Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 1,770
- 1,173
WEKENI MBELE MASLAHI YA TAIFA - WAZIRI KOMBO
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefungua Kikao cha Kwanza cha Baraza la Wafanyakazi la Wizara na kuwasihi wafanyakazi wa Wizara kuweka mbele maslahi ya Taifa.
Mhe. Waziri Kombo ametoa Rai hiyo jijini Dar es Salaam alipozindua Baraza Hilo na kuwapongeza wafanyakazi wa Wizara kwa ushirikiano wanaompatia katika kipindi cha miezi 10 Wizarani
“Nawapongeza kwa utendaji mzuri na wenye tija ambao nimeushuhudia tangu Ninga hapa wizarani, mbali na kufurahishwa na utendaji wenu, ni vyema watumishi wote mkakumbuka kutanguliza maslahi ya Taifa mbele wakati wote mkitekeleza majukumu yenu”. alisema
Pia Mhe Waziri amewasihi wawakilishi wa Idara na Vitengo katika Baraza hilo kuwa wawakilishi wazuri na kupeleka mrejesho wa kikao hicho kwa maafisa wenzao wanaowawakilisha.
Aidha, Mhe. Waziri Kombo amewasihi viongozi kujenga tabia ya kuwajengea uwezo watendaji walioko chini yao ili kuwa na watendaji wenye ubora na ujuzi katika maeneo yao pale ambapo viongozi hao wataenda kufanya majukumu mengine ama kustaafu.
Nao Wajumbe wa Baraza hilo, wamewasilisha hoja mbalimbali kuhusu masuala yatakayosaidia kuiinua utendaji wa Watumishi ikiwemo kuongezwa kwa mafunzo maalum kwa ajili ya kuwanoa Maafisa katika maeneo maalum kulingana na uhitaji wa kazi za kila siku.
Kwa upande wake Afisa Kazi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Bi. Honesta Ngoli, amewasihi watumishi wa Wizara kufahamu malengo ya Wizara na kutekeleza vyema majukumu yao ili kuweza kwa pamoja na hivyo kuchangia kufikia malengo ya Taifa.
Baraza hilo pia limehudhuriwa na wawakilishi kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) Taifa pamoja na Wizara.
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefungua Kikao cha Kwanza cha Baraza la Wafanyakazi la Wizara na kuwasihi wafanyakazi wa Wizara kuweka mbele maslahi ya Taifa.
Mhe. Waziri Kombo ametoa Rai hiyo jijini Dar es Salaam alipozindua Baraza Hilo na kuwapongeza wafanyakazi wa Wizara kwa ushirikiano wanaompatia katika kipindi cha miezi 10 Wizarani
“Nawapongeza kwa utendaji mzuri na wenye tija ambao nimeushuhudia tangu Ninga hapa wizarani, mbali na kufurahishwa na utendaji wenu, ni vyema watumishi wote mkakumbuka kutanguliza maslahi ya Taifa mbele wakati wote mkitekeleza majukumu yenu”. alisema
Pia Mhe Waziri amewasihi wawakilishi wa Idara na Vitengo katika Baraza hilo kuwa wawakilishi wazuri na kupeleka mrejesho wa kikao hicho kwa maafisa wenzao wanaowawakilisha.
Aidha, Mhe. Waziri Kombo amewasihi viongozi kujenga tabia ya kuwajengea uwezo watendaji walioko chini yao ili kuwa na watendaji wenye ubora na ujuzi katika maeneo yao pale ambapo viongozi hao wataenda kufanya majukumu mengine ama kustaafu.
Nao Wajumbe wa Baraza hilo, wamewasilisha hoja mbalimbali kuhusu masuala yatakayosaidia kuiinua utendaji wa Watumishi ikiwemo kuongezwa kwa mafunzo maalum kwa ajili ya kuwanoa Maafisa katika maeneo maalum kulingana na uhitaji wa kazi za kila siku.
Kwa upande wake Afisa Kazi Mkuu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Kazi, Ajira, Vijana na Wenye Ulemavu, Bi. Honesta Ngoli, amewasihi watumishi wa Wizara kufahamu malengo ya Wizara na kutekeleza vyema majukumu yao ili kuweza kwa pamoja na hivyo kuchangia kufikia malengo ya Taifa.
Baraza hilo pia limehudhuriwa na wawakilishi kutoka Chama cha Wafanyakazi wa Serikali na Afya Tanzania (TUGHE) Taifa pamoja na Wizara.