Naona kama kwamba ulipokuwa unaandika huenda mlikuwa pamoja na lusungo. Sawa kabisa, lakini kesho yako huijui. Fikiri tu maneno ka haya, nami naku quote;
Chakujiuliza ni kuwa hivi hawa vikongwe walipokuwa kwenye system 'walikula ujana' pasi kujua kesho inajengwa na leo?
Hawa waajiri hawajawaona watu wenye sifa stahiki mpaka wawaajiri hawa vikongwe?
*kula sana ujana ukumbe fainali uzeeni*
Weye na lusungo, tayari mshafikia hiyo fainali au ndo mnajiona kama kwamba hao hawakuwa na akili? Jamani, msiseme hivyo. Hakuna hata mmoja wetu anayetamani kesho ije.
Wengi waliathiriwa na mfumo wa serekali isiyojali utu wa mtu. Wengi wameathiriwa na vijana wao walio angukia kwenye mawazo ya kutomjali mzazi wake.
Baba ni baba tu, hata kama kakupatia kwenye mbio za mwengi, ukiisha mjua, kama weye una nafasi nzuri, mpende tu, ni babako huyo kakuzaa.