Wilaya ya Nkasi na Mfumo wa ESS

Wilaya ya Nkasi na Mfumo wa ESS

HESC

Member
Joined
Jul 18, 2015
Posts
5
Reaction score
1
Ndugu zangu hii naiona wilaya ya Nkasi iliyoko mkoani Rukwa , wilaya hii ni ngumu sana kupata uhamisho hasa kupitia mfumo wa Ess ambao uliletwa mbali na shughuli nyingine kumrahisishia mtumishi kufanya maombi ya uhamisho , Katika wilaya ya Nkasi maombi ya uhamisho tena yenye vigezo kabisa katika mfumo huu wa ESS Wala ayajibiwi yanaishia ngazi za chini kabisa eti wanadai wanaogopa kupungukiwa watumishi , Nkasi kigezo Cha kumwamisha mtumishi ni ndoa peke yake , vigezo vingine vilivyo kwenye huu mfumo avipewi nafasi kabisa , labda uelewa wangu mdogo vipi katika almashauri nyingine tujuzane mambo yakoje au mwenye uelewa kuhusu hizo taratibu za uhamisho kwenye mfumo wa ESS wakuu maana huku Nkasi wanachojali ni kujaza PEPMISS
 
Wilaya yangu hiyo imejaa vilaza sana,mkuu ungekuwa kirando Republic usinge hama Nkasi,hakika.
 
Mimi ni Clinical Officer, mkuu lakini concern yangu ni kuwa wilaya ya Nkasi inapuuza sana maombi yaliyo katika mfumo wa ESS , wanayatazama tu , kazi Yao kubwa nikuhimiza ujazaji wa majukumu, pia wilaya ya Nkasi imekaa kirushwa rushwa hivi maana mtu akifanikiwa kutoka ukiuliza anakuambia jipange uwezi kutoka kirahisi pale,
 
Kaa huko Nkasi uwahudumie.
wakati unaomba ajira Nkasi hukupaona mbali...hivi sasa ndio unataka upakimbie.
 
Back
Top Bottom