Wi-Fi mbadala wa vifurushi vya mitandao

Wi-Fi mbadala wa vifurushi vya mitandao

LUBEDE

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2013
Posts
4,322
Reaction score
6,700
wakuu msaada tafadhali,baada ya hii mitandao kutufanya wateja wake kichwa cha mwendawazimu,hivi hakuna njia inaweza kufanikisha hili suala la Wi-Fi majumbani mwetu au mtaani,gharama zake huwa zipoje kama linawezekanika ili nijiunge kwa ajili ya familia yangu na baadhi ya jamaa zangu mtaani,kwa mwenye ujuzi au uelewa wa hili anisaidie nnachotakiwa kukifanya ili nifanikishe hili,kuna mdau aliniambia niwacheki TTCL,ndio manguli wa internet supply kwa hapa nchini,naombeni muongozo ili mimi nijitoe muhanga,watu wanayaogopa haya mambo sababu ya kutokuwa na elimu nayo,ila inawezekana ikawa ni msaada kwa wengi wetu,dunia inabadirika,tubadirikeni nayo...
 
Nadhani huduma hii wanaitoa TTCL kwa gharama nafuu ktk baadhi ya maeneo.

Jaribu kuwaona mawakala wao ktk eneo unaloishi au jirani kwa ufafanuzi zaidi.
 
mkuu wala usiilaumu mitandao ya simu wao hawahusiki na sio lazima wao kutoa hio broadband ya majumbani,

kama unaweza kutoa kuanzia 70,000 kwa mwezi na unaishi mikoa mikubwa kama Dar, Arusha na Mwanza cheki smile wana unlimited bundles ambazo zina dedicated speed kunzia 2mbps, 6mbps na 21mbps. pia smart wanayo unlimited ila sifahamu speed ipoje.

Mpeto Unlimited – Smile – Now you can

pia kama upo nje ya dar smart wana vifurushi unlimited vya mwezi kwa 20,000 tu
 
Kwa uelewa wangu mdogo ni kwamba utahitaji router ambayo nayo itahitaji bandle ili upate net, sasa hapo angalia mtandao gani una nafuu ya bandle....uende ofisin kwao wakupe router... kama ukipata router ambayo si mtandao mmoja itakua njema zaidi
 
Hapo asiye na hela anachukua unlimited ya mwezi mzima ya 70,000 alafu anagawa hiyo bei pasu na jirani moja au wawili. Ni kununua router tu na cable ya kufika kwa jirani, au kumrushia kwa wifi extender. Ukiwa nje ya nyumba unatumia bundle za jero tu za kawaida maana huna matumizi makubwa, ukirudi nyumbani ni full kustream large files kwenye computer bila mawazo. Tatizo linakuja controller ni moja, umeme ukizima kwake au mtu akachezea cable wengine wote wanakosa net na am not sure kama ni legal kwa terms zao.
 
Back
Top Bottom