Wimbo mpya wa Young Killer, jumba bovu anaangushiwa Harmonize

kijanamtanashati

JF-Expert Member
Aug 22, 2014
516
903
Jana young killer msodoki alidondosha kichupa chake kipya ambacho humo ndani amemshirikisha msanii kutoka lebo ya WCB, cha ajabu video hiyo toka imewekwa jana usiku mpaka sasa inaongoza kuwa na dislike nyingi kuliko like.

Kitu ambacho kimeteka hisia za wengi juu ya ngoma hiyo ni upande wa comments, kwani comments nyingi ambazo watu wametupia katika mtandao huo wa YouTube zimekuwa zikimponda harmonize kuwa hakuitendea haki nyimbo hiyo, ameimba kiitikio vibaya haijawahi kutokea.

Wengine wameenda mbali zaidi na kusema kuwa harmonize amezidi kumuiga sana boss wake mpaka imekuwa kero kwani wanashindwa kutofautisha sauti za watu hao wawili. wengine wamediriki kutupia comments kuwa wameweka dislike kwa hiyo nyimbo kwa sababu ya harmonize.

Kuna baadhi ya comments zimedai kuwa, kiitikio hiko angeimba rich mavoko basi angekitendea haki ipasavyo kuliko harmonize. mpaka sasa katika video hiyo ina dislikes zaidi ya 3,000 na likes 2,000 huku ikiwa ina views zaidi ya 100,000 ndani ya masaa 18.
 
Jana young killer msodoki alidondosha kichupa chake kipya ambacho humo ndani amemshirikisha msanii kutoka lebo ya WCB, cha ajabu video hiyo toka imewekwa jana usiku mpaka sasa inaongoza kuwa na dislike nyingi kuliko like.

Kitu ambacho kimeteka hisia za wengi juu ya ngoma hiyo ni upande wa comments, kwani comments nyingi ambazo watu wametupia katika mtandao huo wa YouTube zimekuwa zikimponda harmonize kuwa hakuitendea haki nyimbo hiyo, ameimba kiitikio vibaya haijawahi kutokea.

Wengine wameenda mbali zaidi na kusema kuwa harmonize amezidi kumuiga sana boss wake mpaka imekuwa kero kwani wanashindwa kutofautisha sauti za watu hao wawili. wengine wamediriki kutupia comments kuwa wameweka dislike kwa hiyo nyimbo kwa sababu ya harmonize.

Kuna baadhi ya comments zimedai kuwa, kiitikio hiko angeimba rich mavoko basi angekitendea haki ipasavyo kuliko harmonize. mpaka sasa katika video hiyo ina dislikes zaidi ya 3,000 na likes 2,000 huku ikiwa ina views zaidi ya 100,000 ndani ya masaa 18.



wakubeba mikoba pale WCB Ni Rayvan huyu konde boy hapana kwa kweli
 
Angeimba Mavoko wangesema tena " Tangu Mavoko usainiwe WCB sijui unaimba nini, umavoko wako umeisha.

- Anyways kuhusu DISLIKES wala hata usijali maana unajua wimbo wa JUSTIN BIEBER uliomtambulisha ULIMWENGUNI wa BABY ndio wimbo wenye DISLIKES Nyingi Duniani
Hahaha huwa nashangaa hizo dislike huwa zinatoka wapi kwenye huo wimbo wa justin B
 
- AIYOLA

- BADO

- KIDONDA CHANGU

- MATATIZO

- HAPPY BIRTHDAY

- SHOW ME

- INDE
ila haimaanishi kuwa na list hiyo ya hits ndio ataendelea kuwa masikioni mwa watu, mwenzie yule ana nyimbo chache ila ni alama ya kipaji halisi na chenye ubunifu, kama ulikuwa humfatilii anza sasa
 
ila haimaanishi kuwa na list hiyo ya hits ndio ataendelea kuwa masikioni mwa watu, mwenzie yule ana nyimbo chache ila ni alama ya kipaji halisi na chenye ubunifu, kama ulikuwa humfatilii anza sasa
Ndugu yangu mimi ninachoangalia ni INFUENCE ya MSANII na MAUZO kwenye PLATFORM za MAUZO EAST AFRICA

- Ukimtoa Diamond, Harmonize ndo "the most subscribed artist kwenye mtandao wa YouTube" hata kwa VIEWS ana shika namba 2 baada ya Domo. Hata hapo www.wasafi.com Nyimbo zake zinauza balaa baada ya domo

- Kumbuka hata hatutumii ushabiki ni FACTS zilizopo mezani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom