa kivita…
Kila mmoja alibaki akiwa amelala mahala pake, akitafuta ishara aliyoandaliwa kuitafuta mara baada ya kutua ndani ya eneo lile kusudiwa. Wakaiona. Kutokea kwenye kona moja ya eneo lile, hatua kadhaa kutoka kwenye moja ya marundo ya mioto iliyokuwa ikiwaka eneo lile, taa nyekundu ilikuwa ikiwashwa na kuzimwa kwa kufuata utaratibu maalum. Iliwaka mara nne kwa kuacha kiasi cha kama sekunde moja baina ya muwako mmoja na mwingine, kisha ikafuatiwa na miwako mingine mitatu ya haraka haraka. Ilikuwa ni mbinu maridhawa kwani kwa pale ile toch maalum yenye mwanga mwekundu ilipokuwa ikiwakia, haikuwa rahisi hata kwa mtalebani mwenye macho makali kiasi gani, kuweza kuutofautisha mwanga ule kutoka kwenye mwanga wa moto uliokuwa ukiwaka hatua chachekutokea pale.
“Mmeona?” Mmoja alisaili kwa mnong’ono mkali.
“Yah!” Mwingine alijibu, na wengine wawili nao walituma majibu yao kuwa wameiona ile ishara. Lakini hakuna aliyetoka pale alipokuwa amelalia tumbo, akiwa na silaha yake mgongoni.
Kule kwa wanakijiji, watalebani waliendelea kujificha huku wakiyatazama yale marobota yakiendelea kubiringika huku wakiwa wamewaamuru wanakijiji wote kutulia mahala walipokuwa. Marobota yalipotulia kila moja upande wake, bado watalebani waliojaa shuku na wasiyemuamini yeyote isipokuwa wao wenyewe, wanawazuia wanakijiji kuyasogelea. Wanayatazama kwa umakini mkubwa yale marobota kutokea kule walipokuwa, wakitaraji jambo baya kutokea. Lakini halitokei. Hatimaye wanatoa amri kwa wanakijiji kuyaendea yale marobota. Kelele za shangwe zasikika pale wanakijiji wanapokurupuka na kuyakimbilia marobota yale, na ndipo kule walipokuwa, wale makomando wanatambaa kwa kasi sana kuelekea kule ile ishara ilipotokea. Wakati watalebani wako makini kufuatilia harakati za wanakijiji kule kwenye yale marobota ya vyakula, hawatakuwa makini kufuatilia kitu kingine na hawataweza kuona wakati wale makomando wakitambaa kwa uficho namna ile kuelekea sehemu tofauti na kule yale marobota yalipokuwa.
Makomando wanafika pale ishara ilipotokea, na hapo wanakutana na mshirika wao, mwenyeji wao, raia wa Pakistani aitwaye Imraan Gopang. Naye akiwa amevaa nguo kama walizovaa wao, ila akiwa amebeba begi mgongoni na akiwa amening’iniza bunduki mbili mgongoni kwake, Imraan anawaongoza kwa usiri bila ya kuongea lolote hadi kwenye shimo la wastani mithili ya yale mashimo ya vyoo yatumikayo kwenye jamii nyingi.
Haraka haraka wanaufunua mfuniko mzito wa zege wa shimo lile, na tochi zilizounganishwa kwenye bunduki zao zinawaonesha ngazi za chuma zilizojengewa kwenye ukingo wa shimo lile, ambazo zingewateremsha hadi kwenye kichanja kikubwa cha chuma kizito ambacho kilikuwa kinakatisha kutoka upande mmoja wa mtaro mkubwa kabisa wa chini ya ardhi, hadi mwingine, na kuwa kama daraja la aina fulani..
Wale makomando wanne na yule mwenyeji wao wanaingia ndani ya shimo lile na kuufunika ule mfuniko wake kwa ndani. Wateremka hadi pale kwenye kile kichanja kirefu cha chuma kizito, sasa wakiwa ndani ya mtaro mkubwa wa chini ya ardhi. Kiasi cha kama mita tatu hivi chini ya daraja lile, maji machafu ya kitongoji kile cha Waziristan yalikuwa yakitiririka kuelekea kwenye mdomo mpana wa mtaro ule, ambao ulichomoza kutokea kwenye uso wa jabali refu sana, kiasi cha kama kilomita moja zaidi kutokea pale walipokuwa. Njia nyingi kutoka pande mbali mbali za nchi ile zilikuwa zikimimina vinyesi na majitaka kwenye mtaro ule mkubwa kabisa, ambao nao ulisafirisha shehena ile ya uchafu kwa hiyo kilometa moja zaidi kutokea pale wale makomando walipokuwa na hatimaye kwenda kuitiririsha kwenye mto mkubwa kabisa uliokuwa umbali wa mita zipatazo mia saba kwenda chini kutokea kwenye uso wa jabali refu ambalo juu yake ndipo kijiji kile cha Dargah Mandi kilikuwepo.

***Watu wakazi mtaroni! Lengo lao litatimia kweli? NJOO KESHO muda uleule...
 
RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi

MTUNZI: Hussein Tuwa

SEHEMU YA TATU

TUWIENI RADHI KWA KUCHELEWA KUWEKA HII KITU HAPA KWA DAKIKA 25...

Njia nyingi kutoka pande mbali mbali za nchi ile zilikuwa zikimimina vinyesi na majitaka kwenye mtaro ule mkubwa kabisa, ambao nao ulisafirisha shehena ile ya uchafu kwa hiyo kilometa moja zaidi kutokea pale wale makomando walipokuwa na hatimaye kwenda kuitiririsha kwenye mto mkubwa kabisa uliokuwa umbali wa mita zipatazo mia saba kwenda chini kutokea kwenye uso wa jabali refu ambalo juu yake ndipo kijiji kile cha Dargah Mandi kilikuwepo.
Wanajitosha kwenye maji yale machafu na kuufuata ule mtaro kuelekea kule vinyesi vinapotokea, zile nguo zao za kupigia mbizi majini zikiwakinga dhidi ya uchafu ule uliowafika viunoni, puani wakiwa wamevijisha viziba pua kujikinga na harufu mbaya na kali ya maji yale machafu.
Ikiwa ni wazi kuwa alishafika eneo lile peke yake hapo kabla, Imran Gopang anawaongoza hadi kwenye ngazi za chuma zilizoegeshwa kwenye ukuta wa mtaro ule, ambapo kwa lugha za ishara anawaelekeza kumulika paa la mtaro ule kwa kurunzi zao kali. Baka la unyevunyevu lililo kwenye dari lile linawajuza kuwa pale ndio mahala walipopakusudia.
Wanaangalia saa zao. Muda bado. Wanasubiri. Wote kimya kabisa. Dakika ishirini na tano zinapita wakiwa wima kwenye mtaro ule mkubwa, wakiwa wamezama hadi viunoni kwenye maji ya vinyesi.
Muda unawadia.
Wanapeana ishara na kuanza kutekeleza jukumu lao. Wanaisimamisha ile ngazi kwa kuishikilia usawa wa lile baka lililokuwa kule darini. Mmoja wao, mtaalamu wa milipuko, anapanda kwenye ile ngazi iliyoshikiliwa wima na wenzake na kubandika milipuko maalum, kitaalamu ikijulikana kama “plastic explosives”, kwenye ile sehemu yenye lile baka la unyevu. Anateremka haraka, na yeye na wenzake wanajisogeza pembeni, mbali na lile baka lililowekewa milipuko. Imraan anatoa wavu maalum kutoka kwenye begi lililokuwa mgongoni kwake, na haraka haraka makomando wanashirikiana kuukunjua ule wavu mpana, mgumu, na mahsusi kwa kazi waliyokuwa wanataka kuufanyia.
Wawili wanakamata upande mmoja wa wavu ule wakiwa ubazi mmoja wa mtaro, ilhali makomando wengine wawili wakishikilia upande mwingine wa ule wavu, wakiwa ubazi mwingine wa mtaro. Ule wavu ukawa umewamba mithili ya kitanda cha kamba moja kwa moja chini ya lile baka. Imraan Gopang anatupia lile begi alilokuwa nalo pale juu ya ule wavu na kuliacha pale.
Wanatulia, wanasubiri. Kimya kabisa. Maji machafu yanasafiri chini yao kuelekea kwenye mdomo wa mtaro ule, mapanya buku yakiogelea kwenye maji yale na kuwagonga gonga miguu yao. Hawajali. Wanatupiana macho kwenye ule mwanga hafifu, wakiutaraji muda muafaka wa kutekeleza wajibu wao ule wa hatari, ilhali yule mtaalamu wa vilipuzi akiwa makini maradufu na kifyatulio chake mkononi.
Hatimaye muda unawadia. Mtaalamu akawaashiria wenzake kwa kichwa kuwa alikuwa anatekeleza lililowafikisha pale muda ule na wenzake wakajizatiti kila mmoja mahala alipokuwa, tahadhari kubwa ikiwavaa wote.
Akabonyeza kifyatulio, na wote wakaficha nyuso zao huku wakigeukia kwenye kuta za ule mtaro mkubwa.
Mlipuko mkubwa ulisikika mtaroni ilhali kuta na sakafu za mtaro ule wa chini ya ardhi vikitikisika kana kwamba kulikuwa kuna tetemeko la ardhi lililokuwa likipita. Ile sehemu iliyotegewa mabomu ilipasuka, mapande ya zege na plasta yaliporomoka kutoka kule juu na kuanguka kwenye yale maji machafu yaliyorushwa huku na huko na kuzilowesha zile nguo za kuzamia mbizi walizovaa wale wapiganaji mahsusi.
Kisha kukawa kimya.
Makomando wakaelekeza kurunzi zao kali pale ambapo palitegwa yale mabomu kutazama matunda ya kazi yao, lakini walichokiona sicho walichokitarajia. Lile eneo lililokuwa na unyevu hapo awali sasa lilikuwa limeharibika na kumegeka vibaya. Nyufa nyingi zilikuwa zimetawanyika kila upande kutokea pale palipokuwa pamezungushiwa vile vilipuka, maji yakichuruzika kutokea kule juu kupitia kwenye baadhi ya nyufa zile.
Lakini bado lile eneo lilionekana madhubuti. Mabomu yaliyotegwa hayakufanya madhara yaliyotarajiwa kwenye eneo lile.
Doh!
“Ina maana hukuweka vilipulizi vya kutosha?” Mmoja wa makomando alimuuliza mtaalamu wa vilipuzi.
“Naijua kazi yangu jamani...” Mtaalamu wa vilipuzi alinong'ona kwa msisitizo.
“Unajua huu mtaro umejegwa ndani ya jabali lililochongwa tangu enzi na enzi...ni jiwe la mwamba mgumu sana hili. Hata sijui hao mababu na mababu wa zamani waliwezaje kuuchimba mtaro huu... " Imran Gopang alidakia kwa hamaniko, akaendelea, “...ni kama yale mashimo ya tora bora...ya tangu enzi za Nabii Suleiman! Serikali ilikuja kuongezea tu kujengea hili liji-karavati kubwa ndani yake…”
“Sasa muda unazidi kwenda...mashambulizi ya anga yataanza muda si mrefu. Nashauri tufanye la kufanya sasa...kabla nasi hatujaangamizwa pamoja na watalebani humu, demshitt!” Mwingine alikoroma kwa kunong'ona.
“La kufanya kama nini kwa mfano...? Misheni yote ilitegemea kuilipua hii sehemu, na sasa...”
“Hatuwezi kulipua tena…?” Alidakia mwingine.
“NO! Kiwango cha vilipuzi nichoweka kilikuwa sahihi...ila nadhani huu mtaro kama alivyosema kamanda hapa, umekuwa imara kuliko tulivyodhania...kama ningezidisha viwango, mtikisiko ungekuwa mkubwa kiasi cha kuwashitua mapashtuni na watalebani huko juu...hatutaki iwe hiv...” Mtaalamu wa vilipuzi aliipinga hoja kwa wahka, lakini hakumaliza kauli yake.
Kishindo hafifu kilisikika kutoka pale juu ya paa la mtaro ule. Wote wakamakinika mara moja, wale wanne wakauvuta kwa nguvu ule wavu kila mmoja kutokea upande wake. Kikasikikika kishindo kingine kikubwa zaidi. Imraan Gopang akaweka silaha yake sawa kuelekea kule juu, na ghafla mapande ya mawe, udongo, vumbi na beseni la choo cha kuchutama vikaporomoka kutoka kule juu palipowekewa vilipulizi hapo awali, sanjari na ukelele wa hamaniko, maji yenye kinyesi, na mtu mmoja aliyeporomoka na vitu vyote vile kutoka kule juu.
E bwana we!
Jamaa alidunda kwenye ule wavu, akatupwa tena hewani na kuangukia tena kwenye ule wavu, akatupwa tena mara tatu zaidi kabla hajaagukia tena pale wavuni na kubaki akiwa amelalia tumbo.
"Yeeeah! Kazi imetimia! Hakuna muda wa kupoteza tena!" Mmoja wa wale makomando walioushikilia ule wavu alipayuka wakati yule mtu akijiinua kutoka pale kwenye wavu ambao bado ulikuwa umeshikiliwa kwa nguvu na wale makomando wanne...mmoja kwenye kila kona ya wavu ule maalumu.
Kurunzi kali ikammulika usoni yule mtu aliyeporomoka na mawe kutoka kule juu...naye haraka akajiziba uso kwa mikono yake, lakini sio kabla kurunzi ile haijawaonesha wale makomando kuwa alikuwa amevaa nguo za kitalebani na uso wake ulikuwa umezingirwa na madevu mengi.
"Toa mikono usoni hiyo!" Imraan Gopang, ambaye ndiye pekee aliyeweza kushika bunduki wakati ule, alimkemea kwa ukali huku akiikoki bunduki yake tayari kumchabanga risasi yule mtu kama ikibidi.
Jamaa akashusha mikono na kubaki akiwa amefinya uso akiuacha mwanga mkali wa ile kurunzi iliyounganishwa na bunduki ya Imraan Gopang ummulike usoni, lakini hakubaki kimya.
"Sa...samahani jamani! Mimi ndiye muhusika...huko juu sio salama sana...kishindo cha mlipuko kimesikika kiasi. Wakigundua kilichotokea tutakutwa hapa..." Jamaa kutoka juu alisema kwa mashaka, akiongea kwa lugha ya kipashtuni fasaha.
Makomando walimtazama kwa sekunde chache tu zaidi, wakiionanisha sura yake na picha yenye sura ya mtu ambaye ndiye walikuwa wamefika pale mtaroni kwa njia ile ya hatari kabisa kumuokoa; picha ambayo wote waliitazama na kuikariri kabla ya kuianza ile misheni yao ya hatari.

****Ndiye???
 
RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi

MTUNZI: Hussein Tuwa

SEHEMU YA NNE

"Sa...samahani jamani! Mimi ndiye muhusika...huko juu sio salama sana...kishindo cha mlipuko kimesikika kiasi. Wakigundua kilichotokea tutakutwa hapa..." Jamaa kutoka juu alisema kwa mashaka, akiongea kwa lugha ya kipashtuni fasaha.
Makomando walimtazama kwa sekunde chache tu zaidi, wakiionanisha sura yake na picha yenye sura ya mtu ambaye ndiye walikuwa wamefika pale mtaroni kwa njia ile ya hatari kabisa kumuokoa; picha ambayo wote waliitazama na kuikariri kabla ya kuianza ile misheni yao ya hatari.
“Ndiye yeye...lets get out of here!” Mmoja wa makomando alisema, akimaanisha kuwa waondoke eneo lile haraka, muda wa kuwa tayari wameshathibitisha kuwa aliyeporomoka kutoka kule juu ndiye mlengwa wa misheni yao ile ya kifo.
"Toa hizo nguo…vaa zilizomo humo kwenye hilo begi hapo...haraka!" Imraan, ambaye ndiye alikuwa kiongozi wa operesheni ile aliamuru. Haraka sana jamaa akatekeleza. Kutoka kwenye lile begi lililokuwa pale juu ya ule wavu alioangukia, alitoa nguo za kupigia mbizi kama zile walizovaa wale makomando, ambazo ziliuganika moja kwa moja kutoka unyayoni hadi kichwani kuwa kama kofia iliyobana na kuacha sehemu ya uso tu, na kuzivaa kwa pupa. Alipomaliza, Imraan akachomoa bunduki nyingine kama zile walizokuwa nazo yeye na wale wenzake iliyokuwa ikining’inia mgongoni kwake na kuitupia pale juu ya ule wavu.
“Kamata hiyo tuondoke hapa kabla maonesho ya fataki hayajaanza!”Alimkoromea. Jamaa kutoka juu ya paa la mtaro aliiokota ile bunduki na kujirusha mtaroni kwenye yale maji ya kinyesi bila hata ya kuambiwa. Wale makomando wanne walioshuka Dargah Mandi kwa yale marobota ya chakula cha msaada waliuacha ule wavu ukiangukia majini na kwa pamoja wale wanaume sita wakaanza kukimbia kwa haraka yenye tahadhari kueleka kwenye mdomo wa mtaro ule, wakifuata mkondo wa yale majitaka yaliyowafika viunoni.
Hawakuwahi kuufikia mdomo wa ule mtaro…
***********
Kule uwanjani baadhi ya wanakijiji wa Dargah Mandi walikuwa wakiyapandisha kwa taabu magunia mengi yenye uzito wa kilo mia kila moja, kwenye malori matatu ya watalebani chini ya ulinzi mkali wa wale wanamgambo wenye roho mbaya. Hii ilikuwa ni baada ya kurarua mikanda maalumu ya khaki ngumu kabisa iliyokuwa imeyabeba yale marobota makubwa yaliyotengenezwa kwa mbao maalumu ambazo ndani yake ndio kulikuwa kumepangiliwa yale magunia makubwa...yakiwa yamesheheni mchele, ngano, sukari na madawa mbali mbali ya binaadamu hususan kwa kutibu maradhi ya milipuko na yale yatokanayo na utapiamlo.
Ilikuwa ni taswira ya kusikitisha kwa kweli, kwani walionekana wazee na vijana waliokondeana kwa njaa ambayo pia iliwafanya wasiwe na nguvu, wakijitutumua kuburura na kuyapandisha kwenye malori yale magunia, ilhali wale wanamgambo wenye afya kuliko wao, wakiwa wamewasimamia kwa mitutu ya bunduki huku wakiwashinikiza kwa ukali na kelele, kuwa wafanye haraka kupandisha chakula kile kwenye yale malori; chakula ambacho wanakijiji wale waliokondeana wala hawakuwa na matumani ya kukipata, pamoja na kwamba kilikuwa kimeshushwa pale kijijini kwa njia ile ya hatari kabisa, kwa ajili yao.
Pembezoni kabisa mwa uwanja ule, akina mama na watoto walikuwa wamejikunyata wakiwa na mabakuli, makapu na masinia mapana kabisa, wakishuhudia namna tumaini lao la mlo walioukosa kwa kipindi kirefu, likishehenezwa kwenye yale malori ya watalebani, wakitaraji na wao kugawiwa chakula kile na kukipeleka majumbani mwao kikiwa kwenye vile vyombo vyao na kunusuru maisha yao kutokana na kifo cha unyonge kabisa duniani...kifo cha njaa.
Na katikati ya harakati zile zilizokuwa zikiendelea pale uwanjani usiku ule, mtoto mmoja wa kike aliushika na kuutikisa kwa nguvu mkono wa mama yake, wahka uliomkumba ukijidhihirisha kwenye nguvu aliyoiweka kwenye mtikiso ule. Mama aliyekuwa amemakinika na kilichokuwa kikiendelea kule kwenye magunia ya chakula alimgeukia kwa kukereka huku akiwa amekunja uso tayari kumkaripia, lakini hofu aliyoiona usoni kwa bintiye ilimfanya ageuzie uso wake angani kufuatisha kule ambako kidole chenye kutetema cha mwanaye kilikuwa kinaoneshea...na ndipo sanjari na kile alichokiona kule angani, miungurumo ya kwanza wa zile ndege za ajabu ilipoyafikia masikio yake pamoja na ya wanakijiji wenzake aliokuwa nao pale uwanjani.
"Eee Khuda!" Mama alimtaja mola wake kwa woga mkubwa na punde hiyo hiyo sauti za wanakijiji wenzake walioona kile ambacho yeye na bintiye walikiona, zilimezwa na sauti kali mithili ya mbinja ndefu kabisa ikisindikizwa na mwale wa moto uliopasua anga ya usiku ule kutokea kwenye moja ya ndege zile za kivita zilizoshindikana. Wanakijiji walijitupa chini kwa taharuki na mayowe makubwa wakiogopea uhai wao duni...na hapo hapo kishindo na mlipuko mkubwa vilisikika umbali wa mita kadhaa kutoka pale walipokuwa. Watalebani waliokuwa wanawalinda wale wanakijiji walihamanika vibaya, na kuwah-kika vilivyo.
"Tunashambuliwaaaaa!" Mmoja wao alipayuka huku bila ya kufikiri akifanya lile ambalo mafunzo yao ya kijeshi yalimuelekeza, kwa kumnyakua mmoja wa wanakijiji aliyekuwa karibu naye na kumuweka mbele yake kama ngao huku akigeuka huku na huko na bunduki yake macho yakiwa yametumbuka.Wenzake walijitupa chini ya yale magari yao huku wakitapatapa na bunduki zao pasina kuelewa ni wapi shambulizi lilikuwa limetokea na nani alikuwa anashambulia.
Mbinja nyingine mbili zilirindima angani zikifuatiwa na ile miale mirefu na mikali ya moto iliyopasua anga mithili ya vimwondo...na sekunde ile ile milipuko mingine miwili ilisikika kutokea sehemu mbali na pale walipokuwa...mioto mikubwa kabisa ikiruka hewani na vumbi kali likijichanganya na hewa ile ya ubaridi wa usiku.
"AAAH ni mashambukizi ya droni! Wanashambulia kambi yetu… wanaharamu!" Mtalebani mwingine alibainisha kilichokuwa kinatokea kwa hamaniko lililobadilika na kuwa ghadhabu.
"Nguruwe weupe! Yaani wamarekani wametutega kwa msaada wa chakula kwa raia kumbe walikuwa wana lao jambo??! Ua wanakijiji wooot..." Mwingine alidakia lakini kabla hajamaliza mbinja nyingine fupi ilisikika na muda huo moja ya yale magari yao pale uwanjani likasambaraishwa vibaya kwa kombora kutoka kwenye moja ya zile ndege zisizotumia rubani.
Loooh…Mtafaruku!
Watalebani na wanakijiji kadhaa waliokuwa kwenye lile gari walisambaratishwa vibaya na bomu lile. Bomu la pili likalisambaratisha lile lori la pili...ambalo safari hii halikuwa na mtu lakini hata hivyo lilijeruhi watalebani na baadhi ya wanakijiji waliokuwa wakikimbia kwa woga na mayowe mengi.
Vita haina macho.
Hekaheka ikashamiri...watalebani na wanakijiji wote wakawa wanakimbia sasa, kila mmoja akiwaza "yarabi nafsi yangu…!"
Zile ndege zisizo na rubani maarufu kama "drones" zikaachana na yale malori na kuendelea kutupa makombora kule katikati ya kijiji, hususan kwenye jengo moja tu ambalo vipimo vya satelaiti vilionesha kuwa ndimo ambamo wafuasi waliobakia wa hayati Osama Bin Laden walikuwa wamehifadhiwa na wale washirika wao hatari, wataleban.
Mzizimo wa usiku ule wenye baridi ulibadilika na kuwa mrindimo wa milipuko ya makombora na fukuto la hofu.
**********
Kiasi cha kama dakika moja kabla yule mtoto wa kike kule uwanjani hajaziona zile ndege za kuvizia na kumgutusha mama yake, kule mtaroni makomando waliokuwa wakitembea haraka na kwa tahadhari kuelekea kwenye ndomo wa karavati lile kubwa kabisa la chini ya ardhi waligutushwa na kishindo cha mtumbukio wa kitu kizito majini, sanjari na ukelele wa ghadhabu.
"Ah! Tumeshitukiwaa!" Jamaa aliyeporomoka na beseni la choo kutoka kule juu ya paa la ule mtaro aliropoka huku akijirusha pembeni na kujibabatiza kwenye ukuta mnyevu wa ule mtaro, na hapo hapo milipuko ya risasi ikasikika kutokea nyuma yao.
"Pumbaaavvvv!" Mmoja wa makomando alilaani huku akigeuka na kumimina risasi kule walipotokea ilhali wale wenzake nao wakijitupa pembeni huku nao wakitupa risasi. Na hata pale alipokuwa akitupa macho kule alipotokea huku naye akiwa ameshikilia imara bunduki yake, mpiganaji aliyeshuka na beseni la choo kutoka kule juu aliona watalebani kadhaa wenye silaha wakirukia pale mtaroni kutokea kwenye lile tundu alilolitoboa kwa taabu sana kwenye sakafu ya choo cha lile jumba alilokuwamo kwa masiku kadhaa, sakafu ambayo kutokea kwa pale alipokuwa ilikuwa ndio sehemu ya paa la ule mtaro unukao.
"Tusonge mbeleee!!" Imraan Gopang alibwata huku akitupa risasi kuwaelekea wale watalebani ilhali akirudi nyuma akiwa amejibaza kwenye ukuta wa mtaro. Milipuko ya risasi ndani ya ule mtaro ilirindima kwa kelele kubwa isivyo kawaida, sauti za milipuko ya bunduki zao zikitupwa huku na huko mtaroni na kubaki mle mle bila ya kuwa na mahala pa kutokea. Kurunzi kubwa iliwamulika makomando...watalebani walikuwa wakiwakimbilia kwa jazba mle mtaroni...wawili walidunguliwa na kupiga mieleka huku wakiachia mayowe. Risasi ilichimba ukuta wa mtaro sentimeta chache kutoka pale jamaa alipojibanza...naye akazinduka. Akatupa risasi mbili...watalebani wawili zaidi wakaenda chini. Mmoja wa wale wenzake akamkamata kiwiko na kumvuta kibabe kuelekea kwenye mdomo wa ule mtaro...ambao ulikuwa kiasi cha kama mita hamsini hivi kutokea pale walipokuwa.
"Achana nao...twende!" Jamaa alimkoromea. Hapo hapo mwenzao mmoja akaachia yowe la uchungu...risasi moja ilimpata begani naye akatupwa vibaya kwenye ukuta wa mtaro na kuangukia majini.

***Kimenuka!
 
RIWAYA: Wimbo wa Gaidi

MTUNZI: Hussein Tuwa

SEHEMU YA TANO

ILANI:
Hii ni kazi ya kubuni. Majina, wahusika, mahala na matukio yote yaliyotajwa katika riwaya hii ni aidha matokeo ya ubunifu wa mtunzi au yametumika kibunifu tu. Vilevile, kufanana kwa aina yoyote na mtu yeyote wa kweli, aliye hai au aliyekufa, matukio au maeneo yoyote ya kweli ni kwa lengo la kuleta uhalisia katika kisa cha riwaya hii.

TWENDE KAZI SASA...

Akatupa risasi mbili...watalebani wawili zaidi wakaenda chini. Mmoja wa wale wenzake akamkamata kiwiko na kumvuta kibabe kuelekea kwenye mdomo wa ule mtaro...ambao ulikuwa kiasi cha kama mita hamsini hivi kutokea pale walipokuwa.
"Achana nao...twende!" Jamaa alimkoromea. Hapo hapo mwenzao mmoja akaachia yowe la uchungu...risasi moja ilimpata begani naye akatupwa vibaya kwenye ukuta wa mtaro na kuangukia majini. Imraan Gopang akamnyanyua haraka.
"Tukingenii!" Alipiga kelele huku akimburura yule mwenzao aliyejeruhiwa. Makomando waliobaki wakajipanga pamoja na yule mwenzao waliyekuja kumkomboa kutoka kwenye ngome ile ya watalebani iliyojengwa juu ya ule mtaro mkubwa na kujibu mapigo ya watalebani kwa kuwamiminia risasi za mfululizo huku wakizidi kurudi kinyumenyume kuuelekea mdomo wa mtaro ule waliokuwamo, na katikati ya majibizano yale ya risasi, kurunzi kubwa ya watalebani ilikuwa ikiranda huku na huko mle mtaroni, ikimsaka mtu aliyeshuka na beseni la choo kutoka kule juu, ambaye sasa watalebani walijua kuwa ndiye msaliti wao...ndiye msaliti wa Osama bin Laden. Ikammulika.
"Yuleee...!" Yowe kutoka kwa mtalebani mwenye kurunzi lilienda sambamba na mwanga wa kurunzi ile uliomnasa yule jamaa, na hapo mmiminiko wa risasi za watalebani ukamgeukia yule jamaa aliyekuwa akibururwa na yule mwenzake. Upesi sana jamaa akamsukuma yule mwenzake katikati ya mtaro huku naye akijitupa huko huko kutoka kule ukutani walipokuwa wamejibanza huku wakikimbia. Ukuta wa mtaro kwa pale walipokuwapo nukta moja tu iliyopita ukachabangwa marisasi bila mpangilio. Akiwa kwenye yale maji ya kinyesi katikati ya mtaro jamaa akajigeuza na kutupa risasi mbili za haraka na ghafla kiza kikatawala mtaroni sanjari na yowe la uchungu kutoka kwa yule mtalebani aliyekuwa ameishika ile kurunzi kubwa baada ya risasi ya kwanza ya yule jamaa kumdungua yule mtalebani na ya pili kuipasua vibaya ile kurunzi.
Mayowe yasiyo mpangilio yalisikika miongoni mwa watalebani walioachwa kizani.
"Safi sana bro!" Yule mwenzake alimpongeza jamaa, ambaye hakujisumbua kumjibu.
"Kila mtu awahi kule mbele gaddemmit...mashambulizi yataanza muda wowote sasaa!" Imraan Gopang alibwata huku akizidi kumburura yule mwenzao aliyejeruhiwa. Bila ya kusubiri kuhamasishwa zaidi jamaa aliyeshuka na beseni la choo alivuta pumzi nyingi mapafuni na kupiga mbizi kwenye yale maji ya kinyesi.
Na hapo kishindo hafifu kilisikika kutokea juu ya ule mtaro, ukifuatiwa na mtikisiko mkubwa kabisa ulioyatikisa yale maji machafu mle mtaroni kiasi cha kufanya mawimbi hafifu.
"OOOH! Tayari yameanza huko juu!" Mmoja wa makomando alimaka huku naye akichupa mbizi kwenye yale maji machafu. Watalebani walipigwa butwaa kwa kutoelewa kilichokuwa kikitokea, lakini butwaa yao haikudumu sana kwani hapo kombora jingine lilishuka kule juu kwanye ngome yao na kupitiliza moja kwa moja hadi kwenye paa la mtaro ule, likaupasua vibaya na kujikita mtaroni kutokea kule juu.
Hatari!
Watalebani kadhaa waliokuwa karibu zaidi na usawa wa jengo la ngome yao kule juu walisambaratishwa vibaya wakati mapande ya mawe, udongo na matofali ya ngome yao kule juu vilipoporomokea mle mtaroni. Maji yale machafu mle mtaroni yalisukumwa kwa nguvu kuelekea kule kwenye kinywa cha mtaro ule mkubwa huku yakifanya wimbi kubwa kabisa lililokaribia kugusa paa la mtaro ule.
Na ndipo wale makomando waliokuwa wamekaribia kuufikia mdomo wa mtaro ule waliposombwa kwa nguvu na maji yale na kutupwa vibaya sana nje ya mtaro ule...kila mmoja akipiga mayowe kwa woga na wahka, kwani
ingawa tangu awali walikwa wamepanga kutoroka kutoka kwenye mtaro ule kwa njia ile...hili la kusukumwa kwa nguvu namna ile kwa wimbi zito la maji yale halikuwa sehemu ya mpango wao...
***********
Yale maji machafu yalitupwa kutoka kwenye kinywa cha mtaro ule kilichochomoza kutoka kwenye uso wa jabali kali na kuanguka kwenda chini kwa umbali wa mita mia saba kutoka kwenye uso wa jabali lile lisilopandika. Makomando walianguka kutoka kule juu pamoja na maji yale huku wakipiga mayowe na roho zikiwapaa, kwa muda ambao ulionekana kuwa ni milele, ingawa kwa hakika iliwachukua dakika zisizozidi kumi tu kutoka kule juu hadi pale walipotoswa kwa kishindo kikubwa sana kwenye maji ya mto mkubwa uliokuwa ukipita chini ya jabali lile, ambapo majitaka ya mji mzima kutoka kule juu yalichanganyika na maji mengi zaidi ya mto ule mkubwa na kusombwa yakiwa yamechanganyika na maji ya mto ule kuelekea kaskazini zaidi ya kijiji kile cha Dargah Mandi ambacho kutokea kule mtoni, kilikuwa umbali wa mita mia saba juu kutoka usawa wa bahari.
Pamoja nao ilianguka miili isiyo hai ya watalebani waliokuwa wakikabiliana nao kule mtaroni.
Kila mmoja aliibukia upande wake pale mtoni huku akitweta na kutapatapa hali akisukwasukwa na mkondo wa ule mto wenye nguvu. Kwenye kiza kizito cha usiku ule, jamaa aliona vijitaa vyekundu viking’aa kutoka sehemu mbali mbali mle mtoni. Aliinama na kujitazama kifuani, akagundua kuwa ile nguo aliyovaa nayo ilikuwa ina kitufe kilichokuwa kikitoa mwanga mwekundu mara baada ya kuwa kimekutana na maji. Hapo akajua ni kwa nini wale waokozi wake walimshurutisha kuvaa nguo zile.
"Wote salama?" Imraan Gopang alipiga kelele ili asikike juu ya sauti ya mfoko wa maji ya mto ule huku akigeuka huku na huko kuwasaka wenzake. Kila mmoja aliitika kutokea alipokuwa, akiwemo yule mwenye ndevu nyingi.
“Tuna majeruhi mmoja! Yu-hali gani?” Imraan alimaka.
“Nitaishi kamanda! Twenden’zetu!” Komando aliyejeruhiwa aliwatoa hofu wenzake.
“Okay, tuongelee kufuata mkondo wa maji…tutakutana na mwenzetu huko mbele!” Imraan alibwata, na kuanza kuogelea. Wenzake wakafuata, na kiasi cha kama dakika kumi na tano baadaye waliona tochi ikiwashwa na kuzimwa kutokea mbele yao.
“Tulieni!” Imraan aliamuru na wote wakatulia walipokuwa, wakijitahidi kutosombwa na mkondo wa ule mto mkubwa. Waliitazama ile tochi ikiwashwa na kuzimwa kufuatisha ishara fulani ambayo walitakiwa waitambue. Baada ya kuitazama ile tochi ikiwashwa na kuzimwa mara kadhaa, wakajiridhisha.
“Okay, mtu wetu yule. Twendeni… ila tahadhari ni muhimu!” Imraan alisema, na kwa ukimya wa hali ya juu makomando na yule mtu waliyetoka kumkomboa waliogelea kuifuata ile tochi na hatimaye kulifikia lile boti maalum.
“Misheni imetimia?” Sauti nzito kutoka kwenye boti ilisaili.
“Misheni gani?” Imraan aliuliza, na jamaa mwenye ndevu nyingi aliguna kwa mshangao.
“Safi! Ingeni tuondoke eneo hili…mbwembwe ndio kwanza zinaaza huko juu…” Sauti kutoka kwenye boti ilisema, na jamaa aliyekombolewa akashusha pumzi za ahueni. Kumbe majibizano yale ilikuwa ndio ishara yao ya kutambuana. Hapo taa hafifu ziliwaka kwenye lile boti na makomando wakashudia watu wengine watatu wakiwa na silaha nzito, ihali yule aliyekuwa akijibizana na Imraan akiwa anatabasamu.
“Kama kawaida yako Imraan…kazi imeenda vizuri!” Yule mtu ambaye alikuwa ni mmarekani mwenye asili ya Afrika alisema huku akimshika mkono Imraan na kumsaidia kupanda ndani ya lile boti, wakati wale makomando na yule mtu waliyetoka kumtorosha wakiparamia kwa pupa ndani ya lile boti, ambalo muda huo huo liliwashwa na kuondoka eneo lile kwa mwendo wa kasi. Nyuma yao, ndege zaidi zilikuwa zikielekea Dargah Mandi kupelekea mashambulizi zaidi…na wakati huo huo ndege nyingine mbili zilikuwa zikipeleka marobota mengine ya vyakula vya msaada. Safari hii, yale marobota hayakuwa na komando yoyote aliyejilaza juu yake…

***Uuumphh! Wametoka. Nini kitafuata sasa? Ndio stori imeishia hapa?
LA HASHA...NJOO TOSOME zaidi hii kitu hap
 
[22:05, 4/26/2016] ZAMIRA RIWAYA: RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi
MTUNZI: HUSSEIN TUWA
SEHEMU YA SITA
Nyuma yao, ndege zaidi zilikuwa zikielekea
Dargah Mandi kupelekea mashambulizi zaidi…na
wakati huo huo ndege nyingine mbili zilikuwa
zikipeleka marobota mengine ya vyakula vya
msaada. Safari hii, yale marobota hayakuwa na
komando yoyote aliyejilaza juu yake…
_______________
Wakati boti ikipasua maji kufuata mkondo wa
mto ule, makomando walibadili zile nguo za
kupigia mbizi na kuvaa za kawaida. Wawili kati
yao waliokuwa na asili ya kiasia walivaa "salwan
khameez", nguo maarufu za ki-pakistani, ilhali
yule mwingine aliyejeruhiwa kwa risasi aliyekuwa
wa asili ya afrika, alikuwa akisaidiwa kutolewa
zile nguo kabla ya kupatiwa huduma haraka
haraka na tabibu mmoja waliyemkuta mle botini.
Ile risasi ilimkwaruza tu sehemu ya bega hivyo
haikuwa na madhara makubwa sana kwake. Yule
mmarekani mweusi alimtupia nguo za kipakistani
yule jamaa aliyechoropolewa kutoka kwenye
ngome ya watalebani.
"Vaa hizo nguo!" Alimkoromea.
Jamaa akatii bila kutia neno, ingawa muda wote
akili yake ilikuwa ikimtembea kwa kasi sana.
Aliona wale watu wengine kama watati hivi
waliokuwa pamja na yule mmarekani mweusi mle
botini wakiwa makini sana na bunduki zao, na
mara moja alibaini kuwa umakini wao wote
ulikuwa umeelekezwa kwake yeye, na si kwa
wale wenzake alioibuliwa nao kutoka mle mtoni.
Upande mwingine wa boti ile, mpakistani Imraan
Gopang naye alikuwa akivaa kanzu safi ya kijivu
juu ya suruali nyeupe ya "panjabi", baada ya
kutoa zile nguo za kuzamia mbizi alizokuwa
amevaa. Akiwa makini sana bila ya kujionesha
kuwa yuko kwenye hali ile, jamaa alivua fulana
mchinjo aliyokuwa ameivaa chini ya zile nguo za
kuzamia mbizi...na ndipo wale wenzake aliokuwa
nao mle ndani walipouona mwili wake kuwa
kutumia mwanga wa taa zilizokuwa ndani a lile
boti.
"Eeh...!" Mmoja wa wale makomando wa kiasia
alimaka huku kama wale wenzake na wale
walinzi waliowakuta mle botini, akilikodolea
macho kovu baya kabisa lililotambaa kutokea
upande wa kushoto wa kifua cha yule jamaa,
hadi ubavuni kwake. Lilikuwa ni kovu lenye
michirizi mitatu mizito iliyotokea kwenye vishimo
vitatu vilivyochimbwa pale kifuani na kuacha
makovu yenye vishimo. Yaani ni kama vile kuna
mtu katika siku za nyuma alimshindilia kwa reki
la kukusanyia majani kifuani, na kujaribu
kuzikusanya ngozi yake kutokea pale kifuani hadi
chini kabisa ya ubavu wake wa kushoto. Hakika
lilikuwa ni kovu baya sana.
"Nini?" Jamaa aliuliza huku akiwatembezea
macho wote mle botini, hali akiwa kidari wazi,
ameshikilia shati la kipakistani alilotupiwa na yule
mmarekani mweusi, ambaye ndiye pekee
aliyeonekana kutolishangaa kovu lile.
"Umekutwa na nini hapo komredi? Hilo kovu...."
Imraan Gopang akawasilisha swali ambalo bila
shaka lilikuwa likirindima vichwani mwa wale
wenzake. Jamaa aliinama na kujitazama pale
penye kovu, kisha akawatazama wale wenzake
kwa uso uliosajili hali ya kutokuwa na jibu kwa
swali aliloulizwa.
"Nyie ni wapiganaji halafu mnaogopa makovu?"
Aliwauliza badala ya kuwajibu, huku akilivaa lile
shati refu la kipakistani, na kulificha kovu lake.
Jamaa walichanganyikiwa kiasi kwa jibu lile.
"Ah...mimi nimepitia makabiliano ya kila namna
komredi...lakini sisi ni watu tunaocheza kwa
bunduki, risasi na mabomu kaka...hilo ulilo nalo?
Si kovu litokanalo na chochote kati ya hivyo
aisee..." Imraan Gopang alimjibu.
Kwa mara ya kwanza jamaa akaachia tabasamu,
na alivyofanya vile, sura yake ngumu ikabadilika
na kuwa ya kuvutia kwa namna fulani ya ugumu.
"Basi bado hujapitia makabiliano ya kila aina
komredi..." Alimjibu bila kujali.
"Okay...imetosha jamani..." Yule mmarekani
mweusi alidakia, akaendelea, "Tumalize hii
biashara Imraan..."
"Nyie ni kina nani kwani....?" Jamaa akauliza
lililokuwa likimtatiza kichwani mwake tangu
aporomoke kutoka kwenye dari la ule mtaro wa
majitaka.
“Hutaki kujibu maswali yetu, unataka tukujibu ya
kwako?” Komando mwenye asili ya kiafrika
alimuuliza, sasa akiwa amefungwa bandeji
kitaalamu begani. Alikuwa amevaa suruali ya jinzi
huku akiwa kidari wazi. Jamaa akamtupia jicho
fupi, kisha akageukia Imraan Gopang.
“Nilitaka niwashukuru tu kwa kunitoa mle ndani
kwa namna mlivyonitoa…sasa nisingependa
kushukuru watu nisiowajua, pamoja na kuwa ndio
mlioniokoa.” Alimueleza mpakistani yule ambaye
alishajua tangu kule mtaroni kuwa ndiye kiongozi
wa wale jamaa waliomuokoa. Jamaa
walitazamana.
“Okay sio mbaya…” Imraan Gopang alisema, na
kuendelea, “tuchukulie sisi kama matarishi tu
komredi.”
“Matarishi?”
“Yah…kazi yetu kubwa ni kusafirisha vifurushi
kutoka sehemu moja kwenda nyingine…kwa
malipo, of course….”
“Na kwenye swala hili la leo, kifurushi chetu
kilikuwa ni wewe…wajibu wetu ulikuwa
kuhakikisha kuwa tunakutoa kwa watalebani na
kukufikisha kwenye hili boti…ukiwa hai.” Yule
komando aliyemvuta mkono kule mtaroni wakati
wanashambuliwa na watalebani alidakia.
“Oh? Kwa hiyo nyie ni mamluki…mercenaries?”
Jamaa alisaili.
“Matarishi ni sahihi zaidi…” Imraan akasisitiza,
kisha akaendelea, “Hatujui umefanya nini na wala
ni kwa nini umejipatia umuhimu wa kulazimisha
sisi tupewe kazi ya kwenda kukuchoropoa kule
ulipokuwa, kwa namna ya hatari namna ile…na
hatujali. Ndivyo matarishi walivyo. Wao hulipwa
kwa kubeba na kuifikisha bahasha mahala
patakiwapo pasina kujua ndani ya bahasha ile
kuna ujumbe gani…”
Jamaa akaafiki kwa kichwa na kumgeukia yule
mmarekani mweusi.
“Ina maana wewe ndiye uliyeandaa mkakati huu
wa kunitoa mle ndani kwa kuwatumia hawa…
matarishi.” Alimwambia, na bila kusubiri
uthibitisho kutoka kwake akaendelea, “Basi
ahsante sana. Nilijua tu kuwa msingeweza
kuniacha mle ndani…ingawa mmekawia sana.
Hali ilikuwa ngumu sana kule…hasa baada ya
kuuawa kwa yule mwenzangu…sikujua kama
hangenitaja, ilikuwa ni hali tete kwa kweli…”
“Ni kweli. Ilitubidi tubahatishe kufuata ile ile
kanuni mliyowekewa na mwenzako aliyewahiwa
na watalebani…kuwa siku ya kuja kuwachomoa
mle ndani itatangazwa sana maredioni hapa
Pakistani kwa wiki nzima…kuwa idara ya hali ya
hewa inawatahadharisha wananchi wote dhidi ya
kimbunga kikali…kitakachoipiga pwani ya
Pakistani kwenye siku, tarehe na saa maalumu…
tulitaraji tu kuwa utakuwa umesikia tangazo hilo
ukiwa mle ngomeni mwa watalebani, na utajua
kuwa hiyo ndiyo siku na saa ambayo tutakuja
kukuchomoa mle ndani…” Mmarekani alimjibu.
“Ni kweli…na ndipo nilipoanza kujinadi kushikwa
na tumbo la kuhara…nikawa naenda chooni mara
kwa mara, nikikichimba kidogo kidogo kile choo
ambacho tangu awali nilishaelekezwa na
mwenzetu aliyeuawa kuwa ndio ingekuwa njia
yangu ya kutokea mle ndani pindi hali ikifikia
pabaya…”
“Okay, tutaongea zaidi mimi na wewe…kwanza
wacha nimalizane na matarishi wetu hapa…”
Mmarekani alisema.
Kwa dakika kumi na tano zilizofuatia jamaa
alimshuhudia yule mmarekani mweusi
akihamishia pesa kwenye akaunti za wale
mamluki wanne waliokuwa wakiongozwa na
mpakistani Imraan Gopang, kwa kutumia
kompyuta mpakato maalum aliyokuwa nayo mle
botini. Alipomaliza alipeana mikono na wale
jamaa mmoja baada ya mwingine, akimalizia na
Imraan Gopang.
"Ilikuwa ni faraja kufanya tena biashara na wewe,
Imraan." Alimwambia, na kwa mara nyingine
jamaa akaelewa kuwa ile haikuwa mara ya
kwanza kwa wale jamaa kufanya pamoja kazi
kama ile.
"Na mimi vile vile, kamanda! Ukija tena kwenye
nchi yetu hii ya majanga usisite kunipigia...tuk
utane japo kwa kikombe cha kahawa..." Imraan
alimjibu.
"Ha ha ha haaaa...Okay poa, Imraan haina
shida.Ila unue umipokea simu yangu haitakuwa
kwa ajili ya kuoanga miad ya kupata kikombe
cha kahawa kaka...itakuwa ni kwa kazi tu".
Imraan akacheka pamoja naye, na walipomaliza
kucheka, mmarekani mweusi akamwambia, "Basi
sasa nyinyi na sisi tutagawana njia baada ya
kama dakika kumi hivi...helikopta maalum
itawafikisha Karachi...na pale kila mmoja
atatawanyika kivyake...mimi na ninyi hatujaonana
kabisa jamani...na siku hii haipo kabisa katika
historia zenu...sawa?"
"Kama kawaida..." Mmoja wale makomando alini
u wakati Imraan akiafiki kwa kichwa tu swala lile.
"Good. Basi mpaka hapo tutakapohitajiana
tena...kama ikibidi." Mmarekani mweusi alisema.
"Poa."
______________
Dakika kama saba baadaye boti liliegeshwa
kwenye ukingo wa pili wa mto ule, likiwa
limesafiri kiasi cha kama kilometa kumi na tano
kutokea pale ambapo lilipokuwa likiwasubiria
wale makomando. Kutokea mle kwenye boti
zilionekana helikopta mbili zikiwa zimeegeshwa
umbali fulani kando ya mto ule.
“Okay Imraan…nyie mtaingia kwenye ile helikopta
ya kushoto…itawafikisha Islamabad na huko kila
mtu ataangalia ustaarabu wake…sisi tutaingia
kwenye ile ya kulia na kuelekea Karachi …”
Mmarekani mweusi alisema.
Lakini haikuwa hivyo...
***MNH, Leo tumepata jipya...lile kovu baya, vipi
habari yake...? Na kwa nini haikuwa kama
Mmarekani mweusi alivyopanga?
NJOO TUSOME ZAIDI hizi beti za wimbo huu
hapo kesho...
Mar 29 · Public · in Timeline Photos
View Full Size · Send as Message · Report
Zainab Jamal and 328 others like th
[22:07, 4/26/2016] ZAMIRA RIWAYA: RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi
MTUNZI: HUSSEIN TUWA
SEHEMU YA SITA
Nyuma yao, ndege zaidi zilikuwa zikielekea
Dargah Mandi kupelekea mashambulizi zaidi…na
wakati huo huo ndege nyingine mbili zilikuwa
zikipeleka marobota mengine ya vyakula vya
msaada. Safari hii, yale marobota hayakuwa na
komando yoyote aliyejilaza juu yake…
_______________
Wakati boti ikipasua maji kufuata mkondo wa
mto ule, makomando walibadili zile nguo za
kupigia mbizi na kuvaa za kawaida. Wawili kati
yao waliokuwa na asili ya kiasia walivaa "salwan
khameez", nguo maarufu za ki-pakistani, ilhali
yule mwingine aliyejeruhiwa kwa risasi aliyekuwa
wa asili ya afrika, alikuwa akisaidiwa kutolewa
zile nguo kabla ya kupatiwa huduma haraka
haraka na tabibu mmoja waliyemkuta mle botini.
Ile risasi ilimkwaruza tu sehemu ya bega hivyo
haikuwa na madhara makubwa sana kwake. Yule
mmarekani mweusi alimtupia nguo za kipakistani
yule jamaa aliyechoropolewa kutoka kwenye
ngome ya watalebani.
"Vaa hizo nguo!" Alimkoromea.
Jamaa akatii bila kutia neno, ingawa muda wote
akili yake ilikuwa ikimtembea kwa kasi sana.
Aliona wale watu wengine kama watati hivi
waliokuwa pamja na yule mmarekani mweusi mle
botini wakiwa makini sana na bunduki zao, na
mara moja alibaini kuwa umakini wao wote
ulikuwa umeelekezwa kwake yeye, na si kwa
wale wenzake alioibuliwa nao kutoka mle mtoni.
Upande mwingine wa boti ile, mpakistani Imraan
Gopang naye alikuwa akivaa kanzu safi ya kijivu
juu ya suruali nyeupe ya "panjabi", baada ya
kutoa zile nguo za kuzamia mbizi alizokuwa
amevaa. Akiwa makini sana bila ya kujionesha
kuwa yuko kwenye hali ile, jamaa alivua fulana
mchinjo aliyokuwa ameivaa chini ya zile nguo za
kuzamia mbizi...na ndipo wale wenzake aliokuwa
nao mle ndani walipouona mwili wake kuwa
kutumia mwanga wa taa zilizokuwa ndani a lile
boti.
"Eeh...!" Mmoja wa wale makomando wa kiasia
alimaka huku kama wale wenzake na wale
walinzi waliowakuta mle botini, akilikodolea
macho kovu baya kabisa lililotambaa kutokea
upande wa kushoto wa kifua cha yule jamaa,
hadi ubavuni kwake. Lilikuwa ni kovu lenye
michirizi mitatu mizito iliyotokea kwenye vishimo
vitatu vilivyochimbwa pale kifuani na kuacha
makovu yenye vishimo. Yaani ni kama vile kuna
mtu katika siku za nyuma alimshindilia kwa reki
la kukusanyia majani kifuani, na kujaribu
kuzikusanya ngozi yake kutokea pale kifuani hadi
chini kabisa ya ubavu wake wa kushoto. Hakika
lilikuwa ni kovu baya sana.
"Nini?" Jamaa aliuliza huku akiwatembezea
macho wote mle botini, hali akiwa kidari wazi,
ameshikilia shati la kipakistani alilotupiwa na yule
mmarekani mweusi, ambaye ndiye pekee
aliyeonekana kutolishangaa kovu lile.
"Umekutwa na nini hapo komredi? Hilo kovu...."
Imraan Gopang akawasilisha swali ambalo bila
shaka lilikuwa likirindima vichwani mwa wale
wenzake. Jamaa aliinama na kujitazama pale
penye kovu, kisha akawatazama wale wenzake
kwa uso uliosajili hali ya kutokuwa na jibu kwa
swali aliloulizwa.
"Nyie ni wapiganaji halafu mnaogopa makovu?"
Aliwauliza badala ya kuwajibu, huku akilivaa lile
shati refu la kipakistani, na kulificha kovu lake.
Jamaa walichanganyikiwa kiasi kwa jibu lile.
"Ah...mimi nimepitia makabiliano ya kila namna
komredi...lakini sisi ni watu tunaocheza kwa
bunduki, risasi na mabomu kaka...hilo ulilo nalo?
Si kovu litokanalo na chochote kati ya hivyo
aisee..." Imraan Gopang alimjibu.
Kwa mara ya kwanza jamaa akaachia tabasamu,
na alivyofanya vile, sura yake ngumu ikabadilika
na kuwa ya kuvutia kwa namna fulani ya ugumu.
"Basi bado hujapitia makabiliano ya kila aina
komredi..." Alimjibu bila kujali.
"Okay...imetosha jamani..." Yule mmarekani
mweusi alidakia, akaendelea, "Tumalize hii
biashara Imraan..."
"Nyie ni kina nani kwani....?" Jamaa akauliza
lililokuwa likimtatiza kichwani mwake tangu
aporomoke kutoka kwenye dari la ule mtaro wa
majitaka.
“Hutaki kujibu maswali yetu, unataka tukujibu ya
kwako?” Komando mwenye asili ya kiafrika
alimuuliza, sasa akiwa amefungwa bandeji
kitaalamu begani. Alikuwa amevaa suruali ya jinzi
huku akiwa kidari wazi. Jamaa akamtupia jicho
fupi, kisha akageukia Imraan Gopang.
“Nilitaka niwashukuru tu kwa kunitoa mle ndani
kwa namna mlivyonitoa…sasa nisingependa
kushukuru watu nisiowajua, pamoja na kuwa ndio
mlioniokoa.” Alimueleza mpakistani yule ambaye
alishajua tangu kule mtaroni kuwa ndiye kiongozi
wa wale jamaa waliomuokoa. Jamaa
walitazamana.
“Okay sio mbaya…” Imraan Gopang alisema, na
kuendelea, “tuchukulie sisi kama matarishi tu
komredi.”
“Matarishi?”
“Yah…kazi yetu kubwa ni kusafirisha vifurushi
kutoka sehemu moja kwenda nyingine…kwa
malipo, of course….”
“Na kwenye swala hili la leo, kifurushi chetu
kilikuwa ni wewe…wajibu wetu ulikuwa
kuhakikisha kuwa tunakutoa kwa watalebani na
kukufikisha kwenye hili boti…ukiwa hai.” Yule
komando aliyemvuta mkono kule mtaroni wakati
wanashambuliwa na watalebani alidakia.
“Oh? Kwa hiyo nyie ni mamluki…mercenaries?”
Jamaa alisaili.
“Matarishi ni sahihi zaidi…” Imraan akasisitiza,
kisha akaendelea, “Hatujui umefanya nini na wala
ni kwa nini umejipatia umuhimu wa kulazimisha
sisi tupewe kazi ya kwenda kukuchoropoa kule
ulipokuwa, kwa namna ya hatari namna ile…na
hatujali. Ndivyo matarishi walivyo. Wao hulipwa
kwa kubeba na kuifikisha bahasha mahala
patakiwapo pasina kujua ndani ya bahasha ile
kuna ujumbe gani…”
Jamaa akaafiki kwa kichwa na kumgeukia yule
mmarekani mweusi.
“Ina maana wewe ndiye uliyeandaa mkakati huu
wa kunitoa mle ndani kwa kuwatumia hawa…
matarishi.” Alimwambia, na bila kusubiri
uthibitisho kutoka kwake akaendelea, “Basi
ahsante sana. Nilijua tu kuwa msingeweza
kuniacha mle ndani…ingawa mmekawia sana.
Hali ilikuwa ngumu sana kule…hasa baada ya
kuuawa kwa yule mwenzangu…sikujua kama
hangenitaja, ilikuwa ni hali tete kwa kweli…”
“Ni kweli. Ilitubidi tubahatishe kufuata ile ile
kanuni mliyowekewa na mwenzako aliyewahiwa
na watalebani…kuwa siku ya kuja kuwachomoa
mle ndani itatangazwa sana maredioni hapa
Pakistani kwa wiki nzima…kuwa idara ya hali ya
hewa inawatahadharisha wananchi wote dhidi ya
kimbunga kikali…kitakachoipiga pwani ya
Pakistani kwenye siku, tarehe na saa maalumu…
tulitaraji tu kuwa utakuwa umesikia tangazo hilo
ukiwa mle ngomeni mwa watalebani, na utajua
kuwa hiyo ndiyo siku na saa ambayo tutakuja
kukuchomoa mle ndani…” Mmarekani alimjibu.
“Ni kweli…na ndipo nilipoanza kujinadi kushikwa
na tumbo la kuhara…nikawa naenda chooni mara
kwa mara, nikikichimba kidogo kidogo kile choo
ambacho tangu awali nilishaelekezwa na
mwenzetu aliyeuawa kuwa ndio ingekuwa njia
yangu ya kutokea mle ndani pindi hali ikifikia
pabaya…”
“Okay, tutaongea zaidi mimi na wewe…kwanza
wacha nimalizane na matarishi wetu hapa…”
Mmarekani alisema.
Kwa dakika kumi na tano zilizofuatia jamaa
alimshuhudia yule mmarekani mweusi
akihamishia pesa kwenye akaunti za wale
mamluki wanne waliokuwa wakiongozwa na
mpakistani Imraan Gopang, kwa kutumia
kompyuta mpakato maalum aliyokuwa nayo mle
botini. Alipomaliza alipeana mikono na wale
jamaa mmoja baada ya mwingine, akimalizia na
Imraan Gopang.
"Ilikuwa ni faraja kufanya tena biashara na wewe,
Imraan." Alimwambia, na kwa mara nyingine
jamaa akaelewa kuwa ile haikuwa mara ya
kwanza kwa wale jamaa kufanya pamoja kazi
kama ile.
"Na mimi vile vile, kamanda! Ukija tena kwenye
nchi yetu hii ya majanga usisite kunipigia...tuk
utane japo kwa kikombe cha kahawa..." Imraan
alimjibu.
"Ha ha ha haaaa...Okay poa, Imraan haina
shida.Ila unue umipokea simu yangu haitakuwa
kwa ajili ya kuoanga miad ya kupata kikombe
cha kahawa kaka...itakuwa ni kwa kazi tu".
Imraan akacheka pamoja naye, na walipomaliza
kucheka, mmarekani mweusi akamwambia, "Basi
sasa nyinyi na sisi tutagawana njia baada ya
kama dakika kumi hivi...helikopta maalum
itawafikisha Karachi...na pale kila mmoja
atatawanyika kivyake...mimi na ninyi hatujaonana
kabisa jamani...na siku hii haipo kabisa katika
historia zenu...sawa?"
"Kama kawaida..." Mmoja wale makomando alini
u wakati Imraan akiafiki kwa kichwa tu swala lile.
"Good. Basi mpaka hapo tutakapohitajiana
tena...kama ikibidi." Mmarekani mweusi alisema.
"Poa."
______________
Dakika kama saba baadaye boti liliegeshwa
kwenye ukingo wa pili wa mto ule, likiwa
limesafiri kiasi cha kama kilometa kumi na tano
kutokea pale ambapo lilipokuwa likiwasubiria
wale makomando. Kutokea mle kwenye boti
zilionekana helikopta mbili zikiwa zimeegeshwa
umbali fulani kando ya mto ule.
“Okay Imraan…nyie mtaingia kwenye ile helikopta
ya kushoto…itawafikisha Islamabad na huko kila
mtu ataangalia ustaarabu wake…sisi tutaingia
kwenye ile ya kulia na kuelekea Karachi …”
Mmarekani mweusi alisema.
Lakini haikuwa hivyo...
***MNH, Leo tumepata jipya...lile kovu baya, vipi
habari yake...? Na kwa nini haikuwa kama
Mmarekani mweusi alivyopanga?
NJOO TUSOME ZAIDI hizi beti za wimbo huu
hapo kesho...
Mar 29 · Public · in Timeline Photos
View Full Size · Send as Message · Report
Zainab Jamal and 328 others like th
[22:14, 4/26/2016] ZAMIRA RIWAYA: Next
KONA YA Riwaya Reloaded
RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi
MTUNZI: Hussein Tuwa
SEHEMU YA NANE
“Sio kazi bure komredi…akaunti zetu zimenona…
tuombe tunusurike tu hapa…” Imraan alimjibu.
“Kweli kaka…”
Safari yao iliendelea bila ya tukio lolote…
________________
Saa moja baadaye helikopta ilitua pembezoni
mwa jiji la Islamabad, na mara baada ya Imraan
na kundi lake kuteremka,rubani aliirusha tena ile
helikopta na kutokomea angani.
Imraan aliwaongoza wenzake kimya kimya,
wakikata mitaa kadhaa kabla ya kutokea kwenye
kituo cha teksi. Walionekana kama wenyeji
watatu tu waliokuwa na mgeni wao mmoja wa
kiafrika wakitoka kwenye moja ya sehemu
kadhaa za starehe, ambazo kwa mazingira ya
nchi ile zilikuwa ni za siri sana.
"Okay makomredi...mimi naelekea kwangu sasa.
Ninyi mtarudi kwenye mahoteli yenu na
kukipambazuka mtoweke nchi hii...si tiketi na
pasipoti zenu viko sawa?" Imraan aliwaambia na
kuwauliza wenzake.
"Yah...tuko vizuri..."Mmoja alijibu.
"Okay..tutawanyike. Ikiwa kutatokea kazi
nyingine ninajua nitawasiliana vipi na nyie..."
"Kuna kazi tena na dalali wako wa madili
keshadunguliwa kule?" Mwenzake mmoja
alimuuliza.
Imraan akafyatua kicheko kifupi, kisha akamjibu,
"Kufa ndio sehemu kuu ya kazi yetu kaka…ndio
maana hata kama mmoja wetu angeuawa leo hii,
bado hela yake ingetumwa tu kwenye akaunti
yake, familia yake ikanufaika. Kafa yeye...sio
harakati, bwana. Atawekwa mwingine wa
kusimamia mambo haya badala yake...na
atanitafuta tu muda ukifika..." Alimjibu.
Kila mmoja akachukua teksi yake na kuelekea
kwenye hoteli aliyofikia. Imraan alimuelekeza
dereva wa teksi yake amrejeshe nyumbani
kwake...ambako alipaacha kwa siku kadhaa
alipokuwa ameenda kwenye misheni ile ya hatari.
________________
CNN ndio walikwa wa mwanzo kutangaza juu ya
shambulizi lile kubwa kabisa la ndege zisizo na
rubani dhidi ya ngome kuu ya wataleban
iliyokuwa kilomita saba kutoka kwenye kile kijiji
cha Dargah Mandi.
Kupitia taarifa ile, dunia ilihabarishwa kuwa
kiongozi mkuu wa wataleban ndani ya Waziristan
alikuwa ameuawa pamoja na wafuasi wake
wengi wakiwemo wale wa Al-Qaida waliokuwa
wamehifadhiwa kwenye ngome ile.
Aidha, CNN ilihabarisha kuwa katika kampeni ile
ya mashambulizi iliyofanywa kwa ushirikiano kati
ya jeshi la marekani na lile la Pakistani, jeshi la
shirikisho lilifanikiwa kumtia mbaroni gaidi
muhimu aliyehusika katika ulipuaji mabomu
ubalozi wa Marekani nchini Tanzania mwaka 98,
aliyekuwa akisakwa sana, Nouman bin
Fattawi...lakini helikopta aliyokuwa akisafirishwa
nayo kutoka Pakistani ilidunguliwa na vikosi vya
wapiganaji wasiojulikana na yeye pamoja na watu
wengine saba waliuawa. Mpaka muda habari ile
inarushwa hewani, hakukuwa na kundi lolote
lilojinadi kuhusika na udunguliwaji wa helikopta
ile. Habari hii ilidakwa na vyombo vingine vya
habari na kusambaa dunia nzima.
Ni habari iliyoleta kizaazaa kikubwa nchini
Tanzania...
___________________
Makaburi ya Kisutu, Dar es Salaam, Tanzania.
Wiki moja baadaye:
Umma wa watu ulikuwa umefurika kwenye
makaburi ya kisutu. Muda ulikuwa ni saa kumi za
alasiri. Ufurikaji wa umma makaburini pale
haukutokana na kwamba kulikuwa kuna mtu
maarufu aliyekuwa akizikwa siku ile, La Hasha.
Mfuriko ule ulitokana na ukweli kwamba kulikuwa
kuna marehemua watano waliokuwa wakizikwa
siku na wakati ule, na hivyo kulikuwa kuna
makundi matano ya ukubwa tofauti kwenye
makaburi matano yaliyochimbwa sehemu tofauti
ndani ya uzio wa eneo lile la makaburi maarufu
jijini.
Ni kutokana na ujumla wa makundi yale matano
yenye ukubwa tofauti kuwa ndani ya eneo lile
kwa wakati mmoja, ndipo taswira ya umma wa
watu kufurika ilipopatikana makaburini pale.
Nje ya uzio wa makaburi yale magari mengi
yalikuwa yameegeshwa pande zote za barabara
finyu, kiasi kwamba ilikuwa ni shida kwa magari
mengine kupita tu pale barabarani, wachilia mbali
kupishana.
Kwenye kaburi lililochimbwa pembeni kabisa ya
eneo lile la makaburi, upande wa kushoto mara
baada ya kuingia kwenye geti la makaburi yale,
kulikuwa kuna kundi la wastani la wanandugu
waliokuwa wakimzika mpendwa wao,
wakiongozwa na sheikh aliyekuwa mjuzi katika
taratibu za kuendesha maziko. Lilikuwa ni kundi
lenye huzuni kwa kuondokewa na ndugu na
jamaa yao ambaye hata hivyo wamekuwa mbali
naye kwa muda mrefu, siku zote hizo kabla ya
umauti kumkuta mpendwa wao, wakiwa
wamegubikwa mashaka mazito juu ya hatma
yake…mpaka habari zilipowafika kuwa hatimaye
mpendwa wao alikuwa ameuawa kwenye kifo
kibaya kabisa, huko ughaibuni.
Walikuwa wamekusanyika kumzika Nouman
Fattawi.
Kaka, mwana, mjomba, rafiki, mpenzi…na kwa
wengine, ndugu yao katika imani.
Hata hivyo, hawa wote walikuwa ni sehemu moja
tu ya wale waliokuwapo kwenye mazishi ya
Nouman Fattawi siku ile.
Pamoja nao walikuwepo wana usalama wa taifa,
ambao walikuwa pale kushuhudia maziko ya gaidi
aliyekuwa akisakwa na wamarekani kwa udi na
uvumba, akihusishwa na ulipuaji wa ubalozi wa
marekani jijini Dar miaka kumi na minane
iliyopita… na pia kuwatazama kwa makini wote
waliokuwa wamefika kwenye mazishi ya mtu yule
hatari sana kuwahi kutokea kwenye historia ya
Tanzania tangu vita dhidi ya kile kilichokuja
kunadiwa na kutambulika kama “ugaidi” inadiwe
duniani. Na ni kutokana na kulijua au kulitarajia
hilo ndio maana hata kundi lililokuwa kwenye
maziko ya Nouman Fattawi jioni ile pale kisutu
ndilo lilikuwa dogo kuliko yale mengine manne
yaliyokuwa pale makaburini siku ile.
Ni nani anayetaka kuhusishwa na gaidi?
Hakuna…isipokuwa kama ni ndugu wa damu au
wa karibu sana…au ambaye yuko bega kwa bega
na harakati za marehemu kiasi kwamba hajali
iwapo na yeye atahusishwa na harakati hizo.
Na ni hawa wa mwisho ndio ambao
wanausalama waliojipenyeza kwenye maziko
yale, wakiwa wamejivika kanzu na vibaraghashia
ili kufanana na waombolezaji halisi wa tukio lile,
ndio waliokuwa wakijaribu kuwabaini kwenye
mkusanyiko ule. Walitaraji kupata cha
kuwaongoza kwenye azma yao ile kutoka kwenye
mawaidha ya mwisho yatakayotolewa na yule
shekhe atakapomaliza kuongoza maziko yale.
Lakini pia walikuwepo watendaji wa shirika la
ujasusi la marekani, C.I.A., ambao nao walikuwa
ni weusi kama wengine pale kaburini, wakiwa
wamejivika mavazi muafaka kwa tukio lile, na
ambao pia walijua namna ya kuitikia dua
zilizokuwa zikielekezwa na shekhe mazikoni pale.
Lengo lao lilikuwa ni kujithibitishia kuwa kweli
gaidi waliyekuwa wamemtamani kwa miaka
mingi, hakika alikuwa amezamishwa ndani ya
tumbo la ardhi jijini Dar…ili watakapopeleka ripoti
huko kwenye makao yao makuu kule Langley,
Virginia, wawe na ushahidi wa dhahiri kabisa kwa
kile walichokishuhudia. Lakini vilevile, uwepo wao
pale ulikuwa na lengo la kujaribu kuona iwapo
kutakuwa kuna atakayepandwa na jazba pale
makaburini na kubwabwaja kulipiza kisasi kwa
wamarekani kwa kifo cha yule mshirika wao…au
kuona yeyote ambaye angeelekea kuwa alikuwa
akishirikiana na marehemu kwa namna moja au
nyingine.
_________________
Maziko yaliendelea kama ilivyotakiwa. Kutokana
na namna mwili wa marehemu ulivyoharibika,
ulizikwa kwa shida sana, kilichozikwa kikiwa ni
mabaki yaliyopatikana ya mwili wake. Baada ya
mwili kuingizwa kaburini na kuzikwa, shekhe
alitoa mawaidha kwa wafiwa kuwa wawe
wastahamilivu, na kuwa Nouman Fattawi alikuwa
ameshakunywa kifo chake kutoka kwenye gilasi
ya umauti, ambayo sote hapa duniani
tumeahidiwa kunyweshwa baada ya muda
fulani…hivyo wote waliobakia pamoja na yeye
mwenyewe walikuwa wana gilasi zao
zinazowasubiri.
“Siku gani…saa ngapi…mahala gani na sisi
tutaletewa gilasi zetu za umauti haijulikani.
Mwenzetu kapelekewa gilasi yake Pakistani,
lakini huenda kuna miongoni mwetu ambaye ya
kwake inamsubiri hapo morogoro road akiwa
njiani kutoka hapa mazikoni…basi na tushike
ibada ndugu zangu, tumrejee mola wetu na
tuchukulie kifo cha ndugu yetu, mpendwa wetu,
mwana imani mwenzetu, raia mwezetu huyu…
kuwa ni ukumbusho kwetu sisi tuliobaki…”
Shekhe alimalizia. Akapiga “Fat-ha”, kisha
akaomba dua ndefu kwa lugha ya kiarabu. Watu
wakaitikia dua. Alipomaliza akaruhusu watu
kutawanyika kwa maelezo kuwa wanafamilia
wamesema kuwa hakutakuwa na matanga
nyumbani kwao. Hakuongelea hata neno moja
kuhusu ugaidi wa Nouman Fattawi wala namna
alivyokufa.
Maziko yakaisha.
Watu wakatawanyika.
Wanausalama wa taifa na wenzao wa C.I.A.
wakaambulia kunufaika na mawaidha tu ya
shekhe kwenye maziko yale.
Kutokea chini ya mti uliokuwa hatua kadhaa
kutoka kwenye kaburi la jirani ambako napo
maziko mengine yalikuwa yakiendelea, mtu
mmoja mrefu aliyevaa suruali nyeupe ya
kitambaa chepesi, viatu vyeusi vya ngozi bila ya
soksi na shati jeupe la mikono mirefu ambalo
hakulichomekea, wala hakuwa amelifunga
vifungo kiasi cha kuionesha fulana nyepesi
nyeusi aliyoivaa chini ya shati lile, alikuwa
akifuatilia kwa makini sana kile kilichokuwa
kikiendelea sio pale kwenye yale maziko
aliyokuwa amesimama karibu nayo, bali kule
kwenye maziko ya gaidi Nouman Fattawi.
Usoni alikuwa amevaa miwani ya jua iliyoficha
macho yake, na kichwani alikuwa amevaa
barghashia moja ghali sana. Kwa pale alipokuwa
amesimama kando ya mti, uso wake ulikuwa
umeelekea pale kwenye yale yaliyokuwa
yakiendelea kwenye maziko yaliyokuwa jirani na
ule mti aliokuwa amesimama chini yake,
miongoni mwa wazikaji wengine, lakini macho
yake yaliyokuwa nyuma ya miwani ile myeusi, na
masikio yake vilikuwa kule kwenye kilichokuwa
kikifanyika kwenye kaburi la Nouman Fattawi.
Na sasa alibaki pale pale chini ya mti wakati
akiwatazama watu waliokwenda kumzika
Nouman wakitawanyika, ilhali wale waliokuwa
wakimzika marehemu wa kwenye kaburi
alilokuwa amesimama kando yake, wakimalizia
kumfukia yule marehemu wao pale kaburini.
Alibaki akiwa amesimama pale pale chini ya mti
hata pale wale watu waliokuwa wakimzika yule
marehemu mwingine walipomaliza na
kutawanyika…
****Doh, katoka Nouman, kaja mzee wa chini ya
mti...nini hii sasa?
NJOO TUSOME zaidi khabari hizi hapo kesho,
muda kama wa leo.
[22:33, 4/26/2016] ZAMIRA RIWAYA: ONA YA Riwaya Reloaded
RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi
MTUNZI: Hussein Tuwa
SEHEMU YA TISA
Alibaki akiwa amesimama pale pale chini ya mti
hata pale wale watu waliokuwa wakimzika yule
marehemu mwingine walipomaliza na
kutawanyika…
__________________________
Kiasi cha kama saa moja na nusu baada ya watu
wote kutawanyika pale makaburini, kaburi la
marehemu Nouman Fattawi likapata mgeni. Jua
lilikuwa limeshazama na mwanga ulikuwa
unatowekea kutoka kwenye hafifu kwenda
kwenye kiza, na umbile la mtu likafika pale
kaburini kama mzuka tu na kusimama wima
upande ambapo miguu ya marehemu aliyelala
chini ya tuta lile la udongo ingekuwapo.
Kutokea pale chini ya mti alipokuwa
amechutama baada ya kuwa ameshasimama kwa
zaidi ya saa tatu, tangu wakati mwili wa Fattawi
unaletwa, unazikwa na kuachwa peke yake pale
chini ya udongo, mtu mrefu aliyekuwa amevaa
nguo nyeupe alimakinika vilivyo, huku akijibanza
zaidi nyuma ya mti ule. Alijifuta machozi
yaliyokuwa yakimtiririka na kukaza macho
kukitazama kile kiumbe kilichokuwa kimesimama
pale mbele ya kaburi la hayati Nouman.
Kutokea pale nyuma ya mti, jamaa alibaini vitu
viwili. Kwanza yule mtu alikuwa ana umbo dogo…
halafu, kutokana na mavazi yake, alikuwa ni wa
jinsia ya kike.
Umakini wake ukapanda daraja.
Yule mwanamke alikuwa amevaa vazi la dera
lenye rangi iliyojificha, aidha buluu au kahawia…
au nyeusi… hakuweza kujua kwa urahisi kutokea
pale alipokuwa. Alikuwa amesimama wima hali
mikono yake akiwa ameishika pamoja kwa mbele,
chini kidogo ya kitovu chake, na kichwa chake
akiwa amekiinamisha kwa mbele kama
anayeomba dua fulani kwa marehemu yule.
Jamaa alizidi kumfuatilia huku kwa wakati huo
huo akitembeza macho huku na huko ili kuona
iwapo yule mwanamama alikuwa amekuja na
watu wengine pale makaburini muda ule.
Hakuona mtu mwingine yeyote.
Kisha, ghafla kama alivyoibuka, yule mwanamke
aligeuka na kuondoka pale kaburini kwa mwendo
wa haraka.
Jamaa akajichomoa nyuma ya mti na kuanza
kumfuata kwa mwendo wa tahadhari. Nje ya uzio
wa makaburi yale mwanadada alikunja kulia na
kutembea kwa mwendo mfupi kabla hajalifikia
gari dogo ambalo jamaa hakuweza kulitambua
mara moja lilikuwa ni la muundo gani, na dakika
moja baadaye lile gari likaondoka eneo lile kwa
mwendo mdogo.
Bila kujishauri zaidi, jamaa akafungua mnyororo
uliokuwa umeifunga pikipiki yake aina ya boxer
aliyokuwa ameipaki pale nje, na kuiingiza
barabarani, akilifuata lile gari.
Baada ya kulifuata lile gari kwa muda, likikata
mitaa kadhaa wa kadhaa ya jiji, hatimaye lile gari
ambalo sasa alibaini kuwa lilikuwa ni Toyota
Duet, liliashiria kukata kona kuingia kwenye jengo
la hoteli moja nzuri sana ya ghorofa tano
iliyokuwa maeneo ya sinza. Jamaa alipitiliza na
pikipiki yake hadi kwenye maegesho yaliyokuwa
nje ya hoteli ile, akamkabidhi mlinzi wa kimasai
pale kwenye maegesho yale, na kuelekea kwenye
lango kuu la hoteli ile, akiliona lile gari la yule
dada bado likiwa pale nje ya geti la hoteli ile
likisubiri geti lifunguliwe ili liingie.
Jamaa akapitiliza hadi sehemu ya mapokezi ya
hoteli ile na kukuta watu kadhaa wakijiandikisha
pale. Akaketi kwenye moja ya makochi ya pale
mapokezi akiwa makini sana.
Dakika chache baadaye alimuona yule
mwanamke mwenye umbo dogo akiingia mle
hotelini na kupita moja kwa hadi kaunta ya
mapokezi.
“Naomba ufunguo wangu dada…namba mia tatu
na saba…” Dada alipaaza sauti kumwambia binti
wa mapokezi. Binti alimkabidhi ule ufunguo na
mwanadada akaongoza kwenye lifti
iliyompandisha huko juu.
Jamaa akakunja uso. Hakuwa amepata kumuona
yule dada hata siku moja hapo kabla, na wala ile
sauti yake haikumletea kumbukumbu yoyote.
Lakini jambo moja lilimfunukia wazi wazi akilini
mwake, na ndilo lililomfanya akinje uso.
Yule mwanamke aliitaja namba ya chumba chake
kwa sauti makusudi…kwa faida yake yeye…ili
yeye ajue kuwa yule dada yuko kwenye chumba
namba mia tatu na saba.
Kwa nini?
Ina maana yule dada alijua kuwa yeye
angekuwepo pale makaburini muda ule? Na alijua
kuwa alikuwa akimfuata kwa pikipiki muda wote?
Kama ndivyo…ni kwa nini basi?
Kwanza anahusika vipi na Nouman Fattawi yule
dada?
Akili ilimuwamba mtu mwenye nguo nyeupe, au
mzee wa chini ya mti.
Hatua gani ifuate sasa?
Jamaa alijiuliza akiwa ametulia kwenye kochi la
pale mapokezi. Jibu lilijileta kwake dakika tano
baadaye.
___________
Sehemu nyingine ya jiji, mzee Fattawi, baba wa
hayati Nouman alikuwa kwenye wakati mgumu
sana. Vijana waliombeba kwa gari lao wakati
wakitokea makaburini akiamini kwa ni miongoni
mwa waombolezaji kwenye msiba ule wa
mwanaye aliyemkosa kwa miaka mingi, walikuwa
wakimuongelesha maneno ambayo hakuwa
akiyaelewa.
“Mzee…tunajua kuwa uko kwenye msiba mzito…
sisi pia tuna masikitiko na kifo hiki. Letu kwako ni
moja tu…elewa kuwa mwanao amekufa kishujaa,
hivyo asitokee mtu yeyote akaja kukuletea habari
za kuwa eti alikuwa gaidi…yeye amekufa kwenye
njia iliyo sahihi. Na tuko wengine pamoja naye
kwenye njia hiyo hiyo aliyoenda yeye…” Mmoja
wao alimwambia. Mzee akapagawa.
“Wanangu…mbona siwaelewi? Mimi Nouman
nilishamzika miaka zaidi ya kumi iliyopita!
Nilimzika moyoni mwangu. Sikuwahi kuonana
naye tangu nimeanza kusikia hizo habari za eti
naye ni gaidi. Nilishahojiwa na watu wa kila aina
mimi…na wote jibu langu limekuwa ni hili hili…
sitambui swala la mwanangu kuwa gaidi na
siamini…sio Nouman…sasa mmeshamuua,
haitoshi kuwafanya muiache nafsi yake ipumzike
jamani? Hebu nishusheni hapa! Nishusheni
haraka tena!” Mzee alifoka.
Bila kuongea zaidi, jamaa walipaki gari kando ya
barabara na kumteremshia njiani, nao wakatia
moto gari lao na kutoweka.
Mzee wa watu akabaki akilia kwa uchungu peke
yake barabarani…
_______________
Akiwa pale mapokezi, jamaa aliona watu wawili
wenye asili ya kiajemi wakiingia mle hotelini huku
wakiangaza macho huku na huko, wakiwa na
mabegi yao ya safari. Muonekano wa watu wale
mara moja ulimjuza kuwa hawakuwa wenyeji,
lakini pia hawakuwa wema. Hakusubiri zaidi.
Aliinuka na kuziendea ngazi za miguu na
kuzikwea haraka hadi ghorofa ya tatu. Huko
akaanza kukisaka chumba namba mia tatu na
saba. Alipokifikia alisimama nje ya mlango wa
chumba kile na kutazama huku na huko, akaona
korido ilikuwa tupu. Akajaribu kusikiliza iwapo
kulikuwa kuna mienendo yoyote nyuma ya
mlango wa chumba kile. Kulikuwa kimya kabisa.
Akajaribu kushika kitasa cha mlango ule, na
ajabu mlango ukajisukuma ndani kirahisi kabisa.
Kengele za hatari zikaanza kugonga kichwani
mwake. Akili ikamwambia ageuze pale pale,
aondoke. Lakini udadisi ukamwambia vinginevyo.
Akausukuma zaidi ule mlango na kujidhihirishia
chumba kilichokuwa kimegubikwa na kiza.
Haraka akaingia ndani na kuusukuma taratibu ule
mlango nyuma yake na kuufunga. Alianza
kutafuta kitasa cha kuwashia taa kando ya
mlango ule wakati ghafla taa ya mezani
ulipowaka moja kwa moja mbele yake. Alihemka
huku akijisogeza pembeni kwa hamaniko,
akitafuta pa kujificha.
“Tulia hivyo hivyo…!” Sauti nzito ilimkoromea, na
hapo hapo ndipo alipomuona mtu mmoja
aliyekuwa ameketi kwenye kochi lililokuwa
upande wa pili wa chumba kile. Kutokea pale
alipokuwa, aliweza kuona miguu tu iliyokuwa
imekunjwa nne, na juu ya goti la mmoja kati ya
miguu ile kulikuwa kuna mkono ulioshika bastola
kubwa, ambayo ilikuwa imemuelekea yeye.
Duh!
Ule mwanga wa ile taa ulikuwa ukimmulika usoni,
na hivyo hakuweza kumuona vizuri yule mtu
mwenye bastola. Aligwaya kidogo.
“Weka mikono yako sehemu ambayo nitaiona
kwa urahisi, na usifanye utundu wowote hapo!”
Sauti ilimkoromea tena, na jamaa akahisi moyo
ukimlipuka.
Ile sauti!
Alishapata kuisikia kabla…
Akasikia mchakacho hafifu jirani na pale
alipokuwa amesimama, na ghafla, kabla hajaweza
kugeuka vizuri kutazama kule ambako
mchakacho ule ulitokea, akapigwa kwa nguvu na
kitu kizito kichwani.
Mguno hafifu ukamtoka, naye akaenda chini bila
kupenda…kiza kikatanda mbele ya uso wake…
***DOH!
Apr 1 · Public · in Timeline Photo
[22:37, 4/26/2016] ZAMIRA RIWAYA: Wimbo Wa Gaidi
MTUNZI: Hussein Tuwa
SEHEMU YA KUMI
Akasikia mchakacho hafifu jirani na pale
alipokuwa amesimama, na ghafla, kabla hajaweza
kugeuka vizuri kutazama kule ambako
mchakacho ule ulitokea, akapigwa kwa nguvu na
kitu kizito kichwani.
Mguno hafifu ukamtoka, naye akaenda chini bila
kupenda…kiza kikatanda mbele ya uso wake…
No way!
Kwa namna isiyotarajiwa alijiachia kwenda chini
na hapo hapo akalikwapua kwa nguvu sana zulia
refu na jembamba lililokuwa limetandikwa pale
juu ya sakafu ya marumaru ya chumba kile,
likitambaa kutokea pale mlangoni hadi pale
kwenye kiti alichokalia yule mtu mwenye bastola,
na kubingirika nalo sakafuni.
Kile kiti kilichokuwa juu ya lile zulia kilipinduka
pamoja na yule jamaa aliyekuwa amekikalia,
ambaye aliachia mgutuko wa kutotarajia huku
akienda chini na bastola yake. Jamaa
hakuhangaika naye bali alijizungusha zaidi pale
chini akiunyooshea mguu wake kule alipohisi
kuwa pigo la kichwa lilipotokea, lakini akaambulia
patupu, kwani mtu aliyempiga lile pigo aliwahi
kuruka juu na ngwara yake ikapita patupu.
Pale pale chini akajigaragaza kufuata kule miguu
ya mtu mwenye bastola ilipokuwa na kumkumba
vibaya yule jamaa. Wote wawili wakajibabatiza
kwenye kiti alichokuwa amekalia yule jamaa
hapo awali.
Jamaa akawahi kujiinua lakini akakutana na teke
zito la ubavu kutokea nyuma yake. Akagumia
huku kwa pembe ya jicho lake akimuona yule
mtu mwenye bastola akiinuka ilhali bado ile
bastola yake ikiwa mkononi mwake. Jamaa
akachanganya miguu huku akijirusha nyuma kana
kwamba alikuwa akicheza dansi isiyojulikana,
kisha kwa namna ya ajabu mguu wale
ukafyatuka kama kofi kali la mkono na
kuipangusa vibaya ile bastola kutoka mkononi
mwa yule jamaa.
Heh!
Hapo mshirika wa yule mtu mwenye bastola
alimrushi teke jingine kali sana, na kwa mara
nyingine mzee wa chini ya mti alijigeuza kwa
wepesi wa ajabu mithili ya mtu aliyekuwa
akicheza dansi, na pigo la yule mwanadada
mwenye umbo dogo likapotea, naye akayumba
kibwege na kujikuta akiwa amedhibitiwa kwa
namna ambayo wala hakuielewa.
“Basi inatosha nyinyi…ebbo!” Jamaa alibwata, na
yule mtu aliyekuwa ameshika bastola hapo awali
alibaki akiwa amepiga mduwao usiosemeka pale
alipomshuhudia yule jamaa akiwa amemkaba
kabali kali sana yule mwanadada huku akiwa
amemuwekea kisu kooni.
E bwana we!
Walitazamana.
“Tulia mzee…huhitaji kabisa kuanzisha mambo
haya na mimi nakwambia…nielezeni ni nini
kinaendelea hapa?” Mzee wa chini ya mti alisaili
huku akiwa amemkazia macho makali sana yule
bwana aliyekuwa na bastola hapo awali.
Jamaa alikuwa akimtazama kwa makini na
kutoamini.
“Oh…okaayy…tulia basi…tulikuwa tunataka
kuongea tu…!” Yule bwana alisema kwa mashaka
huku akiwa ametawanya mikono yake kuonesha
kuwa hakuwa na silaha yoyote mikononi mwake
muda ule.
“Hivi ndivyo mnavyoongea na watu?” Mzee wa
chini ya mti akasaili.
“Sasa unaniachia au huniachii wewe?” Yule dada
naye alikoroma kwa hasira. Jamaa alimpapasa
mwilini haraka kwa ule ule mkono wake ulioshika
kisu huku bado akiwa amemkaba.
“Toa hiyo bastola uloificha pajani…taratbu sana,
kisha tuongee!” Jamaa alimkoromea yule dada.
“Dah!” Dada alinywea na kutekeleza kwa
kupitisha mkono ndani ya ile nguo iliyoonekana
kuwa kama dera, lakini kumbe ikiwa ni suruali
iliyoshonwa kwa mtimbo wa bwanga pana
aliyoivaa chini ya blauzi ya kitambaa kile kile cha
ile suruali, ambayo ilishonwa kwa mtindo wa
namna madera yanavyoshonwa, ila yenyewe
ikiishia sehemu baina ya kiuno chake na magoti
yake.
Akaitupia sakafuni ile bastola.
Jamaa akamsukuma mbele kwa nguvu
kumuendea yule bwana na wale washirika wawili
wakapamiana vibaya. Walipojiweka sawa, jamaa
alikuwa ameketi kitandani mle ndani huku akiwa
amewanyooshea ile ile bastola iliyokuwa kwenye
uvungu wa paja la yule mwanadada, ilhali kile
kisu alichokuwa nacho hapo awali hakikuwepo
tena mkononi mwake.
Loh!
Walikodoleana macho.
“Anzeni maongezi!” Jamaa alisema kwa ukali.
________________
“Ulikuwa unatafuta nini pale makaburini wewe?”
Bwana aliyekuwa na bastola hapo awali
alimuuliza.
“Hatuendi hivyo…utambulisho kwanza…sauti yako
naijua, lakini sura yako hainiletei kumbukumbu
yoyote…ni nani wewe?” Jamaa alisaili.
Swali lake lilionekana kumzidishia udadisi
mkubwa yule bwana, aliyepata umri wa kama
miaka hamsini au hamsini na miwili hivi.
“Hunikumbuki?”
“Sikujui! Ila sauti yako…? Sauti yako si ngeni
kabisa masikioni mwangu…ni nani wewe? Na
huyu dada…ni nani? Mnanitakia nini?”
“Mnh! This is interesting…kwamba hunikumbuki
kabisa ila sauti yangu unaikumbuka?” Babu
alisaili tena.
“Hebu acha mambo ya kis…nge hapa wewee! Mi
nakuuliza maswali unajitia kukomaa na hilo la
kuwa sikukumbuki? Nimekwambia sikujui na
nataka nipate maelezo ya mchezo huu haraka
sana!” Jamaa alimjia juu.
“Ondoka hapa jijini wewe, usiwe mjinga! Hutakiwi
kuwepo hapa na wala hukutakiwa kuwepo kule
makaburini leo hii…!” Yule dada alidakia kwa
hasira.
“Excuse me…na wewe ni nani tena?” Jamaa
alihoji zaidi.
“Okay Grey, nadhani tunahitaji kuwekana sawa
kwanza hapa…” Yule mtu mzima alisema, na
jamaa akaonekana kumakinika baada ya kusikia
akitajwa kwa jina lake.
“Unalijua jina langu?”
“Na zaidi ya hapo…tutulie, tuwekane sawa…”
Mzee alimjibu.
“Sawa…anza maelezo.”
“Naitwa Benson Kanga…”
“Jina geni masikioni kwangu hilo…”
“Si ajabu kuwa hivyo, lakini ridhika tu kuwa hilo
ndio jina langu na niko upande wako.”
“Mnh, sasa kama mko upande wangu…kwa nini
hamkunijia kistaarabu zaidi?”
“Ni ngumu kidogo kuelezea…ila tu ni kwamba
baada ya kifo cha Nouman Fattawi…na mchango
wako hadi kufikia kwenye kifo kile, hukutakiwa
kabisa kuonekana popote pale ambapo japo
mzuka tu wa Nouman ungekuwepo. Uwepo wako
pale makaburini leo ulikuwa unahatarisha sana
swala hili. Watu wengine watapoteza maisha yao
bure…” Mtu aliyenadi kuwa ni Benson Kanga
alimwambia.
Yule mtu aliyetambuliwa na Benson kwa jina la
Brey alimung’unya midomo kwa namna
iliyoonesha kuwa alimuelewa sana, ingawa kama
angewepo mtu mwingine anayewasikiliza wakati
ule ambaye si katika wao, hakika asingeelewa
kitu.
“Ni kweli, lakini ilikuwa ni muhimu kujihakikishia
kuwa ni kweli Nouman Fattawi amezikwa,
Benson.”
“Haikuwa lazima uwepo pale makaburini ili
kupata uhakika wa hilo. Mimi kazi yangu ni
kuhakikisha kuwa swala zima la Nouman Fattawi
linabakia kuwa limezikwa. Nouman Fattawi
anatakiwa asahaulike kabisa kwenye uso wa
dunia…uwepo wako jijini na hususan pale
makaburini leo hii hausidii sana kwenye hilo.”
Benson Kanga alimwambia.
“Kwa hiyo mliniona nikiwa pale makaburini?”
“Tulikuhisi kuwa ni wewe pale ulipoingia
makaburini ila hatukuwa na uhakika…umebadilika
sana katika miaka michache ya hapa kati, Brey…
lakini baada ya maziko hatukukuona ukitoka…
tukapata wasiwasi. Ndio ikabidi nimtume
msaidizi wangu arudi pale kukuchomoa mle
makaburini”
“Mlijua kuwa nimo mle?”
“Ndio jibu pekee lililopatikana Brey…tumeona mtu
anayeshabihiana na wewe akiingia kisha
akatupotea mle mle makaburini. Tukaweka kambi
kwenye milango yote miwili ya kutokea nje ya
makaburi, na bado hatukukuoana ukitoka…ikabidi
tubahatishe kwa njia ile. Na imesaidia…”
Brey Jabba alitikisa kichwa.
“Hivyo ndivyo ilivyokuwa…ilibidi tujihakikishie
kuwa ni wewe kweli, ndio maana ikabidi tujihami
kwa bastola namna ile pale ulipoingia humu
ndani…”
“Nimeelewa.”
“Basi sasa fanya utoweke hapa jijini…ukae mbali
sana na jiji...huo ndio ulikuwa utaratibu. Hatutaki
ya Fattawi yaje yakukute…kazi yako umeifanya
kwa hiyo sasa nenda ukaanze maisha mapya nje
ya jiji. Tayari umeshaandaliwa pa kwenda…
natakiwa nihakikishe umefika huko na nikuache
huko. Sahau kila kitu kuhusu kazi uliyoifanya
kwenye swala la Nouman Fattawi!” Benson
alimwambia.
“Nadhani mmechelewa…” Brey Jabba alimjibu.
“Ukimaanisha nini?”
“Kuna watu nimewaona wakiingia hapa hoteini…
kama dakika tano baada ya huyu msaidizi wako
kuingia…wamenitia mashaka sana.”
Wenyeji wake wote wawili wakamakinika.
“Unamaanisha nini…? Ni watu gani?”
“Wana asili ya asia wale jamaa…kimuonekano tu
ni kama wapakistani, au wa-afghanistan…lakini
sio waarabu. Hii hoteli iko sinza, sidhani kama
watu kama wale ni wa kuja kukaa hoteli ya
sinza...wangekaa angalau kariakoo huko au
katikati ya jiji…” Brey Jabba alisema.
Benson aliguna.
“Unamaanisha nini?”
“Kwamba wao, kama mimi, waliweza kumfuata
huyu msaidizi wako kutoka huko alipokuwa hadi
hapa…”
“No! Hilo haliwezekani! Nilikuwa makini sana…”
Mwanadada alimaka, na kuendelea, “…mbona
wewe nilikuona wakati unanifuata na nilikuacha
kwa kuwa nilitaka uje hapa!”
“Sawa. Ulimakinika na mimi…hukuweza
kumakinika na wale wengine…jamaa wamo humu
hotelini nawaambia.” Brey Jabba alisema.
“Lazima tutoweka hapa…sasa hivi!” Benson
alisema huku akiinuka. Akaganda kwenye hatua
zake pale wote mle ndani waliposikia mlango wa
kile chumba walichokuwamo ukabishwa hodi
kutokea nje.
Wakatazamana, wakiwa kimya, macho
yakiwatembea.
Hodi ikabishwa kwa mara ya pili, kwa nguvu
zaidi.
“Wamefika.” Brey Jabba alisema kwa utulivu wa
kuogopesha…
***mnh! Kuna usiri ndani ya usiri hapa
 
Dah mbona kimya sana mazeee wimbo wa gaidi haupati aitime kihivyo tatizo nn
 
Dah mbona kimya sana mazeee wimbo wa gaidi haupati aitime kihivyo tatizo nn
Wimbo wa Gaidi mtunzi wake ni Hussein Tuwa na alikua akitoa kwenye ukurasa wa Kona ya Riwaya Reloaded kule Facebook..

hadithi imesitishwa kwa kuwa atatoa kitabu chake
 
Wimbo wa Gaidi mtunzi wake ni Hussein Tuwa na alikua akitoa kwenye ukurasa wa Kona ya Riwaya Reloaded kule Facebook..

hadithi imesitishwa kwa kuwa atatoa kitabu chake
Dah haya atakapotoa mtuambie vinakopatikana mana sie wengine riwaya ndio starehe zetu
 
Wimbo wa Gaidi mtunzi wake ni Hussein Tuwa na alikua akitoa kwenye ukurasa wa Kona ya Riwaya Reloaded kule Facebook..

hadithi imesitishwa kwa kuwa atatoa kitabu chake
mkuu kitabu kipo kwenye funal na kasema anatoa kwa idadi maalum tuu hivyo nawe kama wakihitaji ni PM nikutumie namba ya zamira ili akuweke kwenye list ya wanaotaka kitabu cha brey jaba
 
Dah kila siku nakatiza kimyax2 kucheki kama umeupdate,fanya mambo mkuu unatutesa sana wapenzi wa riwaya.
 
usiwe na shaka mkuu kama kule fb ni free port basi hata hapa ni ruksa mkuu. maana kule hakuna kulipia why hapa tuikosee?? na uzuri hana group la kulipia kama watunzi wengine .

kama nimekosea nambie mkuu.bado hii kitu hajaitolea kitabu ndio maaana ipo free
Naomba account I'd ya Facebook!!
 
Back
Top Bottom