Who will bring Kagame to Justice????

Kagame anamalizia muhula wake wa mwisho.Na amesema hagombei tena kama katiba isivyoruhusu.Mbona tunapenda stori za kuungaunga?
Kwani na Mseven alikuwa hajamaliza muda wake mbona aligombea tena, mambo ya siasa ni magumu na wala usiusemee moyo wa mwenzio
 
Zawadi ya Kagame kwa rafiki yake wa tokea utotoni alimchagulia kifo, hakuna mtu asiejua kuwa Kagame ndo aliemuua Fred Rwigema period check hii site then you will get the whole saga http://www.africaglobalvillage.com/africanews/central-africa/rwanda/1281-un-answered-questions-about-the-death-of-gen-fred-rwigema.html
 
Kwani na Mseven alikuwa hajamaliza muda wake mbona aligombea tena, mambo ya siasa ni magumu na wala usiusemee moyo wa mwenzio
Hivi sisi tuna ugonjwa gani? Katiba ya Uganda haina term limitation...hakuna kikomo tofauti na katiba ya Rwanda.Bahati unajifunga mwenyewe kwa kusema kuwa tusiusemee moyo,mbona nyie mnausemea moyo wake kuwa hatatoka mpaka 2024?Nimemnukuu mwenyewe anavyodai,sijaongezea wala kupunguza kitu.Kagame si Museveni na kwa mtu aliyefuatilia uchaguzi wa Rwanda uliopita tayari anaujua ukweli wa ahadi hii.
 

Acha kupotosha uma on sasa umeamua kumkingia kifua Kagame wazi wazi ndugu yangu soma mwenyewe na pia soma site aliyoipost Bornagain muda si mrefu ndo utajua kazi ya Kagame sasa It was Kagame Not Museveni who Killed Fred Rwegyema | Ugandans-At-Heart
 
Acha kupotosha uma on sasa umeamua kumkingia kifua Kagame wazi wazi ndugu yangu soma mwenyewe na pia soma site aliyoipost Bornagain muda si mrefu ndo utajua kazi ya Kagame sasa It was Kagame Not Museveni who Killed Fred Rwegyema | Ugandans-At-Heart
Sioni evidence yoyote zaidi ya uzushi tu katika article hii.Jamaa anasema hivi mara vile bila kuelezea tukio au motive yoyote.Kagame wakati alikuwa masomoni Marekani na hakuwa kiongozi mkuu sasa iweje alimuua Fred?Kumbuka Kagame alikataa kushambulia Rwanda wakati kikosi kikiwa bado dhaifu na hata ukiangalia utagundua alikuwa sawa kwani kikosi kilichoongozwa na Fred wengi wao walifia mikononi mwa majeshi ya serikali huo mwaka 1990 ikamchukua Kagame takribani miaka minne kuikomboa Rwanda,1994...twende kwa factual history and logical reasoning sio kumeza udaku tu.
 
kwani mara ngapi uchaguzi ukikaribia anawatafutia tuhuma wapinzani wake,acha upenzi wewe
 
Fred rwigema ndio hero wa Rwanda, kagame alidandia tu treni kwa mbele.

...wewe upo bado na propaganda zako za ant kagame? Rwanda is doing fine under Kagame and economy is growing faster than average,rudi kwenu kigali lakini kama na genocide lazima wakuweke kwenye trial ila utapewa lawyer wa kukutetea na watasikiliza kesi yako kwa haki kuna rule of law sasa sio kama zamani
 

...Hivi hizi garbage mnatoa wapi?huna idea na ulichoandika na hujui Rwanda/genocide history,is just waste of time to debate na mtu kama wewe, ila one thing Rwanda is doing fine & very peacefully na kuna watanzania wengi sana wako huko wanafanya professional jobs with good pay.
 

Sasa kwa nini akubaki huko huko Merikani na kuendela na masomo yake, kwa nini alirudi kuongoza jeshi ambalo alikuwa anajuwa halina uwezo 4 the time being, kisaikolojia naona unamlahumu FRED karibu kwa kila jambo kuanzia:Kufanya vitu kwa papala, kutokuwa level headed and what have you!! Eti jaribio lake la kwanza lili shindwa na majeshi ya Serikali, mbona hilo ni jambo la kawaida kwenye medani za vita mbona Castro Fidel alishindwa katika jaribio lake la kwanza, alikuja kufanikiwa mara ya pili alipo shirikiana na Comrade Che Guaverra - why pick on FRED(R.I.P) if I may ask?

Umemsema sema sana FRED kwani aliwahi kukukwaza nini katika maisha yako, hutaki kabisa watu watoe maoni yao ambayo hayarandani na ya kwako, actually unaonekana ni wewe peke yako (lone Ranger) mwenye kumjuwa vizuri FRED like back of your HAND sijuhi kama kuna ukweli wowote katika hilo!! - kwa nini wewe ujione ndio mwenye factual history na a MEGA SMART reasoning capacity wengine vichwa vyao viko kwenye vegetative state, oh yes watu wengine wasizungumze chochote kuhusu Rwanda kwa kuwa wewe ni Encyclopaedia RWANDANICA.

Nimejaribu kuangalia kwa umakini majibu jibu yako, nikisema na wewe huko kwenye group ya wale wenye tabia ya kukumbusha watu kwa kutamka unnecessarily kwamba: "UJUHI MIMI MTUTSI" je, nikikuweka kwenye kundi lenye trait kama hiyo ntakuwa nimekosea?

Eti watu wanameza udaku, yaani unataka kutwambia information zako zinatoka kwenye respectable source, au mwenzetu uliwahi kuwa platoon commander au Brigedia wa jeshi la RPF - wacha kudhalau watu bwana - hapa kila mwana JF ana uhuru wa kutoa maoni yake bila ya kuomba kibali kutoka kwa any SOUL. CHEERS.
 

The story of Rwandan Genocide is more than what media made us to believe. For a long time it has been one-sided, but recent appeal cases concluded at the ICTR in Arusha shaded lots of light. Ukiangalia wote wale waliokuwa kwenye Military Trial I wamefutiwa mashtaka mengi na hata adhabu zao kupunguzwa. Kitu kimoja kikubwa kuliko vyote ni conclusion ya appeal chamber kuwa MAUAJI HAYAKUPANGWA. Appeal chamber pia ilisemea juu ya zile radio za uchochezi za wahutu na kusema zile zilikuwa ni propaganda radio ambayo pia hata RPF walikuwa nayo. Kinachokubalika kuliko vyote ni kuwa yeyote aliyehusika na kuanzisha vita April 6 1994 ndiye anawajibika na mauaji yaliyofuatia.
 
I will just ignore your other nonsense and dwell on the topic.Unauliza kwamba kwa nini Kagame hakubaki Marekani,nahisi aidha haujui kilichompeleka Marekani au you are too emotional to the extent of losing...kifupi Kagame ilibidi arudi kuweka hali sawa maana baada ya kuawawa kwa Kiongozi Fred morali ya wanajeshi wa RPF ilikuwa chini sana.RPF ilikuwa imeshindwa na walikuwa almost wa-give up kabisa so they needed someone to lead them in re-assembling themselves.That's what Kagame did.Na hapo juu nimeandika kuwa ilimchukua almost miaka minne kuipanga RPF hadi kuwa imara.Simtetei Kagame wala simpuuzi Fred kwa sababu sifaidiki na lolote kutoka kwao.Kuna tofauti kubwa kati ya mtu wa combat na mtu intelligence na nikatoa analogue ya Che Guevarra na Fidel Castro. Kuna watu mpaka leo wanaamini Castro alimuua Che Guevarra...huo ndio uzushi naopinga.
 
Tutaongea sana kuhusu Kagame,mtaongea sana kuhusu uzushi ilhali akizidi kuivusha Rwanda.In ten years time Rwanda watakuwa na sekta kubwa ya huduma kuliko sisi ambao tumekalia kusema kilimo kwanza na madini.Historia inaonesha nchi zilizoendelea na kuendelea zinaimairisha sekta ya utoaji huduma.Kagame has the ball squarely on his feet dribbling towards developing Rwanda so we expect more and more attack geared at him. Historia inaonesha kuwa hakuna Mtu mweusi aliyeonesha rekodi ya maendeleo na kusifiwa na hizo BBC na CNN na serikali zao.
 
What justice? Gacaca justice or some alien justice to the Rwandese?
 
Kinachokubalika kuliko vyote ni kuwa yeyote aliyehusika na kuanzisha vita April 6 1994 ndiye anawajibika na mauaji yaliyofuatia.

Then if that is the case Kagame and the then heads of RPF must go for trial ICTR in Arusha maana ndo walioanzisha vita April 6 1994
 
Then if that is the case Kagame and the then heads of RPF must go for trial ICTR in Arusha maana ndo walioanzisha vita April 6 1994

Hili jambo la 'double genocide' ilitokea Rwanda i.e. wahutu waliua watutsi na watutsi waliua wahutu. ICTR walifungua mashtaka ya upande mmoja kuwaandama wale walioshindwa vita (RGF-Wahutu), lakini hawakufungua mashtaka dhidi ya wale walioshinda vita (RPF-Watutsi). Carla Del Ponte alipojaribu kufungua faili la uchunguzi dhidi ya maafisa wa RPF waliotuhumiwa kwa genocide ya wahutu alifukuzwa ICTR. Kwa maneno yake alisema ikiwa ikifahamika ni nani alitungua ndege ya Habyarimana, basi historia ya Rwanda genocide itaandikwa upya.
 
Nashukuru sana kwa uchambuzi wako, tena kwa upande wangu nasema Watusi wameua Wahutu wengi sana kuliko hata Wahutu walivoua Watusi. Naema hivo maana Wahutu walikufa 1994 kwenye genocide ya Rwanda na mwaka 1997 majeshi ya RPF yakaamua kuwafuata kwenye makambi yao yaliyokuwa Eastern DRC ikawaangamiza vya kutosha. Naungana na wewe tena na tena kwamba siku wakitaja alietungua ndege ya Havyarimana pale Kigali kwenye uwanja wa Kanombe usiku ule wa tarehe 06/04/1994 basi historia ya Rwanda genocide itandikwa upya na dunia itaujua ukweli wote. Waache time is a good teacher
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…