WikiLeaks: Lowassa's corrupt activities have been an open secret throughout Tanzania for many years

Masilahi ya Taifa..kwann unakimbilia kuamini kwamba gazeti la citizen wanamsafisha Lowasa?kwani Lowasa amechafuka? Chombo ambacho kina mamlaka ya kusema Lowasa ni mchafu ni mahakama peke yake,je mahakama ilishawahi kutangaza?Gazeti la citizen wanajaribu kuwafumbua wananchi macho yao yaliofumbwa mda mrefu na wapinzani wa lowasa kua yeye ni fisadi.Gazeti "halimsafishi" lowasa bali lina "clear misunderstanding" kuhusu yeye.Watu wameaminishwa uongo huu mda mrefu lakini umefika mda sasa wa maji kujitenga na mafuta.Kwa bahati nzuri wasio mtakia mema Lowasa waliijua njia ya Lowasa anayotaka kupita,lowasa alionyesha dhamira ya kupambana na umasikini tokea"1995" hili wabaya wake hawakulipenda hata kidogo ndo mana wana muandama.Kwangu naamini wanaomchafua lowasa "2015" ndio hao hao walio anza kumchafua"1995".Hivyo naiomba kambi ya lowasa ijue kua Mkuu wao ana damu ya KUNGUNI hata akiwa Raisi baada ya uchaguzi wa mwaka huu haya yataendelea kumtokea.Kama lowasa hajui mwambieni kua yeye kusemwa na kutukanwa kwake ni "fate" au destine" yake,hayo ndo majaaliwa yake,kuchafuliwa ndio hatima yake,lakini asilan abadani hatima hii au majaaliwa haya hayatamzuia kuingia IKULU 2015, wapiga firimbi wanabadilisha wimbo tu,1995 walimwambia amejilimbikizia mali lakini hawasemi ameziibia wapi,baadae tena wakaja na hoja eti amefuja mradi wa" kituo cha mikutano cha kimataifa Arusha" walipo ona wimbo huo hauchezeke na watu wa kizazi cha dot com,wakaja na Richmond,ndo mana akaamua ajiuzulu kuonyesha kua yeye kwake "cheo sio ishu" na wala hatumii cheo kupata mali kama mnavyo taka sisi tuamini.Lowasa anadhamira ya dhati ya kufanya jambo flani kwa taifa,hata kama ataiba kama mnavyo sema,lakini nina imani kabisa kuna jambo zuri atatufanyia watanzania.Lowasa wamemchafua lakini sisi wapiga kura hatukumchafua,ndo maana tuna mlaki kwa maelfu na tunamdhamini kwa wingi sana.Tena wapiga kura wengi wala hawasomi mnacho andika kwani "wabongo"hatupendi kusoma vilivyo andikwa,sisi tuna penda kusikiliza,na masikio yetu tumempa Lowasa,

Wahenga wanasema"mchawi mpe mtoto alee" SISI na sio NYINYI tumeamua kumpa lowasa hii nchi kwa miaka 10 ijayo.ATATUVUSHA NDANI YA SAFARI YA MATUMAINI.

Nitukane kama utajiskia hivyo au nidharau kama utapenda.,
 
Masilahi ya Taifa

Sina shaka kwamba hii ndiyo post bora kabisa kuhusu mgombea huyu.

Labda watanzania tuwe na kumbukumbu za panzi. Mwl Nyerere, baba wa taifa letu alishaweka wazi kuhusu ugombea wa Lowassa.

Sijui tumerogwa na nani. Huyu mtu hastahili hata kujadiliwa achilia mbali kudiriki kugombea.
ULICHOSEMA NI UKWELI MTUPU..
ILA UKWELI WAKO UTATHIBITIKA ZAIDI PALE CCM ITAKAPOMTEUA E.LOWASA KUWA MPEPERUSHA BENDERA YAKE KWENYE UCHAGUZI MKUU.
binafsi siamini kama CCM watauingia huu mtego wa LOWASA, ila kama watauingia na kumsimamisha. mungu naapa nitaanza kuichukia hii nchi na watu wake
 
Last edited by a moderator:
ULICHOSEMA NI UKWELI MTUPU..
ILA UKWELI WAKO UTATHIBITIKA ZAIDI PALE CCM ITAKAPOMTEUA E.LOWASA KUWA MPEPERUSHA BENDERA YAKE KWENYE UCHAGUZI MKUU.
binafsi siamini kama CCM watauingia huu mtego wa LOWASA, ila kama watauingia na kumsimamisha. mungu naapa nitaanza kuichukia hii nchi na watu wake

Napenda kuamini kwamba angalau hili la Lowassa ccm wataliona mapema na kukata jina lake mwanzo kabisa wa mchakato ili tuanze kupata matumaini ya kupata kiongozi nafuu au bora.
 
Kama wewe ni UKAWA Membe kaingiaje hapo??
Lowasa ni fisadi mkubwa na wezi wenzake, itakuwa makosa makubwa kuwapa mafisadi Ikulu!!
China walifanikiwa kuinua uchumi baada ya kuwachulia hatua kali mafisadi hadi kuwanyonga!!
Hakuna kucheka na wezi sehemu yao ni jela period!!
 
Sasa na wewe Jenerali Membe katokea wapi? Anayezungumzwa kwenye uzi huu ni EL. Endapo atakatwa, jambo ambalo ni dhahiri, haina maana kwamba atakayeteuliwa ni Membe. Kuna wagombea wengine chungu nzima!
 
Kwa lugha nyingine alibebeshwa zigo la Serikali. Lakini jambo lingine la kutafakari ni hili; Ile mitambo ya Richmond iliyokataliwa na kamati ya Madini na Nishati chini ya Mwenyekiti Shelukindo, isinunuliwe na kumilikiwa na serikali chini ya TANESCO, kwa madai ya kuwa mibovu, ndiyo iliyouzwa kwa Dowans na Rais wa Marekani Mh. Obama alipokuja kwa ziara Tanzania, pamoja na mambo mengine alizindua mitambo hiyo ambayo inazalisha umeme hata leo.

Sasa je na hapo alaumiwe Lowassa?

Ikumbukwe kuwa mchakato wa kumpata mkandarasi wa kutupatia umeme wa dharula kutokana na tishio la nchi kuingia gizani ulipitia kwenye baraza la mawaziri chini ya mwenyekiti wake na kupata baraka zote na baraza lenyewe lakini pia na mwenyekiti wa baraza la mawaziri.

Baraza lilitambuwa kwamba Edward Lowassa alipeleka katika baraza maoni na ushauri kitaalamu alioupokea kutoka kwa watendaji wa wizara, baraza halikuwa na shaka kabisa na Edward Lowassa, likitambua kuwa Mh. Lowassa ni mchapakazi asiyependa kuona nchi inaingia katika taharuki ya kukosa huduma muhimu inayoweza kukwamisha masuala mtambuka kukwama.

Ofisi yake ikabeba jahazi akapewa zoezi la kufuatilia kwa uharaka upatikanaji wa mkandarasi huyo yeye akiwa kama kiranja mkuu wa usimamizi wa serikali na maazimio ya baraza la mawaziri haswa ukizingatia mchakato huu ulipitia katika njia za kitaalam kwa kupata ushauri na baraka zote za baraza la wataalamu kwa maana ya makatibu wakuu kama washauri na barua ya mawaziri kama ushahidi wa kile kinachofanyika kuwa ni sahihi, ripoti kutoka kwa mwanasheria mkuu wa serekali inaonyesha dhahiri katika mchakato huu
Mh. Lowassa bali wataalamu na makatibu wa wizara.

Utaratibu uliopitia unaweka wazi sura ya kuwa serikali yote ilishiriki na kufanya maamuzi juu ya mchakato wa kandarasi ya umeme wa dharula na kufikia maamuzi juu ya kuipa kandarasi hiyo kampuni ya richmond hivyo lowassa kama kiranja mkuu alisimamia maamuzi ya baraza na si yake wala ya familia yake.

Ikumbukwe mara kadhaa Lowassa alitia mashaka juu ya kampuni hii na kutaka kughailisha mkataba na kampuni hii lakini mamlaka zilizokuwa juu yake zilimsihi kuendelea na maelekezo aliyopewa kama kiranja mkuu.

Kilichomponza Lowassa ni dhana yake ya utiifu kwa mamlaka za juu yake alitekeleza kwa hekima kile alichoshauriwa kufanya na hapo ndiyo tukaipata Richmond iliyosabibisha ajali ya kisiasa.

Mh. Lowassa ni kiongozi anaetambua fika matakwa ya watanzania kwa muda mrefu kwani yupo kwenye siasa na serikali kwa ujumla zaidi ya miaka 20 hivyo anaelewa fika kuwa Tanzania yetu inahitaji maboresho ya elimu ambayo itamnufaisha kila mtanzania pamoja huduma bora za kijamii.

Vile vile tatizo sugu la ajira ni suala lingine ambalo Mh. Lowassa analitilia mkazo sana kwani vijana wanatakiwa wapewe kipaumbele kwani fursa zipo nyingi.

Suala la matumizi sahihi ya rasilimali zetu kama vile madini, gesi na mafuta pia hivi vyote ni lazima vitumike kwa ajili ya manufaa ya watanzania na sio watu binafsi; ufufuaji na ukuzaji wa viwanda vyetu na kuwapa nafasi wafanyabiashara na wawekezaji wa ndani ili kukuza uchumi wetu lakini bila kusahau suala la kudumisha haki na usawa kwa kila mtanzania kwani watu wote ni sawa! Suala la mwisho nchi yetu inahitaji utawala bora unaozingatia na kufuata sera na misingi bora ya kidemokrasia ili kuleta maendeleo katika nyanja mbalimbali.

Ametujengea na kusimamia ujenzi wa shule za sekondari za kata, amesimamia ujenzi wa Chuo Kikuu cha Dodoma(UDOM).

Amejenga mradi wa maji safi wa ziwa Victoria katika mikoa ya nyanda ya kati na ukanda wa ziwa.

Amejenga zahanati vijijini, barabara, vyuo vya ufundi stadi.

Ametoa misaada ya boda boda kwa vijana kama sehemu ya kujiajiri.

Huyu ndiye aliyewapokonya wahindi lile eneo la mnazi mmoja na kulirudisha kwa wazawa.

Huyu ndiye aliyesitisha mkataba wa City Water, hakuishia hapo bado amekuwa akijitoa sana katika kusaidia jamii mbalimbali bila kujali ubaguzi wowote ule na ndio maana #TunaImaniNaye
 
Huwenda alionewa kweli,Je vipi hao jamaa zake nao (Chenge,Karamagi,Tibaijuka,Rostam,etc) ni wasafi pia?Na je watakuwa na ushawiahi wowote katika utawala wa Laigwanani?That is what scares the hell out of us,His friends!
 
Tumewachoka Na Uyo Lowa Saa Wenu Hebu Tupeni Nafasi Tujadili Issue Zingine Kama Wabunge Kutuibia Uyo Lowasa Wenu Tafteni Mahali Mumuweke Muwe Mnamtizama Kila Saa Mana Rangi Yake Nyeupe Na Minywele Meupe Na Shingo Isiogeuka Kushoto Wala Kulia Inakuwa Burdani Sana Kwenu
 
Na asipopata huo urais sijui ndo itakuaje.... nani anafahamu kitakachotokea?
 
Napita tuuu nawasubiri wote kutoka pande mbili positive & negative mimi nitakuwa muamuzi wa kati
 
"tumeamua tumpitishe mh.lowassa ili kukiokoa chama kisisambaratike".kwa sauti ya mwenyekiti wa CCM taifa.
 
Kama alishindwa kuvunja system ya ulaji wa Richmond basi hawezi vunja system ya ufisadi wowote nchini chini ya ccm.
 
ni kama uliwekwa headfone kutetea kitu usichokijua. umeeleza kwamba hahusiki na richmond, mbwembwe zingne zinahusikaje hapo? yu can fool some people sometime but yu can't fool all people all the time. WATANZANIA WA LEO HATUDANGANYIKI, TUTAKULA VYA MAFISADI NA KUCHAGUA KILICHO BORA ZAIDI.
 
Back
Top Bottom