Why Catholic seminaries excel in exams

Discipline na committment ya wanafunzi as kuna kitu wanaita below 50 unatimuliwa ie 50% ndo passmark.
Alafu sio seminary zote zina preparatory sem kama ile ST Marry ya visiga hakuna prepa ata ile ya Uru haina preparatory as uko kote nilipitia nyakati tofauti.
Also Malazi na malezi bora ndo msingi wa mafanikio pia
 
Kufeli darasa la saba hakumaanishi mtu si mzuri katika masomo. Kuna factors nyingi zinazochangia mtu kufeli au kufaulu baadhi zikiwa juhudi za kujisomea na kujifunza, uzembe, walimu wabaya, uwezo wa kifedha n.k.

Sio seminary zote zina pre-form one. Kwa experience yangu na uelewa wangu kuna seminary zifuatazo ambazo hazina pre-seminary,mfano maua seminary,uru seminary,st.james, na zinginezo ila zinafanya vizuri sana. Mdogo wangu alifaulu darasa la saba na akachaguliwa kwenda kwenye secondary ya kawaida,day school,akapiga chini tukampeleka semenary akawa kwenye first five kila term na results zake za form four na six zilikua safi sana.
Nakubaliana na wanaosema kwamba kufeli darasa la saba sio kigezo cha ukipanga/ukilaza wa mtu.


Mazee naona hamjanielewa.
1)Nilikuwa najibu post ya ndugu aliyesema kuwa seminari za RC wanachukua vipanga tu.Ndiyo nikasema siyo kweli kwa kuwa binafsi kaka zangu wote walisomea seminarini japokuwa hawakufaulu darasa la 7(as tunavyo assume kwamba wasiofaulu hawana akili) na wote walifanya vizuri sana seminarini RC na waliitwa kwenye upadri wakakataa,wakaamua kwenda chuo kikuu.
2)Mwenyewe pia nilikuwa mtumishi wa misa katoliki na nilikuwa kipanga sana kwenye mambo ya dini na nilifaulu mtihani wa seminari.Kwavile nilifaulu pia mtihani wa serikali,madingi wakaaamua niende serikalini na siyo wote tusomee seminarini wakitegemea labda kaka zangu wangeenda upadri.
3)Kama mnasema kufaulu darasa la saba si kigezo cha akili ya mwanafunzi(partly nakubaliana nanyi),sasa si mseme tu kufaulu katika level yoyote ile ya shule siyo kigezo cha ukipanga,yaani iwe darasa la sana,olevel au high school au hata chuo kikuu.Kwanini darasa la saba tu?
 
mazingira ya shule na nidhamu ya kujifunza unatakiwa kufanya nini inawafanya wanafunzi wawe makini katika matumizi ya muda wao. Kwanini washindwe kufanikiwa?
 
Nadhani hapa cha muhimu ni kujifunza wakatoliki wamewezaje?

Personally, nimesomea shule ya misheni tena kijijini kabisa. So I have lived this experience. Ukweli ni kwamba shule za misheni hazichukua best achievers as people want us to believe. Mfano mimi shule yangu, tuliokuwa pale tulienda baada ya kukosa nafasi ya serikali (mwaka wangu darasa la saba walifaulu watano katika wanafunzi kama 80!). Sema tulikuwa tunafanya mtihani wao....(na kwa vile nilikuwa mtumikiaji kanisani..... ilinisaidia). Naturally wengine tusingekuwa na shule za misheni ni kwamba tungekuwa condemned kuwa wakulima forever.

Nilichojifunza nilipofika pale, kwa kweli nadhani ndo imekuwa silaha yangu katika maisha yangu yote mpaka leo baada ya kumaliza University. Tulikuwa tunasoma kwa bidii, tunasali kwa bidii na usisahahu tulikuwa na mashamba makubwa sana ya mahindi na maharage, ng`ombe, mbuzi, kuku nk! YAANI NAKUMBUKA watoto wa wakubwa wengi waliozoea maisha ya mjini "walihamishwa na wazazi wao" maana wengi walikuw hawawezi kulima wala kuchunga ng`ombe! Tuliovumilia mpaka tukamaliza shule tulikuwa wachache sana. Na tulikuwa watoto wa wakulima ambao tulikuwa hatuna alternative ya kuhama. In all, mpaka leo RC nawaheshimu sana, si kwa sababu walinipa elimu ambayo imetokea kubadilisha maisha yangu forever, lakini kwa sababu walinifundisha maisha ni kitu gani.

Kuna mtu kaongelea kuhusu vyakula. Guess what? Tulikuwa tunakula vizuri sana shuleni kwetu lakini almost kila aina ya chakula ilikuwa ni nguvu zetu. Mfano maziwa, walikuwa ni ng`ombe wetu, mayai, maharage, spinachi, kabeji, mahindi, nyama (kitimoto) nk. Tulikuwa tunanunua mchele tuu. Sasa hebu niambieni ni shule gani ya umma au kwingineko wanamlea mwanafunzi katika mazingira magumu kama yale? Na bado here we are proudly representing our schools?

In all, I will be forever greatful to RC for a wonderful opportunity they gave me. Kama ulisoma kijijini ukafika mjini kwa juhudi zako (kuja kusoma UD au kwingineko) you know what Iam talking about here.
 
Tusisahau pia kuwa walimu wa shule hizi pia wanajituma sana. Wanajali muda wa kazi , wanajiandaa vizuri na kufundisha kwa moyo bila kubakiza material ya tuisheni. Hakuna uzembe katika ufundishaji katika shule hizi.
 
3)Kama mnasema kufaulu darasa la saba si kigezo cha akili ya mwanafunzi(partly nakubaliana nanyi),sasa si mseme tu kufaulu katika level yoyote ile ya shule siyo kigezo cha ukipanga,yaani iwe darasa la sana,olevel au high school au hata chuo kikuu.Kwanini darasa la saba tu?

Kama unaijua historia ya Colin Powell utajua kuwa hakuwa mwanafunzi mzuri darasani. Nadhani kwa kuangalia matokeo yake shuleni utakubali (hata yeye mwenyewe anakubali) alifeli. Na hapa nazungumzia college. Kwa mujibu wa Wikipedia, "He graduated with a Bachelor of Science degree in geology from the City College of New York in 1958, attaining a C average, according to his 2006 graduation address at Marymount University."Sasa baada ya Colin Powell kushika nyadhifa zote hizo ktk serikali ya Marekani bado utasema ni mtupu kwa vile hakupata A?
 
wengi wa wachangiaji hapa mmesoma seminari za 1970's-1980's.

facts:-

1.idadi ya shule ukijumlisha na hizo seminary zimeongezeka kwa kasi ya ajabu.sasa hivi shule nyingi za seminari zimekaa kibiashara-sio kumfaidisha mtoto wa mkulima.shule za seminari zilizobakia at least zile za kanda ya ziwa,may be hizi za huku pwani usanii tu.

fact check:-
kuna watoto wa wakulima wangapi marian?!mmeshawahi kwenda graduation pale?mkaona wale wazazi?

2.mchango wa seminari TZ,Africa unaheshimiwa sana kwani walitoa wanafunzi waliokuwa hawana means nyingine ya kupata elimu na kuwapa elimu hiyo.

fact check:-

kwa kuweka hii system ya ku-interview wanafunzi 2000 na kuchagua 30 wanaenzi malengo ya shule hizo?

fact check?

kuna aliyewahi kwenda Lushoto wakati wa interviews za kifungilo,mazinde etc?kale kamji huwa kana-jam!maelfu ya wazazi wanafurika kule.


my point,asilimia kubwa ya seminari tunazoziona top ten hasahasa zile za girls tupu,sidhani kama zina calibre moja na shule kama nyegezi,maua etc.

i will respect the later,kutokana na mchango wao wa kuturn ordinary joes into productive members of the society.

sio huu mtindo wa kina FEZA wa survival for fittest.
 
Kama unaijua historia ya Colin Powell utajua kuwa hakuwa mwanafunzi mzuri darasani. Nadhani kwa kuangalia matokeo yake shuleni utakubali (hata yeye mwenyewe anakubali) alifeli. Na hapa nazungumzia college. Kwa mujibu wa Wikipedia, "He graduated with a Bachelor of Science degree in geology from the City College of New York in 1958, attaining a C average, according to his 2006 graduation address at Marymount University."Sasa baada ya Colin Powell kushika nyadhifa zote hizo ktk serikali ya Marekani bado utasema ni mtupu kwa vile hakupata A?


Kimsingi Omega nakubaliana na hoja yako ya mwanzo.Nilitaka tu uhitimishe kuwa kufaulu mitihani kisiwe kigezo pekee cha kusema fulani ana akili nyingi na mwingine kidogo au hana.
Nina mifano ya kiuzoefu tangia shule ya msingi,olevel,high school mpaka chuo.Kuna washkaji nilikuwa nao walikuwa wakali sana darasani lakini hawakufaulu na wengine hawakuwa wakali kivile lakini walifaulu.Jamaa mmoja nilikuwa nae high school alikuwa mzuri mno katika Biology na siyo siri alifikia hata kunifundisha Biology.Sometimes discussion nae nilikuwa naogopa kwenda manake jamaa alikuwa anashusha vitu vingi mno halafu mimi bado sijavimeza na mtihani wa taifa ndiyo unakaribia!
Lakini jamaa akaja kuchemsha vibaya sana kwenye necta akapiga E kwenye Biology na Physics na F ya Chemistry na kila mtu aliyemjua hakuamini.
Kwahiyo nakubaliana nawe japo si moja kwa moja manake wengine alama zao za mitihani zina reflect kweli uwezo wao wa kiakili.
 
Wana excel kwasababu wanaiba mitihani ya Taifa

Wana collude na officials kwenye MOE ambao ni loyal kwa mapadre wao

Mitihani mingi ya Taifa inasahihishwa kweny kumbi za kanisa katoliki badala ya majengo ya serikali! wanainfluence the whole process

Hakuna cha ajabu kwenye hilo ni ufisadi kwa kwenda mbele..
 
Tusisahau pia kuwa walimu wa shule hizi pia wanajituma sana. Wanajali muda wa kazi , wanajiandaa vizuri na kufundisha kwa moyo bila kubakiza material ya tuisheni. Hakuna uzembe katika ufundishaji katika shule hizi.

Hakuna kitu ni wanajituma kuiba mitihani sana
 
sio seminari tu kwa ujumla shule za kanisa hata zenye wanafuzi zaidi ya 100 wanaofanya mitihani zinaongoza..mfano shule ya st marian imeanzishwa na cardinal pengo mwenyewe ,maria goretti,st fransis...[mbeya-kila mwaka ina feuture top ten]...na hata watoto wanaoongoza wanatoka huko.....

mimi nimepita seminari kwa muda...Malezi na sala yamepewa kipaumbele...utaratibu ni huo kwa shule zote za kanisa hasa katoliki....pia hawafanyi elimu biashara...hawachukui wanafunzi wengi kupita uwezo ..mfano kama wamekubali ratio kwa darasa ni wanafunzi 30 ..basi hata uwape pesa hawatampokea mtoto...

mfano nidhamu ya muda ninayoikumbuka kwa kipindi nilichokaa seminari ni kama hii..

kuamka-saa 11 asuibuhi kila siku
11;30 Mazoezi binafsi[lazima]
12;00-30-KUSALI IBADA FUPI KANISANI[kingereza,kiswahili,kilatini]
12:30-kazi za mikono
7:00 kujiandaa
7:20 kifungua kinywa
8:00 -darasani
10:00 -chai na karanga[bites] au kavu
10:30-darasani
12:00 kusali
12:15-darasani
13;00-CHAKULA
14:00-KULALA
15:00-DARASANI
16:30-CHAI/BISKUTI au any bite au kavu.
16:45-kazi za mikono
17:20-michezo na mazoezi ya viungo
18:30-usafi binafsi
19:00 - chakula
19:40-ibada
20:20- kujisomea
22:30-KULALA [WOTE]
23;00-TAA ZOTE KUZIMWA

utagundua kuwa mtu yeyote aliyepita hizi shule anaishi kwa ratiba...kila kitu kinatengewa muda mdogo ili kila kitu kifanyike kwa makini.....hata kama ni wakati wa mitihani ratiba ni ileile...tabia ya kukesha kusoma kule hamna..they call that poor time management.....ule msemo wa wakati wa mtihani kuwa 'ngombe hanenepi siku ya shughuli ..umeanzia kwenye hizi shule"" wao wanahitaji masaa mawili tu ya maandalizi binafsi usiku.....kwani maandalizi ya mtihani wa form four wao huyafanya kwa miaka minne...hawahitaji kuhangaika siku ya mwisho.....au kidato cha sita wanapoingia tu wanajiandaa kwa mtihani wa mwisho!

hizi shule za kanisa zitaendelea kutesa ..kama tunapenda tunaweza kuiga ya macheche!

Hakuna muda wa kusubiri daladala !!


wewe nawe, sijui umetumwa! How can more than 10 schools kuweza kuiba mitihani na wanafunzi wake wote kuwa consistent kupasua pepa...

Huyo Tumaini anatania tu! anyway atafanya mabadiliko shule za kiislam zifanye vizuri



Ila tabia ya kuchuja wanafunzi to be honest sio nzuri, maana yake walimu sio wazuri. mwalimu mzuri ni yule unayemfundisha asiyejua ajue!!!

so bado ninapeleleza kabla ya kuwapa sifa, I doubt
 
Pia kuna suala moja muhimu sana ambalo watu hawalizingatii ktk suala la elimu. Seminarini watoto wanakula misosi mizuri sana. Mdogo wangu ananieleza jinsi wanavyokula: maziwa,mayai,kitimoto(nyama),matunda etc ambavyo shule zetu za kawaida havipo hivyo. Mtoto hajala unamfundisha problems ktk linear programming ataelewa? Baada ya shule watoto ktk shule zetu za kawaida hawaeleweki wanafanya nini, ndipo wengine wanaenda kujihusisha na ulevi,uzururaji etc. Seminary mtoto anafuatiliwa hata wakati wa kulala wanahakikisha wote wamelala kwenye vitanda vyao. Nawapa big up RC kwa malezi bora ambayo matokeo yake wote twayaona.



Plus excessive prayers
 
Kufeli darasa la saba hakumaanishi mtu si mzuri katika masomo. Kuna factors nyingi zinazochangia mtu kufeli au kufaulu baadhi zikiwa juhudi za kujisomea na kujifunza, uzembe, walimu wabaya, uwezo wa kifedha n.k.


omega pamoja na yote uliyotaja ni sawa yanachangia ila mwenzangu na jinsi mtoto anavyojituma.wengine wanajifanya wapo updated akifika shule km ni hostel anajifanya hajui kilichompeleke matokeo yake anatuletea yai.
 
Wana excel kwasababu wanaiba mitihani ya Taifa

Wana collude na officials kwenye MOE ambao ni loyal kwa mapadre wao

Mitihani mingi ya Taifa inasahihishwa kweny kumbi za kanisa katoliki badala ya majengo ya serikali! wanainfluence the whole process

Hakuna cha ajabu kwenye hilo ni ufisadi kwa kwenda mbele..

Wewe, elimu dunia muhimu pia! Kukuelewesha wewe it might take a century,bado unaamini nguvu za giza za kuiba mtihani?Seminarini kuzuri jamani, watu kama hawa una ignore tu basi!!
 
Wana excel kwasababu wanaiba mitihani ya Taifa

Wana collude na officials kwenye MOE ambao ni loyal kwa mapadre wao

Mitihani mingi ya Taifa inasahihishwa kweny kumbi za kanisa katoliki badala ya majengo ya serikali! wanainfluence the whole process

Hakuna cha ajabu kwenye hilo ni ufisadi kwa kwenda mbele..
Kwakuwa wizi wa mitihani ni uvunjaji wa sheria tunaomba evidence ama la uzipeleke kwenye vyombo vya sheria ili sheria ichukue mkondo wake.Vinginevyo naweza kuhisi utakuwa ni wivu tu kwanini wale na sio mimi, kwanini dini ile na siyo dini yangu! Lengo hapa ni kujifunza. Kama kuna mazuri tunaweza kujifunza toka seminary ili na shule nyingine nazo zikafanya vizuri kuna matatizo gani?
Ila baadhi kama kawaida tunaangalia kila kitu kwa line za kidini!
 
Nadhani hapa cha muhimu ni kujifunza wakatoliki wamewezaje?

Personally, nimesomea shule ya misheni tena kijijini kabisa. So I have lived this experience. Ukweli ni kwamba shule za misheni hazichukua best achievers as people want us to believe.

Infact hata wana JF wengi hapa ni X Seminarians. Nami Pia.

Personally I always thank the seminary I studied for 6 years. Life was wonderful and in deed very challenging. Every minute is programmed for either, prayer , studies, work, or sports. And now I am happy, because I do the same and my life is not like any other . You know what I mean?

Wanafunzi wanaofeli mitihani wanarudishwa mwaka au wanafukuzwa kuendana na seminary husika. Hili sio geni kwa system ya academics. Hata ungesoma masters ukashindwa kupata mark za kutosha kufikia kiwango kilichowekwa cha kupasi huwezi kupewa tu .

Tatizo la kibongo ni kubebena hata wale wasiojiweza kabisa. Madesa vyuoni, upendeleo wa marks etc then tunakuja kupata mavihiyo kibao kweye system.

By the way kati ya shule 10 bora mwaka 2009 shule 5 zinatoka kilimanjaro na 2 pwani. Na zote zina backround ya misioni.
 
Pia ni kwakuwa wana MUNGU wa kweli..teh teh teh..natania tu jamani!

Sio utani mtu wangu, like it or not, kuwa na uhusiano wa karibu na Mungu unasaidia sana tu. Mimi nimesoma shule ya kikatoliki (sio seminari) na kusali ilikuwa ni lazima kiasi kwamba you grow to enjoy it. Na whether you agree or not, ni one of the factors zinazoset shule hizi apart.

I would also like to disagree a bit with a comment made earlier. Wanafunzi wanaoenda shule hizi za kikatoliki au seminari sio special in any way. I believe mwanafunzi yeyote anaweza akafanya vizuri akilelewa na akafuata sheira katika mazingira ya shule hizi. Ndio maana wapo wanaoshindwa na wanaacha shule na wale wanaobaki na kufuata sheria na mienendo inayokuwa encouraged na shule hizi wanafaulu vizuri.

Kama shule zetu za serikali zingekuwa na madarasa yenye wanafunzi wasiozidi arobaini tuseme, wana maktaba zenye vitabu vyote vinavyotakiwa, wana maabara zenye vifaa vya kutosha, wana walimu wanaojali mwanafunzi asipofanya homework kwa mfano na ambao wanalipwa vizuri kiasi kwamba wanapenda fani zao na wako tayari kujitolea muda wao kufundisha wanafunzi hata iwe usiku au wikiendi. Shule hizi zingekuwa na ratiba ya kusoma inayoeleweka isiyokuwa interrupted na mambo kama ukosefu wa chakula uliosababisha shule zifungwe au sijui matatizo gani, ratiba isiyoruhusu muda wa idleness, kila kitu kiko systematic. Mi nafikiri shule hizi zingefaulu way more than zinavyofanya sasa hivi.

Lakini, we all know, condition ya shule za serikali tena hasa za kata ni the total opposite of what I have just described. This is a problem that will take a while to fix especially considering that ni shule hizi za serkali zinazoaccomodate maelfu ya wanafunzi throughout our country. Ila kama serikali yetu ikiwa na nia ya ukweli ya kuendeleza quality ya elimu yetu then our future could be brighter!

By the way, a point of correction, sijui kwa nini watu wana hii idea kwamba shule za kikatoliki zina chakula kizuri. Trust me when I say, they don't. Shule yetu tumelishwa ugali wa dona kwa maharage yaliyochemshwa mondays through fridays. Nyama ilikuwa mara mbili kwa mwezi, na wali maharage unapikwa huku maharage yanachanganywa na cabbage humo humo, chai ya maziwa tulikuwa tunapata mara moja kwa wiki tena maziwa ya unga. Kaka yangu kasoma seminari na siku wakila kitimoto (ambao wanafuga wao wenyewe seminarini) unaona nyama na nyanya zikielea kwenye maji hadi unaweza kubadilisha mawazo ya kula...and the list goes on. Au labda waliokuwa wanacomment, mlikuwa mnalinganisha chakula hiki na cha wapi?
 
Wana excel kwasababu wanaiba mitihani ya Taifa

Wana collude na officials kwenye MOE ambao ni loyal kwa mapadre wao

Mitihani mingi ya Taifa inasahihishwa kweny kumbi za kanisa katoliki badala ya majengo ya serikali! wanainfluence the whole process

Hakuna cha ajabu kwenye hilo ni ufisadi kwa kwenda mbele..

wewe na wenzio mkaliage hayo hayo wenzenu wansonga mbele. Hivi ile islamic seminary vipi mwaka huu??
 
Back
Top Bottom