Hata Jana Kwenye Press conference ya Mbowe alipokuwa anataja Vyama bya Upinzani vyenye nia ya dhati aliitaja Pia ACT ya Zitto Kabwe Msaliti aliekuwa anaiba Siri Za Chadema Na kupeleka Usalama wa Taifa
Hata Jana Kwenye Press conference ya Mbowe alipokuwa anataja Vyama bya Upinzani vyenye nia ya dhati aliitaja Pia ACT ya Zitto Kabwe Msaliti aliekuwa anaiba Siri Za Chadema Na kupeleka Usalama wa Taifa
Wenyeviti Saba wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA ) Wilayani Arumeru mkoani Arusha wamejiunga na Chama cha Mapinduzi CCM katika ziara ya kikazi ya Mkuu wa wilaya hiyo Ndugu Jerry Cornel Muro katika Kata ya Maji ya Chai.
Wenyeviti wameamua kujiuzulu baada ya hapo juzi aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki Ndugu. Joshua Nassary kuvuliwa ubunge na Spika wa Bunge la Tanzania baada ya kutokuhudhuria vikao vitatu vya bunge mfululizo
Dc Muro akiwa ameambatana na Katibu wa CCM Wilaya ya Meru Mwalimu Kanuthi wamewapokea wenyeviti hao walioleza kuwa wameamua kujiunga na CCM ili kumuuunga mkono Rais John Pombe Magufuli kwa utendaji kazi wake Sambamba na kumpongeza Mkuu wa Wilaya hiyo kwa kazi anazozifanya na namna anavyotatua migogoro ya wananchi
Mwenyeviti waliopokelewa ni Mwenyekiti wa kijiji cha Ngurdoto Ndugu Mosses Ayo, Mwenyekiti wa Kijiji cha Maji ya Chai Ndugu Mase David Mbise pamoja na hapo amewapokea wenyeviti wa vitongoji vitano ambavyo ni Ndugu Perfect Philemon Mwenyekiti wa kitongoji cha Bondeni,Laurant Kessy Kitongoji cha Mburueshi, Elisante Akyoo Kitongoji cha KCenter Mwenyekiti wa kijiji cha Seneto Ndugu Christopher Mbise pamoja na Ndugu Amani Kitali Mwenyekiti kitongoji cha Kimandafu.
hata wakihama wote upinzani wa kweli utabaki siwezi kuunga mkono serikali iliyokuja nyumbani kumkamata ndugu yangu kisha nikarudishiwa maiti ya ndugu yangu baada ya kuchomwa kisu na polisi, siwezi kuiunga mkono serikali iliyonibomolea nyumba kimakosa na ikakataa kunilipa fidia, siwezi kuikubali serikali iliyosababisha mwanangu akafariki kwa kukosa dawa ya nyoka n.k
Hata Jana Kwenye Press conference ya Mbowe alipokuwa anataja Vyama bya Upinzani vyenye nia ya dhati aliitaja Pia ACT ya Zitto Kabwe Msaliti aliekuwa anaiba Siri Za Chadema Na kupeleka Usalama wa Taifa
Mkuu mia yote ni matumaini tu ? Pesa za CCM tunakula sisi ambao hatuipendi CCM. Jiongeze ndugu ;unadhani kuna kazi gani anakifanya Mzee Mangula ambalo kijana hakiwezi kukifanya ? Kaa na matumaini hivyo hivyo.
Na inawezekana yeye ana shida kuliko wewe, anachokikubali ni kwa sababu ndugu yake katumbuliwa. Kuna watanzania wengi wanaoishangilia ccm kwa sababu nurse, au mwalimu katumbuliwa na bado anashida kuliko aliyetumbuliwa.
Huyo Muro anahisi kuwarubuni wapinzani kuhamia ccm anapoonekana kwenye makamera ndio anamfurahisha mkuu. mbona kila siku ni viongozi tu wanaunga juhudi? mbona wananchi ambao ndio wapiga kura wenyewe hatuwaoni wakiunga juhudi?
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.