What's so special with hammer vehicle?

......Mie uzuri wa gari ni umbo, hivyo hummer umbo lake baya silipendi.
 
Msafara wa mamba na kenge wamo inaelekea.
Hummer, Landcruiser na Bugatti wapi na wapi?

SIFA yake kubwa ni lazima uwe na Petrol station nyumbani
hummer-h3 (2).jpg

Aaah, kumbi ni gari la kivita tu tena linalofanana na tractor!!!! Nlilifikiri linazidi haya hapa chini...















bugatti-veyron1-revise.jpg

Nina wasi wasi wa survival ya hawa jamaa wadogo hasa pale bump za kinondoni.
 
Mkuu cc 6000 kama wewe siyo fisadi litatembea kweli? Ni kwa nini mtu utumie gharama kubwa sana kuonesha utofauti wako angali kuna hosptal hazina vitanda na dawa? Mbona kuna watoto wengi tu mtaani wanashindwa kusoma kwa kukosa ada ya kulipia shule? Je, huwezi kugusa Taifa la kesho kwa kusomesha angalau watoto wachache wanaoteseka mtaani? Je, huyu mtoto ukimsomesha akiwa daktari si itakuwa advantage kwa jamii nzima inayotuzunguka? Na kama hiyo gari ni ya kutembelea tu haizalishi chochote, hizo hela haziwezi kununulia gari ya kawaida tu ya kutembelea na hiyo nyingine inayobakia ikawa invested na kutoa ajira zaidi kwa jamii? Mimi nashauri watanzania tufikiri sana kabla ya kufanya decision ya kushindana kwa kununua magari, tushindane kwa kusaidiana kuinua uchumi wetu wenyewe.


Nakushukuru sana kwani umetoa ushauri mzuri mno, pia itakuwa vizuri zaidi ukaaonyesha mfano kwa kuanza wewe kusomesha watoto wa chekechea kwani hao ndio watakaokua madaktari wa kesho.Pia najua uwezo unao sana tu naamini kwa hilo na wengine wataunga mkono katika hilo.Pia si vibaya kuendesha gari ya kifahari kwani wapo wengi tu wanoendesha hayo magari na pia msaada walioutoa kwenye jamii ni kubwa pia.Na si lazima kuwa tajiri ndio uchangie jamii hapo ulipo unayo mengi sana ya kuchangia kwa maendeleo yetu kwa pamoja swala ni kwamba unao moyo wa kusaidia?au unawaza kusaidiwa?.
 
Ni kubwa na linahitaji space kubwa kwa parking. Ukilipeleka Kariakoo watakuibia kila kitu halafu wakuuzie tena kwa kupitia gerezani.
Acha umakinda wako kwani vifaa vya magari huwa vinaibiwa kariakoo tu? mimi niliibiwa site mirror mikocheni, kila sehemu kuna wezi sio kariakoo peke yake
 
Hummer?, thats one cheap semi-luxury powerful SUV! Iko ki-utility zaidi, sema wabongo wakiona Hummer ambazo ziko modified huko US wanapagaaawa! Kama nina pesa za kutupa na nahitaji a luxury SUV, i wouldnt go for a hummer!
 
Ndiyo kuna magari expensive kuliko Hummer, ishu ni kwa mba lilitokea kuwa na ka umaarufu pia pamoja na umbo lake ,tofauti na Bugatti, Lamborghini na mengine expensive ambayo kwa mtu wa kawaida c rahisi ku recognize!
 
Mkuu cc 6000 kama wewe siyo fisadi litatembea kweli? Ni kwa nini mtu utumie gharama kubwa sana kuonesha utofauti wako angali kuna hosptal hazina vitanda na dawa? Mbona kuna watoto wengi tu mtaani wanashindwa kusoma kwa kukosa ada ya kulipia shule? Je, huwezi kugusa Taifa la kesho kwa kusomesha angalau watoto wachache wanaoteseka mtaani? Je, huyu mtoto ukimsomesha akiwa daktari si itakuwa advantage kwa jamii nzima inayotuzunguka? Na kama hiyo gari ni ya kutembelea tu haizalishi chochote, hizo hela haziwezi kununulia gari ya kawaida tu ya kutembelea na hiyo nyingine inayobakia ikawa invested na kutoa ajira zaidi kwa jamii? Mimi nashauri watanzania tufikiri sana kabla ya kufanya decision ya kushindana kwa kununua magari, tushindane kwa kusaidiana kuinua uchumi wetu wenyewe.

Mkuu ndo mana hata mkuu wa nchi anatumia gari amabayo kwa gharama ni almost sawa na hummer je naye haoni mahitaji hayo uloyaorodhesha?
 
Mkuu ndo mana hata mkuu wa nchi anatumia gari amabayo kwa gharama ni almost sawa na hummer je naye haoni mahitaji hayo uloyaorodhesha?

Mkuu kuna uwezekano haoni na kama anaona basii anayapuuza au kutokuyapa vipaumbele,, otherwise hayo mashangingi ya gharama yangekuwa yameuzwa sahivi na hiyo hela kufanyia shughuli za maana na siyo kustarehe wakati asilimia kubwa ya watanzania bado wapo kwenye umaskini wa kupindukia.
 
Back
Top Bottom