Wenye Blackberry, okoeni Jahazi huku.

Shin Lim

JF-Expert Member
Mar 27, 2012
7,300
13,183
Ni juzi tu kuna sista yangu wa tumbo moja alifika home na simu aina ya blackberry kutokea Mwanza. Sasa mimi nikaonesha kuitamani simu yake ingawa sikumwambia wazi wazi.
Nikiendelea kuimezea mate simu yake huku nikimiliki mchina aina ya YUNTERE, yenye thamani ya sh 6,500 (elfu sita na mia tano) kwa bei ya mtaani.
Hii ni simu yenye uwezo na uzoefu mkubwa wa kuingia na kutoka JF bila shida yeyote.
Sasa dada alipoona naitamani simu yake, akasema nimpe simu yeyote ile ilimradi inapiga na kupokea halafu yeye aniachie yake, na mimi bila hiyana nikampa yangu na zoezi likafanikiwa.
Sasa mziki umekuja leo baada ya yeye kuondoka, mama yangu Jf naisikia kwa jirani licha ya kuwa na kifurushi, tena cha heshima tu.
Wakuu naomba mnisaidie simu yangu haina intaneti ingawa nina kifurushi. Ni blackberry 8520.
Ahsante wakuu.
 
Nimeunga cha kawaida cha airtel cha
*149*99# sasa, ambacho ni sh 1999 ila nina uwezo wa kupiga simu na kutuma sms tu na si intaneti yaani mpaka sasa net kwa jirani mkuu.
 
My dear me navyojua blackberry ina bundle lake special kwa ajili ya internet, tofauti na hizo bundle za kawaida za cheka etc. Bahati mbaya me najua kuunga bundle la bb kwa voda. Anyway ngoja niulizie then ntakupa feedback kama itakuwa bado hajajitokeza mtu mwingine anayejua

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
My dear me navyojua blackberry ina bundle lake special, tofauti na hizo bundle za kawaida za cheka etc. Bahati mbaya me najua kuunga bundle la bb kwa voda. Anyway ngoja niulizie then ntakupa feedback kama itakuwa bado hajajitokeza mtu mwingine anayejua

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums

Ahsante mkuu, nitashukuru sana kwa msaada wako, lakini mpaka sasa nashukuru kwa nia yako ya kuisaidia, hali ngumu huku.
 
Mashart makubwa ya b berry mojawapo lazima ujiunge mara2
Kifurushi cha BBM na kama unataka kupiga na kupokea unajhunga na chakawaida
 
  1. Nenda kwenye setting,
  2. Ingia Quick setting
  3. Angalia mobile network
  4. Tick Pata kwenye mobile network
  5. Rudi kwenye main menu
  6. Bonyeza Browser itaconnect
NB-Haitatumia hiyo bundle yako, weka pesa kwenye simu yako.

Ukipata nafasi nenda ofisi za Airtel utapewa huduma za BIS kwa kujiunga na BB world, internet ni bure!, utapewa BB ID, na kujiunga na BBM zote bure!.

Faida
  1. Blackbery ndio simu salama kuliko simu nyingine zozote, ukiishapewa BB ID mtu yoyote akiiba hiyo simu yako, akitumia tuu BBM anadakwa, unaweza kuifunga simu hawezi tena kuiwasha, BB haina na eti kuflush na kufuta kila kitu, simu yako ya BB ikiishakuwa yako ni yako!.
  2. Japo net yake ni 3G, unaweza kuwapatia watu hadi 8 internet connectivity ya WIFI kupitia BB yako, unaweza kuconnect laptop yako kwa Bluetooth au kwa us cable kwenye PC yako na kuitumia kama moderm.

Hasara,
  1. Ni expensive to run, net yake haitumii bundle!, na BIS inalipiwa!.
  2. Ni expensive kuinunua
  3. Haina mchina!.
Pasco.
 
Mashart makubwa ya b berry mojawapo lazima ujiunge mara2
Kifurushi cha BBM na kama unataka kupiga na kupokea unajhunga na chakawaida

Exactly my dear, kwa sababu bundle la b berry linakuwa kwa ajili ya internet tu. Ukitaka sms na dakika za kuongea itabidi uunge vifurushi vya kawaida na zile MB utakazopewa kwenye vifurushi vya kawaida nadhani haviwezi kuunga internet kwenye black berry.

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
  1. Nenda kwenye setting,
  2. Ingia Quick setting
  3. Angalia mobile network
  4. Tick Pata kwenye mobile network
  5. Rudi kwenye main menu
  6. Bonyeza Browser itaconnect

    Pasco, nafikiri akishaunga hilo bundle ndo afate haya maelekezo yako, au?


    Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Mie hiyo simu ya Obama,naiogopa sana,kutokana na appl zake nimeiuza blackbery 9300 sh200000/-sababu ya kadhia hiyo.otherwise ni simu mzuri sana.
 
Hilo BlackBerry walishaliona ndo maana BlackBerry mpya zinazotoka BB Z10,Q10,na z30 hazina hiyo shida zinatumia bundle za kawaida kabisa
 
Dah! Naona kama kifurushi cha blackberry kimevaa koti la muungano hivi!
Yaani kifurushi chake kijitegemee!
 
Nimeunga cha kawaida cha airtel cha
*149*99# sasa, ambacho ni sh 1999 ila nina uwezo wa kupiga simu na kutuma sms tu na si intaneti yaani mpaka sasa net kwa jirani mkuu.

Mkuu blackberry ina bundle zake maalum sio hiyo uliyounganisha ww.wapigie airtel afu wailize khs vifurushi vya BlackBerry utajuzwa na utafurahia tuu
 
  1. Nenda kwenye setting,
  2. Ingia Quick setting
  3. Angalia mobile network
  4. Tick Pata kwenye mobile network
  5. Rudi kwenye main menu
  6. Bonyeza Browser itaconnect
NB-Haitatumia hiyo bundle yako, weka pesa kwenye simu yako.

Ukipata nafasi nenda ofisi za Airtel utapewa huduma za BIS kwa kujiunga na BB world, internet ni bure!, utapewa BB ID, na kujiunga na BBM zote bure!.

Faida
  1. Blackbery ndio simu salama kuliko simu nyingine zozote, ukiishapewa BB ID mtu yoyote akiiba hiyo simu yako, akitumia tuu BBM anadakwa, unaweza kuifunga simu hawezi tena kuiwasha, BB haina na eti kuflush na kufuta kila kitu, simu yako ya BB ikiishakuwa yako ni yako!.
  2. Japo net yake ni 3G, unaweza kuwapatia watu hadi 8 internet connectivity ya WIFI kupitia BB yako, unaweza kuconnect laptop yako kwa Bluetooth au kwa us cable kwenye PC yako na kuitumia kama moderm.

Hasara,
  1. Ni expensive to run, net yake haitumii bundle!, na BIS inalipiwa!.
  2. Ni expensive kuinunua
  3. Haina mchina!.
Pasco.

Pasco nmeipenda, naomba unsaidie kama kwa lin ya voda napo naweza kupata huduma hyo maana m na blackberry ya toch.. Naipenda na cna mpango wa kuibadili maana napata huduma zote...
 
Au piga magic number
*148*00# nenda option ya internet then nenda option ya blackberry utapata
 
Jiunge kifurushi cha mtandao wako cha bb halafu
Ingia option nenda advance option ingia host routing table click kushoto kwenye alama ya bb nafuta neno register now click zima simu wacha utajiunga



Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
na whatsApp unaipataje kupitia bb ikiwa nna bb ya 9780 na natumia mtandao wa vodacom?

Wajameni saidia mimi!
 
Back
Top Bottom