#WhatWouldMagufuliDo: Upepo wa Rais wa Bongo wavuma Ughaibuni

#WhatWouldMagufuliDo: Upepo wa Rais wa Bongo wavuma Ughaibuni

International recognition inakuja namna hiyo, kwa kufanya kazi kwa bidii. Sasa Mkwere alijua inakuja kwa safari za nje
 
watanzania bwana..yaani ndani ya siku 25 amefanya hayo na unaona serikali iko kazini bila mawaziri..

Kwani kunahitaji siku ngapi ili rais kwa mfano aseme sasa pale kivukoni watu wavuuke bure? kama serikali imeweza kuokoa hizo hela za kifisadi na masherehe yasio na maana hii pia inahitaji awe na baraza la mawaziri?
 
kuna misleading nyingi sana katika taarifa zinazosambazwa nje ya nchi kuhusu kilichofanyika. nimefatilia taarifa nyingi zinapotosha. Sijui ni tatizo la tafsiri.

eti hela za uhuru zitumike hospitalini, mara kuna gazeti linasema zitumike kwenye usafi.

Halafu anapaishwa sana,sijui ni kwa faida ya nani, do they want him to make promises while he is happy?
 
Watu kama hao huwa wapo.Watu ambao kila kitu ni kukosoa tu,hata pale ambapo lipo jema.Achana naye.
Mkuu we labda utakuwa hujaisoma. Hiyo habari imeandikwa Australia na imemuelezea Magufuli kwa kulinganisha mbinu zake za kubana matumizi na namna gani waziri mkuu wa Australia anaweza kujifunza hapo. Sasa sijui una maana gani kumkosoa mtoa mada akati yupo sahihi.

Unless labda unataka kutuambia Australia sio ughaibuni?

Halafu nimeona unamkosoa sana Rais kwa vitu ambavyo ni facts hiyo sio nzuri hata kidogo. Utakuwa unajiumiza roho bure kumchukia Magufuli akati kwa kipindi kifupi ameonesha ana nia kweli ya kututoa hatua moja kwenda nyingine.

#growupman
 
Zanzibar crisis what would Magufuli do? Zaidi ya mwezi amefumba macho.
 
That's true imefika wakati tuweke tofaut zetu pemben tusmame kama watanzania, na kujiskia vzur kwa kile kinacho fanywa na Pr. Wetu JPM
 
Zanzibar crisis what would Magufuli do? Zaidi ya mwezi amefumba macho.

Mambo ya Zanzibar yataamuriwa na Wazanzibar wenyewe hasa kuhusu masuala ya uchaguzi. Tume ya uchaguzi ya Zanzibar haitakiwi kuingiliwa na mtu yeyote au chombo chochote. Hii ni kwa mujibu wa sheria. Sasa ulitaka rais wetu Dkt Magufuli avunje sheria!? Rais hatakiwi kuingilia maamuzi ya ZEC...mkitaka aingilie basi sheria ibadilishwe kwanza...ila hiyo iliyopo inapiga marufuku ZEC kuingiliwa.
 
mimi sijaona bado jambo lenye tija tokea kuapishwa kwa magufuli, haya mambo aliyofanya yote fedha zitaingia serikalini hatujui badae zitaishia wapi lakini vipi magufuli angeweza kuleta change ambayo mwananchi mmoja mmoja atafaidika kama:-

- tunataka tuone bidhaa kama chakula vinapungua bei
- nauli usafiri wa ndani zinapungua
- ajira tone anatengeneza
- kama ameweza kusave hizo hela pia tuone ameongeza mishara kwa wafanyakaz wa serikali kuanzia kima cha chini Zaidi.
- lakini pia hospitali sio muhimbili tu, kuna watu Tz hawajuwi ospital inaitwa muhimbili
- tuone anatoa matamko urasimu na ubaguzi ondoke watu kwenye ukuomba ajira nk.
- Azalishe ajira sio jana nimesoma ana mpango kupunguza wafanayakazi lakini sasa waende kufanya kazi wapi?
- Hawa watu maskini tija yao nini? au tufurahie tu kuwafukuza makamishna ambao ni mafisadi inatosha?

Mambo hayo ndio mambo ya msingi kwa taifa la Tz kwa muda huu.

attachment.php
 
As long as he is a CCM member do not TRUST him.....!!
 
Mambo ya Zanzibar yataamuriwa na Wazanzibar wenyewe hasa kuhusu masuala ya uchaguzi. Tume ya uchaguzi ya Zanzibar haitakiwi kuingiliwa na mtu yeyote au chombo chochote. Hii ni kwa mujibu wa sheria. Sasa ulitaka rais wetu Dkt Magufuli avunje sheria!? Rais hatakiwi kuingilia maamuzi ya ZEC...mkitaka aingilie basi sheria ibadilishwe kwanza...ila hiyo iliyopo inapiga marufuku ZEC kuingiliwa.

Usaanii mtupu. Magufuli amri jeshi mkuu,Jecha ametangaza kufutwa uchaguzi mikononi mwa jwtz.No easy way out JPM hawezi kukwepa mkwamo wa kisiasa Zanzibar and that's the way it is.
 
As long as he is a CCM member do not TRUST him.....!!

So was Julius Nyerere, so was Willibrod Slaa, so was Sokoine, so was Luwasa, so was Sumaye. Chama cha Mapinduzi ni mpango wa Mungu.
 
Mkuu kwa waandishi gani wa bongo!

Hawawezi kuripoti hili maana lipo nje ya uwezo wao

Jamani mbona magazeti ya bongo hayaripoti hii? inatakiwa yaripoti kila mtu ajue kwamba JPM anavuma mpaka ughaibuni! au wadau mnasemaje?
 
Back
Top Bottom