William Ruto na dhihaka kwa ujio wa Obama!

HAMY-D

JF-Expert Member
Sep 18, 2011
7,149
3,817
attachment.php



WanaJF!

Nimekuwa nikiwaza mahusiano ya Tanzania na nchi jirani za Afrika ya mashariki baada ya ujio wa Obama yatakuwaje?

Kwani inasemekana kitendo cha Obama kuja Tanzania na kuiruka Kenya, kimeleta gumzo, sio tu ndani ya Kenya, bali hata mataifa mengine yameshangazwa na kitendo hicho. Kwani ukizingatia asili ya rais Obama na ahadi yake kwa Kenya, ni wazi kwamba alipaswa atembelee na Kenya kama sehemu ya ziara yake hapa Afrika mashariki.

Sitakuwa na mengi ya binafsi juu ya hili la Ruto na dhihaka yake kwa ujio wa Obama Afrika, bali nime ambatanisha maelezo yake mwenyewe kama ifuatavyo;


NAIBU wa Rais Bw William Ruto, jana alivunja kimya chake kuhusu hatua ya rais wa Marekani Barack Obama kutozuru nchini Kenya kwa kusema hatua hiyo haina madhara yoyote kwa Kenya.

Huku akiongea katika kanisa la Katoliki la St Gabriel Bahati, kaunti ya Nakuru, Bw Ruto alisema "nchi hii ina 'marafiki' wengine wengi duniani ambao inaweza kushirikiana nao huku akiongezea kuwa hatua ya rais Obama kukwepa kutembelea Kenya haiwezi kutatiza kwa vyovyote vile uhusiano mwema uliopo wa kibiashara baina ya Marekani na Kenya."

Bwana Ruto akasema, "Tunaiheshimu nchi ya Marekani nayo inafaa kuwaheshimu Wakenya,"

Alisema serikali ya Kenya tayari imeanzisha mikakati ya kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na mataifa mengine huku akikariri kuwa safari ya Rais Uhuru Kenyatta nchini Uganda ambapo alikutana na rais wa nchi hiyo Yoweri Museveni na mwenzao wa Rwanda rais Paul Kagame kujadili jinsi nchi hizo tatu zinaweza kushirikiana kibiashara, ni miongoni mwa mikakati hiyo.

Pia akaongezea, "Nchi yetu inamcha Mungu na kamwe hatutaruhusu mataifa ya kigeni kutuletea tamaduni ambazo zinakinzana na desturi zetu," akasema Bw Ruto huku akirejea hotuba ya Rais Obama nchini Senegal ambapo aliitaka nchi hiyo kuheshimu haki za Mashoga."
 

Attachments

  • IMG-20130701-WA0000.jpg
    IMG-20130701-WA0000.jpg
    29.5 KB · Views: 7,705
...

Pia akaongezea, "Nchi yetu inamcha Mungu na kamwe hatutaruhusu mataifa ya kigeni kutuletea tamaduni ambazo zinakinzana na desturi zetu," akasema Bw Ruto huku akirejelea hotuba ya Rais Obama nchini Senegal ambapo aliitaka nchi hiyo kuheshimu haki za Mashoga."

...


Nakubaliana na hoja iliyoko hapo kwenye red japo sikubaliani na hoja za Rais wa Senegal ambazo Ruto amezitumia kama rejea. Rais wa Senegal "amejitetea" mbele ya Obama kwamba hawezi kuruhusu "haki za mashoga" just because Senegal ina "waislamu wengi". Utetezi mfu kabisa kwa Rais wa nchi.
 
Kenya wana wivu wa kijinga sana, nilikuwa naangalia TV moja ya kenya leo asubuhi imenishangaza sana sikujua kama hiliswala la Obama kuja Tanzania limewaathiri kwa kiasi kikubwa hivyo. mtangazaji mmoja akasema "Obama angekuja Kenya akae hata masaa mawili", mwingine akasema "hata bila US kenya itaendelea tu na inazidi kusonga mbele." Yaani Wakenya wamekuwa very desperate, wanatamani hata kulia. Huku Watanzania wengi wanaona hiyo ni ishu ya kawaida sana kutembelewa na marais wa US ambao huja kuzoa utajiri wetu.
 
Kenya wana wivu wa kijinga sana, nilikuwa naangalia TV moja ya kenya leo asubuhi imenishangaza sana sikujua kama hiliswala la Obama kuja Tanzania limewaathiri kwa kiasi kikubwa hivyo. mtangazaji mmoja akasema "Obama angekuja Kenya akae hata masaa mawili", mwingine akasema "hata bila US kenya itaendelea tu na inazidi kusonga mbele." Yaani Wakenya wamekuwa very desperate, wanatamani hata kulia. Huku Watanzania wengi wanaona hiyo ni ishu ya kawaida sana kutembelewa na marais wa US ambao huja kuzoa utajiri wetu.

Lazima tu wangekuwa na wivu, maana aliahidi kwenda!
 
hao akina ruto wanajiliwaza bure na kutaka kenyans wasione kama ni issue obana ku-skip nchi yao. Kwani hawajui kuwa wao ndo kikwazo cha obama kutokwenda kenya??
 
Kumbe kutembelewa na Obama ni ujiko? Sikujua hilo, Kama walinzi wake tu wana fanya sorting ya mawaziri and other gorvernment officials wa kwenda kumsalimu, ni dhihaka kiasi gani hiyo? Mzee mchonga aliisha wahi mpa kifimbo chake Malkia Elizabeth!
 
Tanzania can survive without Kenya,Uganda and Rwanda! Museveni ni ndumila kuwili yetu macho lets wait and see!
 
Sijui kama kuna issue hapa, pengine kama angetembelea Rwanda na kuacha Tanzania yangesemwa haya haya. Sijaona cha ajabu mpaka mjisumbue kufuatilia yanayosemwa Kenya au popote pale. Kwani ujio wa Obama unatuongezea nini ambacho Kenya watakikosa. Ukiangalia katika maelezo ya Obama kuhusu mradi wake wa 'Power Africa' Kenya ni mojawapo ya nchi hizo. Kumbuka Kenya ina uhusiano wa muda mrefu wa kibiashara na Marekani na hawana (Wamarekani) wasiwasi wowote; wana mizizi yao huko, na Obama ua bila Obama. Tanzania ni uhusiano mpya wanaoutafuta kwa kila njia, ili wajiimarishe pia na pengine kwa matakwa mengine nyuma ya pazia tusiyoyajua sisi! Nashauri achaneni na kuleta habari hizi zisizo na maana na kuonyesha tu kuwa sisi tumefaidika kuliko Kenya, na kuwa Kenya wanalalamika na kutuonea wivu; ambayo si kweli.
 
Sijui kama kuna issue hapa, pengine kama angetembelea Rwanda na kuacha Tanzania yangesemwa haya haya. Sijaona cha ajabu mpaka mjisumbue kufuatilia yanayosemwa Kenya au popote pale. Kwani ujio wa Obama unatuongezea nini ambacho Kenya watakikosa. Ukiangalia katika maelezo ya Obama kuhusu mradi wake wa 'Power Africa' Kenya ni mojawapo ya nchi hizo. Kumbuka Kenya ina uhusiano wa muda mrefu wa kibiashara na Marekani na hawana (Wamarekani) wasiwasi wowote; wana mizizi yao huko, na Obama ua bila Obama. Tanzania ni uhusiano mpya wanaoutafuta kwa kila njia, ili wajiimarishe pia na pengine kwa matakwa mengine nyuma ya pazia tusiyoyajua sisi! Nashauri achaneni na kuleta habari hizi zisizo na maana na kuonyesha tu kuwa sisi tumefaidika kuliko Kenya, na kuwa Kenya wanalalamika na kutuonea wivu; ambayo si kweli.

si mpaka wana himaya yao ya kijeshi huko kenya mkuu inayoangalia maslahi ya kijeshi ya marekani mwambao wa North East africa? unisahihishe kama network imekata huku kichwani mwangu.
 
mm nilkikuwa sijui kumbe anatuletea mambo ya ushoga huku hivi hajui kuwa kila nchi ina tamaduni na mila zake kwaninni anataka kutuambukiza roho chafu kiasi hicho anataka vizazi vyetu vipotee na kusahau mila na desturi zao mm sioni chochote cha maana kinachomjia hapa kwetu kama sio kutulia maliasili yetu na kutuangamiza kiuchumi
 
si mpaka wana himaya yao ya kijeshi huko kenya mkuu inayoangalia maslahi ya kijeshi ya marekani mwambao wa North East africa? unisahihishe kama network imekata huku kichwani mwangu.

Ndiyo, wana kila kitu kule, jeshi, ujasusi na biashara na wanajua wote kuwa haitaporomoka kwa sababu ya kutotembelewa na Obama. Wako imara, ndiyo maana kwao (Wamarekani) kwenda huko siyo issue. Kama utakumbuka tulipotaka msaada wa kupeleleza mauaji ya Padri kule Zanzibar na bomu la kanisanai Arusha, FBI walitoka Nairobi! Wamarekani wanatafuta imaya mpya kwa maslahi yao.
 
Ina maana Obama haendi kumtembelea nyanya yake kule Kobelo? Duh, amewadharau sana jamaa!
 
Tanzania can survive without Kenya,Uganda and Rwanda! Museveni ni ndumila kuwili yetu macho lets wait and see!


Kweli kabisa mkuu!MUSEVEN nafsi inamsuta kila akikumbuka tulivyomsaidia kuuupata ufalme (Urais wa maisha bila kikomo) wa UGANDA. Ndiyo maana anakosa msimamo. Kuishi na jirani yako vizuri na kushirikiana naye ni jambo la msingi lakini kama yeye hataki usimlazimishe. Hatupungukiwi chochote tukitengwa na hawa jamaa. Tuimarishe uhusiano na Burundi na Congo DRC pamoja na mataifa wanachama wa SADC tuone kama tutapungukiwa kitu.
 
Kenya watulie tu, Obama ni wa kwao na ataenda tu Kenya. Tatizo ni kuwa kaja Tanzania. Kenya wana wivu sana, na tunawajua, kwani tunafanyanao kazi! Hili ndo tatizo!
 
Lazima tu wangekuwa na wivu, maana aliahidi kwenda!

Mkuu wakati anaahidi kutembelea Kenya walikuwa hawajawachagua hawa washtakiwa wa ICC! .

Sababu kubwa iliyomfanya asitembelee Kenya ni kutokana na kesi inayowakabili Raisi na Makamu wake ICC.
 
Back
Top Bottom