WEWE UNGECHUKUA HATUA GANI?

WEWE UNGECHUKUA HATUA GANI?

Maelau

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2011
Posts
1,365
Reaction score
1,343
Wakuu niko nchi fulani huku majuu. Nina rafiki yangu Mnigeria, kanisimulia kwamba rafiki yake alikuwa ameoa mke mzuri tu na wote walikuwa waajiriwa wa serikali. La ajabu ni kwamba, majukumu yote ya nyumba aliachiwa baba tu mfano ( kulipia pango, ada za shule kwa watoto na chakula). Huku nyuma kumbe mke alikuwa akitumia mshahara wake kujenga,na alifanikiwa kujenga nyumba mbili chini ya umiliki wake.
Wakati huo nyumba ya familia iliyokuwa ikijengwa na mumewe haikuweza kukamililkka kwa wakati kwa sababu ya majukumu niliyoyabainisha hapo juu. Sasa kwa kuwa walikuwa wamepanga na baada ya mke kukamilisha ujenzi kisirisiri alimshawishi mmewe wahamie katika nyumba mpya eti aliyoiona inafaa, kwa bei sawa na ile waliyokuwa wamepanga. Kwa kuwa nyumba ilikuwa mpya mmewe akashawishika kuhamia bila kujua kuwa ni nyumba ya mkewe. Na kodi aliendelea kulipa kama kawaida kupitia mwakilishi bandia aliyewekwa na huyo mama. Jamaa alikuja kugundua kuwa nyumba ile ni ya mkewe baada ya miaka minne. Yeye aliamua kumuacha mkewe wakati huohuo. Wewe je ungefanyake? ukichukulia kuwa tayari mna watoto?
 
Ntaendelea kulipa kodi kama kawa kwa mwenye nyumba maana sio yangu pia kuhusu mapenzi simwachi.... tena huyo ndio anafaa sasa
 
Ata mie ningemuacha wala hamna jingine....hilo la watoto si ajabu wala sio wake.....wanawake ni kugegeda tuu. Na alafu ukiingia kwenye ndoa kwa imani kuwa mtasaidiana na mkeo ujue ulishafeli. Mwanamke hela yake ni yake.
 
Hapo mpka kwenye kujenga nyumba kisiri panaweza kusameheka ila kwenye kulipa kodi kwenye nyumba ya mkeo ahaa hapo kumuacha ilibid.
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] changu chetu chako chako tu
 
Najua wale wanaokopesha waume zao kwa riba kwa kupitishia pesa kwa rafiki au ndugu zao.
 
.....Hivi kwann mnawapenda wanawake? Wachafu, wakatili. Wanawake wameharibu maisha ya wanaume wangapi, wangap wamekufa kwa ajili ya wanawake, waliojela kwa ajili ya wanawake. NB sio msiwapende wanawake No. Kaeni nao kwa akili hata maandiko yanasema usipomwani mwanamke wako mfiche siri zako.
 
Mbona hiyo scenario hata Bongo imeshatokea sana tu unakuta mke amejenga bila kumwambia mumewe
 
Mbona hiyo scenario hata Bongo imeshatokea sana tu unakuta mke amejenga bila kumwambia mumewe
Binafsi ningemwambia aandikishe hizo nyumba kwa watoto kama urithi kama anataka tuendelee na Maisha. Picha hapo ni kwamba mmeungana kanisani au kimsikitini tu lakini mwenzako anaishi kivyake hana time na ujenzi wa familia kwa ushirikiano na ukiangalia vizuri utakuta ana mtu mwingine anasubiri kikinuka anaendelea nae kwenye mijengo yake
 
tunaposema mkeo hapaswi hata kujua income yako mnakataa....eti mwili mmoja..... ushaona mke na mumu wanazikwa kaburi moja,,,hata kama walikufa kwa wakati mmoja....hawa wadudu sioo kabisaaaa....
 
Alifanya sahihi kumuacha aisee kujenga sio shida shida ni hiyo siri ya miaka minne
Why amuache? Mimi nitaoa mke na Wala sio mshahara wake, natimiza mjaukumu yote Kama mume Hadi pesa ya chumvi nitatoa na Wala sitomuuliza kuhusu kipato chake labda apende mwenyew
 
Why amuache? Mimi nitaoa mke na Wala sio mshahara wake, natimiza mjaukumu yote Kama mume Hadi pesa ya chumvi nitatoa na Wala sitomuuliza kuhusu kipato chake labda apende mwenyew
Ndo ulipie kodi kwa miaka minne ilhali ni ya mkeo!!


Kila mtu na roho yake mi ikinitokea hata km niko mwanamke mume nammwaga
 
Back
Top Bottom