Wewe ni Graduate? Pitia hapa

Wewe ni Graduate? Pitia hapa

mr.kayembele

Senior Member
Joined
Nov 9, 2012
Posts
118
Reaction score
58
Kuna njia nyingi ambazo kijana aliyemaliza chuo anaweza kuongeza kipato chake. Hapa chini nimeorodhesha baadhi ya njia hizo:

Kuanzisha biashara yako: Unaweza kufikiria kuanzisha biashara yako ya mtandaoni au ya nje ya mtandao. Kujenga biashara inayotumia ujuzi wako wa kielimu au hata ubunifu wako unaweza kuwa fursa nzuri ya kukuza kipato chako.

Kuajiriwa: Unaweza kutafuta kazi katika eneo lako la utaalamu na kuajiriwa na kampuni au shirika. Tafuta kazi inayolingana na utaalamu wako na ambayo inakupa fursa ya kujifunza zaidi na kukuza ujuzi wako.

Kufanya kazi za kujitegemea: Unaweza kujiunga na majukwaa ya kazi za kujitegemea kama vile Upwork, Fiverr, au Freelancer na kutumia ujuzi wako kufanya kazi mbalimbali kwa wateja ulimwenguni.

Kufanya kazi za kujitolea: Unaweza kutumia muda wako wa ziada kufanya kazi za kujitolea katika mashirika ya kijamii au misaada. Hii inakupa fursa ya kuonyesha ujuzi wako na kujenga mtandao wako wa kijamii.

Kuendelea kusoma: Unaweza kuendelea kujifunza na kuongeza ujuzi wako kupitia kozi za mtandaoni au mafunzo. Kupata ujuzi zaidi unaweza kuongeza fursa yako ya kupata kazi bora au hata kuanzisha biashara yako.

Kuwekeza: Unaweza kuwekeza katika biashara au hisa. Hii inaweza kusaidia kuongeza kipato chako kwa muda mrefu, lakini unapaswa kuzingatia hatari za uwekezaji na kufanya uchaguzi wa busara.

Kumbuka, hakuna njia moja sahihi ya kuongeza kipato chako. Unapaswa kuzingatia ujuzi wako, maslahi yako, na rasilimali zako zilizopo ili kupata njia inayofaa.
 
Nkisomaga mada kama hizi hua naishia kucheka tu, hili taifa kua graduate ni kama kituko flan ambacho hakijielewi unamwambia chochote tu!

Mtaani mambo magumu sana lkn wazee wakiwa majukwaani au humu mtandaoni wanaongea as if wanatupenda sana na kututakia mema deep down hawana msaada wowote, lkn kama ni kijana wako au ndugu Yako humpi huu ushauri unapiga simu sehemu kijana ajibanze apate chochote ila wengn unawaambia wafungue biashara 😁😁😁usikute mtoa mada ana miaka 47 hajawahi fanya biashara yeyote
 
Nachowashauri graduates msichague kazi ya kukuingizia kipato halali, ukipata boda boda, bajaji wewe nenda nayo tu usisubiri mpaka upate kazi za kisomi, mtaani ni kugumu mno !
 
Nachowashauri graduates msichague kazi ya kukuingizia kipato halali, ukipata boda boda, bajaji wewe nenda nayo tu usisubiri mpaka upate kazi za kisomi, mtaani ni kugumu mno !
Thread closed!
 
Nkisomaga mada kama hizi hua naishia kucheka tu, hili taifa kua graduate ni kama kituko flan ambacho hakijielewi unamwambia chochote tu!

Mtaani mambo magumu sana lkn wazee wakiwa majukwaani au humu mtandaoni wanaongea as if wanatupenda sana na kututakia mema deep down hawana msaada wowote, lkn kama ni kijana wako au ndugu Yako humpi huu ushauri unapiga simu sehemu kijana ajibanze apate chochote ila wengn unawaambia wafungue biashara usikute mtoa mada ana miaka 47 hajawahi fanya biashara yeyote

Nkisomaga mada kama hizi hua naishia kucheka tu, hili taifa kua graduate ni kama kituko flan ambacho hakijielewi unamwambia chochote tu!

Mtaani mambo magumu sana lkn wazee wakiwa majukwaani au humu mtandaoni wanaongea as if wanatupenda sana na kututakia mema deep down hawana msaada wowote, lkn kama ni kijana wako au ndugu Yako humpi huu ushauri unapiga simu sehemu kijana ajibanze apate chochote ila wengn unawaambia wafungue biashara usikute mtoa mada ana miaka 47 hajawahi fanya biashara yeyote

Hapana lengo ni kuwajulisha Graduates kuwa unapokosa nafasi ya ajira kuna namna nyingine unaweza ku generate income kwa njia tofauti. Tupo mtaani vijana wamekata tamaa kabisa . Yaani wanaamini katika ajira ya serikali .
 
Walipoteza nafasi kubwa sana. Wangepata fursa ya kujifunza kazi na kuongeza ujuzi! Na hii mentality ipo kwa sisi waswahili
True nakumbuka ni mwaka jana tu hapo mwanzoni.
Mwaka huu pia nikakutana na mwingine huyu ni wakike wa mwanzo walikua wakiume and i offered her the same.Akauliza nitapata nini.
I told her utajifunza hizo mambo za darasan namna zilivyo huku field plus how to be able not just to create a product but also how to penetrate it kwenye market . unaweza ukawa unasoma na extra time unakuja ofisin na pia kuingia sokoni plus ku provide support kwa wateja waliopo so far

Akatoka nduki..nikaja hisi huenda pia vijana wanasoma vitu ambavyo hawavipendi ila ni basi tu ishu ya allocation za vyuo by tcu hawana namna plus kupata mikopo.

Naonaga tuu status zake anafanya package za maandazi unauza kisasa kidogo nikajua huyu IT anasoma basi tuu
 
Nachowashauri graduates msichague kazi ya kukuingizia kipato halali, ukipata boda boda, bajaji wewe nenda nayo tu usisubiri mpaka upate kazi za kisomi, mtaani ni kugumu mno !
ahahahaha..watakupiga mawe wewe ngoja wakusikie
 
Kaka mtu unajitolea silipwi chochote ntaishije Kodi, maji, chakula, nauli, umeme talipaje? vingn naweza nkajinyima


Najua ni changamoto kubwa !lakkni kukaa home tu haisaidii . Njia nzuri ni kutafuta sehemu unayoweza kuonesha ujuzi wako. Faida ya kujitolea ni kwamba utapata new connections ,networking na hapo unaweza pata mianya mingine ya kutoboa.

Pia unaweza chagua sehemu ya kijtolea ambayo unaweza kuwa comfortable
 
True nakumbuka ni mwaka jana tu hapo mwanzoni.
Mwaka huu pia nikakutana na mwingine huyu ni wakike wa mwanzo walikua wakiume and i offered her the same.Akauliza nitapata nini.
I told her utajifunza hizo mambo za darasan namna zilivyo huku field plus how to be able not just to create a product but also how to penetrate it kwenye market . unaweza ukawa unasoma na extra time unakuja ofisin na pia kuingia sokoni plus ku provide support kwa wateja waliopo so far

Akatoka nduki..nikaja hisi huenda pia vijana wanasoma vitu ambavyo hawavipendi ila ni basi tu ishu ya allocation za vyuo by tcu hawana namna plus kupata mikopo.

Naonaga tuu status zake anafanya package za maandazi unauza kisasa kidogo nikajua huyu IT anasoma basi tuu


Mkuu ni shida sana .Tena hii issue ya IT & ICT inahitaji ifunguliwe UZI humu jukwani maana vijana wa Ict naona kama ndio wahanga wa kubwa sana. Kuna muda nahisi kama mitaala yao inashida mahali.
 
True nakumbuka ni mwaka jana tu hapo mwanzoni.
Mwaka huu pia nikakutana na mwingine huyu ni wakike wa mwanzo walikua wakiume and i offered her the same.Akauliza nitapata nini.
I told her utajifunza hizo mambo za darasan namna zilivyo huku field plus how to be able not just to create a product but also how to penetrate it kwenye market . unaweza ukawa unasoma na extra time unakuja ofisin na pia kuingia sokoni plus ku provide support kwa wateja waliopo so far

Akatoka nduki..nikaja hisi huenda pia vijana wanasoma vitu ambavyo hawavipendi ila ni basi tu ishu ya allocation za vyuo by tcu hawana namna plus kupata mikopo.

Naonaga tuu status zake anafanya package za maandazi unauza kisasa kidogo nikajua huyu IT anasoma basi tuu
Nlifanya field ya kwanza kwenye taasisi Moja baada ya ule mda kwisha nliendelea na majukumu, mkuu wa ile taasisi akanambia utapata chochote siku unarudi chuo, mwisho wa siku hakunipa chochote akanambia ukitaka malipo mwaka wa pili urudi hapa na wenzako wawili au watatu!
Pia alinambia niandike barua za malipo nikatii maagizo lkn wapi .....

Mwaka wa pili nlienda halmashaur X majukumu nliyokua napewa mambo hayakua ya IT kbs hata kidogo yaan kila siku ni kupanga na kupangua mafaili nkafanya maarifa nkapata muhuri na assessment ikafanyika nkasepa pale nkaenda taasis Moja kujitolea huko aiseee nusu nife njaa,🤣 ndo nkaona bora nkajitose mtaani
 
Kaka mtu unajitolea silipwi chochote ntaishije 🤔Kodi, maji, chakula, nauli, umeme talipaje? vingn naweza nkajinyima
UKo sahihi.Lakin ukiendelea kukaa home bado unakua hutatui changamoto hizo.
Halaf pia katika kujitolea ujue unafanya kazi na watu lazima tuu kuna namna ambayo wata tafuta way to compasnte you japo kidogo.Ni watu nao wanajua una mahitaji.

Kwamfano later nikaja nikapata bint wa kukaa ofisin kwakua moat of time niko mtaani akawa anakuja mwenyewe fresh tuu saaa 10 akimaliza kazi anaondoka baadae tuka make sure akiwa ofsin anapata chakula cha mchana kila siku..
NOw tunampa 200k monthly kama nauli bado hatujaweza kumlipa..

SO mbali na maslahi angalia vitu vingine pia.
And she is a graduate ila imagine hata kuandika emails tu za kikaz alikua zero kabisa but she keeps improving
 
Nlifanya field ya kwanza kwenye taasisi Moja baada ya ule mda kwisha nliendelea na majukumu, mkuu wa ile taasisi akanambia utapata chochote siku unarudi chuo, mwisho wa siku hakunipa chochote akanambia ukitaka malipo mwaka wa pili urudi hapa na wenzako wawili au watatu!
Pia alinambia niandike barua za malipo nikatii maagizo lkn wapi .....

Mwaka wa pili nlienda halmashaur X majukumu nliyokua napewa mambo hayakua ya IT kbs hata kidogo yaan kila siku ni kupanga na kupangua mafaili nkafanya maarifa nkapata muhuri na assessment ikafanyika nkasepa pale nkaenda taasis Moja kujitolea huko aiseee nusu nife njaa,🤣 ndo nkaona bora nkajitose mtaani
Halmashuri huwa naona sii mahala sahihi sana kwa fani hizi za It 🤣
 
Back
Top Bottom