Allen Kilewella
JF-Expert Member
- Sep 30, 2011
- 18,235
- 33,825
Kila mara CHADEMA inalaumiwa kwa ajabu kabisa na watu wa CCM kwamba haina mawazo wala mbinu mpya zitakazowasaidia kuitoa CCM madarakani mwaka 2020. Inawezekana kabisa kwamba hii hoja ina ukweli fulani ndani mwake, lakini inapotolewa na wana CCM inatia shaka.
Shaka kwani kwa kila hali CCM inaonekana kuondoka kwake madarakani itakuwa ni kwa mbinde na si kwa hiyari ya chama hicho. Sasa CCM inapokuja na ushauri wa kuwa na mbinu bora za kuitoa madarakani inashangaza sana.
Lakini pia kuna wana - CHADEMA kwa nia njema kabisa wanaona na kuamini kuwa chama chao kinatoka nje ya mkondo wa kuiondoa CCM madarakani. Kundi hili likichagizwa na wanazuoni na watu wengine makini wapenda mabadiliko, lina hoja nyingi sana za msingi.
Lakini si wana CCM wala hawa wana CHADEMA wanaoona mbinu za kuiondoa CCM madarakani zinakosewa wanalo Jukwaa ndani ya vikao vya maamuzi vya CHADEMA. Kwa mantiki hiyo basi wale wanaoona kuna mbinu mbadala zaidi ya hizo zinazotumiwa na Viongozi wa CHADEMA kuiondoa CCM madarakani, basi waziweke hapa ili na wengine tuone ni kwa nini wanawalaumu viongozi wa CHADEMA kuishiwa mbinu za kuitoa CCM madarakani.
Shaka kwani kwa kila hali CCM inaonekana kuondoka kwake madarakani itakuwa ni kwa mbinde na si kwa hiyari ya chama hicho. Sasa CCM inapokuja na ushauri wa kuwa na mbinu bora za kuitoa madarakani inashangaza sana.
Lakini pia kuna wana - CHADEMA kwa nia njema kabisa wanaona na kuamini kuwa chama chao kinatoka nje ya mkondo wa kuiondoa CCM madarakani. Kundi hili likichagizwa na wanazuoni na watu wengine makini wapenda mabadiliko, lina hoja nyingi sana za msingi.
Lakini si wana CCM wala hawa wana CHADEMA wanaoona mbinu za kuiondoa CCM madarakani zinakosewa wanalo Jukwaa ndani ya vikao vya maamuzi vya CHADEMA. Kwa mantiki hiyo basi wale wanaoona kuna mbinu mbadala zaidi ya hizo zinazotumiwa na Viongozi wa CHADEMA kuiondoa CCM madarakani, basi waziweke hapa ili na wengine tuone ni kwa nini wanawalaumu viongozi wa CHADEMA kuishiwa mbinu za kuitoa CCM madarakani.