Kasie
Platinum Member
- Dec 29, 2013
- 21,236
- 36,261
Yaani....
Nimekosa raha, tabasamu langu limepotea...
Nilitoka na niliapa kutokulia, ila jana machozi ya kwikwi yalinitoka.
Ni sehemu ya kufatilia namna ya kupata huduma, unauliza natakiwa nifanye nini nafanya vyote halafu naambiwa kesho asubuhi uje huduma yako iko tayari.
Unafika asubuhi unaambiwa subiri, nakuwa mtii nasubiri masaa kadhaa yanapita unaambiwa endelea kusubiri utapata nakuwa mpole nasubiri.
Inafika jioni unakuwa umechoka muda wa kazi umeisha unaona kabisa ulikuwa unadanywa kama danganya toto.....
Inaumaaaa, bora wangeniambia nenda tutakwambia lini uje... hapo siku nzima ushazungushwa panda floo ya 4 chumba na 12 ukifika unaambiwa nenda floo ya 8 kisha unarudishwa chini mapokezi kisha nenda floo ya 3 halafu unaambiwa ngoja usiondoke muda wa wowote huduma yako itakuwa tayari...
Matokeo yake jua linazama wale waliokupiga danadana tangu asubuhi wanabeba mikoba yao wanakwambia eeehh bado upo...!!!?
Hapo hasira imepanda, donge limenikaba kooni nachukua kikapu changu nielekee kituo cha daladala nirudi nyumbani...
Nikashindwa kujizuia, niliangua kilio kikubwa Cheney kwikwi na hasira na jazba hadi nikakaa chini.
Wakatokea walinzi wakaninyanyua bibi polee, jikaze ukilia haisaidii sanasana hapa utajaza watu wakurekodi na kukurusha mitandaoni.
Nikanyanyuka nikajifuta kamasi na mtandio wa dera huyoo nikaondoka polepole.
Najua muda si mrefu nitatabasamu tena na kurejesha furaha yangu, huduma nimeizira maana nikirudi tena ntaudhika tuu.
Al Jumapili Njema.
Nimekosa raha, tabasamu langu limepotea...
Nilitoka na niliapa kutokulia, ila jana machozi ya kwikwi yalinitoka.
Ni sehemu ya kufatilia namna ya kupata huduma, unauliza natakiwa nifanye nini nafanya vyote halafu naambiwa kesho asubuhi uje huduma yako iko tayari.
Unafika asubuhi unaambiwa subiri, nakuwa mtii nasubiri masaa kadhaa yanapita unaambiwa endelea kusubiri utapata nakuwa mpole nasubiri.
Inafika jioni unakuwa umechoka muda wa kazi umeisha unaona kabisa ulikuwa unadanywa kama danganya toto.....
Inaumaaaa, bora wangeniambia nenda tutakwambia lini uje... hapo siku nzima ushazungushwa panda floo ya 4 chumba na 12 ukifika unaambiwa nenda floo ya 8 kisha unarudishwa chini mapokezi kisha nenda floo ya 3 halafu unaambiwa ngoja usiondoke muda wa wowote huduma yako itakuwa tayari...
Matokeo yake jua linazama wale waliokupiga danadana tangu asubuhi wanabeba mikoba yao wanakwambia eeehh bado upo...!!!?
Hapo hasira imepanda, donge limenikaba kooni nachukua kikapu changu nielekee kituo cha daladala nirudi nyumbani...
Nikashindwa kujizuia, niliangua kilio kikubwa Cheney kwikwi na hasira na jazba hadi nikakaa chini.
Wakatokea walinzi wakaninyanyua bibi polee, jikaze ukilia haisaidii sanasana hapa utajaza watu wakurekodi na kukurusha mitandaoni.
Nikanyanyuka nikajifuta kamasi na mtandio wa dera huyoo nikaondoka polepole.
Najua muda si mrefu nitatabasamu tena na kurejesha furaha yangu, huduma nimeizira maana nikirudi tena ntaudhika tuu.
Al Jumapili Njema.