Mkalukungone Mwamba
JF-Expert Member
- Aug 29, 2022
- 2,437
- 5,235
Wenje ameendelea kujimaliza, mwenyewe na kujiona mjanja
Tumika baba!
====================
Mwanachama mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ezekiah Wenje, amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, jumla ya kesi 417 zilifutwa, ikiwemo kesi sita zilizokuwa zikimkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, kama sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya 4R iliyoanzishwa na Dkt. Samia.
Wenje ametoa kauli hiyo leo Oktoba 18, 2025, alipohutubia mkutano wa kampeni wa Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika katika viwanja vya Sabasaba, Namanyere wilayani Nkasi mkoani Rukwa.
Amesema anashangazwa na baadhi ya watu wanaomshambulia Rais Samia wakidai serikali yake imeminya demokrasia, ilhali ni yeye aliyefungua ukurasa mpya wa siasa za maridhiano nchini.
Ameeleza pia kuwa wakati CHADEMA iliposusia ruzuku ya serikali na kukumbwa na changamoto za kifedha, ni uamuzi wa Dkt. Samia uliowezesha chama hicho kuendelea tena kupokea ruzuku, hatua iliyochangia kununuliwa kwa majengo yanayotumika kama Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Mikocheni, Dar es Salaam.
Tumika baba!
====================
Mwanachama mpya wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ezekiah Wenje, amesema kuwa katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, jumla ya kesi 417 zilifutwa, ikiwemo kesi sita zilizokuwa zikimkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, kama sehemu ya utekelezaji wa falsafa ya 4R iliyoanzishwa na Dkt. Samia.
Wenje ametoa kauli hiyo leo Oktoba 18, 2025, alipohutubia mkutano wa kampeni wa Mgombea wa Urais kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan, uliofanyika katika viwanja vya Sabasaba, Namanyere wilayani Nkasi mkoani Rukwa.
Amesema anashangazwa na baadhi ya watu wanaomshambulia Rais Samia wakidai serikali yake imeminya demokrasia, ilhali ni yeye aliyefungua ukurasa mpya wa siasa za maridhiano nchini.
Ameeleza pia kuwa wakati CHADEMA iliposusia ruzuku ya serikali na kukumbwa na changamoto za kifedha, ni uamuzi wa Dkt. Samia uliowezesha chama hicho kuendelea tena kupokea ruzuku, hatua iliyochangia kununuliwa kwa majengo yanayotumika kama Makao Makuu ya chama hicho yaliyopo Mikocheni, Dar es Salaam.