Wenye akili wameanza kuhama nyumba zilizo wekwa X barabara ya Morogoro

Tulimumu

JF-Expert Member
Mar 11, 2013
14,305
12,969
Baada ya Tanroads kuweka X nyumba zilizo ndani ya hifadhi ya barabara ya Morogoro kuanzia Kimara Stop over baadhi ya watu wenye akili na waelewa wameanza kuondoka ili kupisha upanuzi wa barabara na ili kuokoa baadhi ya mali zao kabla tinga tinga halijafika.

Kwa maoni yangu nafikiri huu ni uamuzi mzuri kwani unasaidia kuokoa zaidi ya asilimia 80 ya mali badala ya kusubiri mpaka dakika ya mwisho kama ilivyowatokea baadhi ya wananchi wabishi kule Mbezi mwisho. Nawashauri wakaazi na wafanyabiashara waliomo kwenye nyumba zenye X waanze kufungasha virago kabla tinga tinga halijafika. Nawashauri wajiepushe ba wenzao wachache wanaowadanganya kwa maelezo kuwa wamezuia kwani hiyo haiondoi ukweli kuwa wataondoka hivyo ni vema wakaondoka taratibu na kuokoa mali zao. Mfano kuna mmiliki wa bar moja maarufu hapa Kimara Suka karibu na kituo cha mafuta yeye kaona isiwe shida kaamua kuondoka badala ya kusubiri vunja vunja ambayo inaweza kuathiri mali zake.

Mimi nimeona niwashauri kwa nia nzuri wananchi hao waondoke mapema badala ya kusubiri gharika kama ile ya Mbezi watafute maeneo mengine wakajipange upya. Ardhi haijaisha katika nchi hii.
 
tatizo unakwenda wapi???? ukute mtu ana nyumba hiyohiyo moja, na anafamilia kubwa anahitaji kodi kwenda kupanga nyumba ya familia asa unadhani atafanyaje????

hali tete, ila kwa ambae ana nyumba sehemu nyingine hana shida ni swala la kuhamisha mizigo basi.
 
Barabara Ni Lazima Kupanuliwa Kwahiyo Ni Lazima Wahame Lakini Je Kwa Fidia Au Kimyakimya Tu
 
Kwa maoni yangu nafikiri huu ni uamuzi mzuri kwani unasaidia kuokoa zaidi ya asilimia 80 ya mali badala ya kusubiri mpaka dakika ya mwisho kama ilivyowatokea baadhi ya wananchi wabishi kule Mbezi mwisho.


Hebu thibitisha ni namna gani umepata hiyo 80%
 
tatizo unakwenda wapi???? ukute mtu ana nyumba hiyohiyo moja, na anafamilia kubwa anahitaji kodi kwenda kupanga nyumba ya familia asa unadhani atafanyaje????

hali tete, ila kwa ambae ana nyumba sehemu nyingine hana shida ni swala la kuhamisha mizigo basi.
Kwa hiyo utasubiri tingatinga lije libomoe na kuharibu vitu vyako kwa sababu huna pa kwenda
 
Baada ya Tanroads kuweka X nyumba zilizo ndani ya hifadhi ya barabara ya Morogoro kuanzia Kimara Stop over baadhi ya watu wenye akili na waelewa wameanza kuondoka ili kupisha upanuzi wa barabara na ili kuokoa baadhi ya mali zao kabla tinga tinga halijafika.

Kwa maoni yangu nafikiri huu ni uamuzi mzuri kwani unasaidia kuokoa zaidi ya asilimia 80 ya mali badala ya kusubiri mpaka dakika ya mwisho kama ilivyowatokea baadhi ya wananchi wabishi kule Mbezi mwisho. Nawashauri wakaazi na wafanyabiashara waliomo kwenye nyumba zenye X waanze kufungasha virago kabla tinga tinga halijafika. Nawashauri wajiepushe ba wenzao wachache wanaowadanganya kwa maelezo kuwa wamezuia kwani hiyo haiondoi ukweli kuwa wataondoka hivyo ni vema wakaondoka taratibu na kuokoa mali zao. Mfano kuna mmiliki wa bar moja maarufu hapa Kimara Suka karibu na kituo cha mafuta yeye kaona isiwe shida kaamua kuondoka badala ya kusubiri vunja vunja ambayo inaweza kuathiri mali zake.

Mimi nimeona niwashauri kwa nia nzuri wananchi hao waondoke mapema badala ya kusubiri gharika kama ile ya Mbezi watafute maeneo mengine wakajipange upya. Ardhi haijaisha katika nchi hii.
Hata wasio na akili wanatakiwa kuhama
 
Kwa hiyo utasubiri tingatinga lije libomoe na kuharibu vitu vyako kwa sababu huna pa kwenda
siyo kwamba asubiri, ukute nae yupo kwenye taratibu za kuhama, lakini hawezi kufanya haraka kama mwingine. kumbuka uwezo haufanani.
 
Hebu thibitisha ni namna gani umepata hiyo 80%
Unaweza kutoa mali zako za ndani vizuri na kwa utaratibu bila kuathirika, utafumua bati au vigae vyako vizuri na kuweza kutumia sehemu nyingine, unaweza kufumua hata tofari baadhi zikaweza kutumika huko mbele ya safari, unaweza kuchukua kifusi chote kilichotokana na wewe mwenyewe kubomoa nyumba yako, unaweza kuokoa sehemu kubwa ya mbao na kuweza kuzitumia tena nk nk nk. Sasa ukisubiri mpaka tinga tinga lifike utaokoa nini mkuu? Inaweza isifike asilimia 80 lakini cha msingi utapunguza hasara kwa kiasi kikubwa

Sent from my SM-N9005 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom