KERO Wiki ya pili hii tunashindwa kununua hisa za CRDB

KERO Wiki ya pili hii tunashindwa kununua hisa za CRDB

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua

Gotze Giyani

Senior Member
Joined
Feb 28, 2022
Posts
143
Reaction score
212
Wadau habarini za muda huu kuna tatizo gani mbona ni wiki 2 inaisha tunashindwa kununua Hisa za CRDB nimewasilina na DSE na broker Mara zaidi ya 5 wanasema shida ni kwenye market hivyo wataalamu wa uchumi na Hisa naombeni msaada wenu je vipi kuhusu Hisa za DSE nazo zinagawio kama za CRDB.Maana hadi sasa naona hisa za trillion 4 kitu ambacho hakuna kampuni kwenye DSE imefikia.
 
Ili ununue lazima bidhaa iwepo sokoni. Ipo? KWa bei ipi? Bei uliyoweka wewe ni ipi??
 
Bei 1510 ndio nimeweka na ndio iliyepo sokoni
Ni kweli kuwa sasa hivi bei ni hiyo uliyoitaja, ila ukiangalia pale kwenye section ya "sell" haina wauzaji, watu hawauzi ndio maana hiki kipindi imekuwa ngumu sana kuzipata hisa hizi sokoni.
 
Ni kweli kuwa sasa hivi bei ni hiyo uliyoitaja, ila ukiangalia pale kwenye section ya "sell" haina wauzaji, watu hawauzi ndio maana hiki kipindi imekuwa ngumu sana kuzipata hisa hizi sokoni.
Hisa kutokuuzwa ni dalili kuwa kampuni husika inafanya vizuri kwenye boashara zake , wenye hisa wanaridhika na gawio!!
Ni kama vile hisa za sigara na tbl zinavyogombaniwa sokoni, adimu sana kumkuta mtu anauza hisa za Tcc au Tbl.
 
Hisa kutokuuzwa ni dalili kuwa kampuni husika inafanya vizuri kwenye boashara zake , wenye hisa wanaridhika na gawio!!
Ni kama vile hisa za sigara na tbl zinavyogombaniwa sokoni, adimu sana kumkuta mtu anauza hisa za Tcc au Tbl.
Hapo pote ulipo ongea ni sawa....ila hisa za tcc na tbl sio adimu kiasi hicho zinauzika sana sema tu bei yake ni kubwa sana watu wanashindwa kununua.

Mfano ni wauzaji wa hisa za tcc=14k hadi 15k wakati tbl=7k hadi 8k kwa hisa moja tu na hakuna wanunuzi.
 
Ni kweli kuwa sasa hivi bei ni hiyo uliyoitaja, ila ukiangalia pale kwenye section ya "sell" haina wauzaji, watu hawauzi ndio maana hiki kipindi imekuwa ngumu sana kuzipata hisa hizi sokoni.
wanasubili bei ipande?
 
wanasubili bei ipande?
Ninavyohisi, kutokana na performance ya hisa za crdb zimekuwa na matokeo mazuri sana sokoni kuanzia kwenye faida hasa kwa report za Q1 na Q2, so wanauhakika wa gawio kubwa ambapo inapelekea pia bei yake sokoni kupanda zaidi kwa hiyo ndio maana watu wanazi hold wanaamini kuna future nzuri zaidi sokoni.

The same scenario ina apply kwa NMB.
 
Back
Top Bottom