Wanaumeeeee, wanaumeee Knyokoooo!
Kiukweli habari iliokuwa ina kiki ni issue ya Nadya kuliwa na Leo na usiku huo huo jamaniii hata kungoja kukuche kaenda kuliwa na mwanaume mwingine, tena wa kumuokota club. Khaaaaaaaaaaaaa! Sh just hit a new low yaaai hata sio low kafikia kabisa savage levels. Nuksiiiii sanaaaaa! Vivi ni beyond kukasirika mpaka kabakia kuhuzunika, anasisitiza hilo ni pepo a ngono. Na pepo kweli jamaniii. Walau hata ingekuwa asubuhi yake.
Mi Monica sikutaka kum judge sanaaa based on experience yangu mpaka nikazalishwa mtoto na mwanaume wa hovyo hovyo kiukweli nlimpa benefit of the doubts tu. Mimi wanaume nawajua jamaniii mwenzenu washanifanya vibayaaaa nafuuu uliwe kibogaaaa. Jiulize walinifanya nini zaidi cha kutishaa nafuuu uliwe kiboga. Hahahaaaa.
Mimi mwenzenu at the peak ya usichana wangu, mzuriiii mzuriii kweliii nikawa nimewivaa kama yai, nimemaliza chuo niawa na shoga angu ana kichen party. Tumepita pita maduka ya vyombo, tukapita duka moja kuna mkaka mzuriii anauza. Akatuambia duka lake akatuchangamkia sana. Akachukua namb zangu za simu.
Tukaanza uhusiano. Naeda pale dukani, naona mipesaaa anayofunga hesabu.Ananinunulia nachotaka, napelekwa nakotaka, nakula nachotaka. Tulipendana sanaa mnooo. Nakaa pale dukani, yaaani duka ndo lililo nitia uchizi. Kufanyana hotel za gharamaa gharamaaa tu, anachota pesa ya mauzo siku zinaenda. Nikaamua nimbebe mimba. Nikabeba mimba bwana.
Ikawa sasa inabidi ku make it official, tujuanee, wazazi wakaweka ngumu wanideposit kwa mkaka. Nishampanga mama bwana huyu mwananume sio hawa vinuka mkojo wa mitaania, mtu na pesa zake, mtu na biashara zake za china, wanashusha makontenaaa. Nikampeleka mpaka dukani akajionea mapesa yalivojaa kwenye drooo. Akaanza kufosi ndoa sasa.
Kikaa kikao, wakaja kwetu kujitambulisha. Hapo ndipo pilau lilipoingia shubiri. Katika utambulisho akaja dada mmoja shangingi shangingi sana, kavaa dhahabu mijikufuuu, hereni, bangili kama sio kilo 2 basi 3. Sio gram nugu msomaji KILO. Lace wig kama ya 1.2 she screamed money all over. Akaja na mumewe mbabu kizeee kabisaa ila kinaonekana mapesaa yamejaaa.Akajitambulisha ndo dada wa baba kijacho. Wakatajiwa mahari wakasema watarudihaina shida. Shughuli ikaisha salama.
Kimbembe kikaanza kesho nimeenda dukani nakuta baba Kijacho yuko nje, pembeni, yule dada mtu ndo yuko ndani, kama incharge na kijan mwingine design kamtoa moshi juzi juzi. Nimekaa pale nje kama hanionii yuko busy ana mkabidhi mahesabu huyo kijana mpya. Anaongea ongea umeibaaa mpaka unaoaaa mwanasheriaaa. Umeniibia sanaaa. Usijali mwanasheria atakutunzaaa.
Kiukweli nilistukaaa, nikavurugwaa ila nilimuonea huruma baba kijacho, nikamwambia twende kwetu. Hapo kawa mdogo kadataa. Njiani ndo kuniambiaukweli sasa kumbe nae kinuka mkojo tu, duka la dada yake kabisaa kabisaa haelewi kwa nini anamfanyia hivo hajui cha mtu mavi. Kuongozana nae kwake kumbe bandugu ana chumba kimojaaa tena cha uani kaibu na choo. Mtu akinya unasikia harufu yooote. Nilikaa dakika 10 nikashindwa kabisaaa.
Nikamwambia mama ukweli, alinichambaaa sina akili, nimemtia aibuuu mtaani, sijui nini. Nikawa niko nyumbani nalea mimba. Sina kazi, baba Kija hana kazi. Anakuja nyumbani kula sasa cha asubuhi, mchana na jioniii. Cha ajabu mama babaKija hamnyanyasi hata kidogo anamuheshimu sanaa, n baba nae anaona ni maisha tu. Wanaume wako simple sanaa, na ishu yangu alikuwa tu muelewa kwamba imetokea. Ila ma mimi ndo alinikalia kooni, atamsimanga baba Kija weeee mpaka kufuru akija mwenyewe kimyaaaaa.
Sasa ile kumsemana kumshusha wadogo zangu wakaanza kutokumuheshimu. Wanamuheshimu vipi mama kutwa kucha kumsema hana maana, analishwa na wakwe sijui nini. Baba Kija akaona tatizo lipo, ila sasa afanyaje maskini. Na duka la dada yake hakukaa kwa akili wala nini. Hakuwa na savings zozote pesa yote aliokuwa analipwa na kuiba tuliitumbua. Ila mwenyewe akajiongeza aanze kutembeza vyombo. Akaongea na dada yake awe anampa vyombo mali kauli anapita navo mtaani jioni anapeleka hesabu.
Mama alipingana sanaa na hilo swalaaa kidogo apate kisukariii. Monica hawezi kuolewa na mtu anaeuza vyombooo mtaani. Degree ya sheria unaishia kwa muza vyombooo. Maneno kibao. Umedhallisha ukoo, umevua nguo baba yako. Baba yangu mwenyewe supervisor kiwandani wala sio mtu na wadhfa sijui au vipi. Maneno mwengiii kapewa u supervisor kusimamia viarua sema mcheza dili sanaaa so kidogo pesa hazimpigi chenga. Hana kikubwa ila kidogo hakimshindi. Baba akasema mwche auze pesa utampa wewe za wembe. Mama aliongeaaa. Maskini aba Kija akipata hata kidogo ananipa hio pesa, ila sasa uzuri wote wa kupulizw na kiyoyozi cha duka na magari ya dada ukaishaaa. Akawa mweusi kafubaa jua. Pesa ya bia hanaa,akaanza kunywa virobaaa.
Nikajifungua salama mtoto wa kiume. Baba akasema tuishi wote tu ila sio pale nyumbani. Akaongea na mkwewe kwamba kuna mchezo wanacheza ofisi mtu anatoka million 8, yeye jina lake ndo limefika, atampatia hio pesa afungue duka la vyombo, kulipa frame na mtaji kidogo vyombo vingine achukue kwa dada yake, afu tukiuza tuwe tunamlipa kidogo kidogo. Aimuona kama Mungu wake wa duniani.
Uzuri baba ake biashara anaijua sanaaa, kaifanya mda sanaa, na ashajlikana. Kuwapata wateja wakewa zamani haikuwa ishu sanaa. Dada mtu hakufurahi yeye kufungua duka, ila yeye si mchaga wachaga wenzie wakaanza kumpa mizigo, mi ndo nakaa dukani, nashika pesa, yeye anatafut kazi. Kiukweli ndani ya miezi 6, tukalipa pesa yote ya baba. Ndani ya mwaka tukaanza kupata jina, maji mkuwa Mr. akasafiri kwenda China akanza kushea container na wenzie wa 4 wana shusha 40 ft. Badae wakabakia wanasha w 2 baadae anashusha la kwake.
Pesa ikawa nyingi sanaa, msicheze na pesa akapatana na dada yake wakaanza kufanya biashara pamoja sasa damu nzito. Akanihadaa mke wangu sahivi na pesa kaa nyumbani nakupa unachotaka nakulipa million 3 kwa mwezi, sitaki ufanye chochote. Nikagomaaa. Baadae akaanza unachongangania dukani ni umalaya si kingine. Nikaamua tu kukaa nyumbani. Manyanyaso yakaanza sasa. Nikaanza kuchakaa. Dukan kawaleta ndugu zake kiba. Pesa inaisha naenda kuomba pesa dkani napewa 15,000 jamani ya wiki nzima hapo kaenda china. Tena mtoto mdogo na madharau ya kichaga ananiambia pesa nyingi sanaa hio. Mama kijijini hatumiii hio.
Nyubani ma shemeji kama 6, wengine wanasoma wengine wako wako afu viburiii viburiiii. Siku ya siku kaaajiri mdada mchaga mwenzao ndo muuza duka, anajua biashara katoka sijui kwa waarabu gani mi natizama tu. Mimi siku hio nimetoka kuingia bafuni nyumba ilikuwa ya kizamani bafu sio master,shemeji kaja kuweka dawa na hirizi chini ya godoro mi sijui. Anarudi kaka yake eti katoka kutazamiwa kwa mganga mie namloga jamanii. Miee huyooo. Kaambiwa nimeweka dawa na hirizi chini ya godoro. Kufunua kweli vipooo. Nkafukuzwa nirudi kwetu bila mtoto. Niliumiaaa roho yanguuu.
Nikaa nyumbani siku moja nasikia mwanangu wanataka kumpeleka Moshi. Nikaenda na panga wasinitanieeee nikachukua mwanangu na kurudi nyumbani. Basi ndo kusema nisikanyage tena dukani wala nyumbani. Nikakaa week baba anampigia aje tuzungumze hataki akamblock. Bababa akasema siwezikukubali ngojaaaa. Akamfatadukani akagoma kuonana nae. Akaanza kumpigia kelele kwamba Mangi huna shukraniiiii, ulitelekezwa nikakulishaaa wewe na kukulelea mimba pesa ya hospital nimetoa mimi, mtaji nimekupa mimi afu sahivi unamnyanyasa mwanangu nasemaje sasa navua nguo hapa leo, mchana kweupeee nakuachia laana ijulikane mojaaaa. Na hata uspolaanika wakisiki watu baba mkwe wako nimevua nguo hapa na kuuza utu wangu watakujua ulivo na hamna mtu atakae kuja tena kununua. Mmmmmmmh! Akaona ngoma nzitoooo. Akaamua kutoka nje wazungmze.
Akakubali nirudi nyumbani, ila kubali yenyewei ili tu baba asimvulie nguo, na anajua mzee wangu zee la mjini hashindwi kuvua kweli ikawa balaaa tupu. Mzee akamwambia ukimnyanyasa kidogo nakuja kuvua nguo hapo saa 4 asubuhi na kaa uchi mpaka jua lizame. Ila kurudi sasa ngoma nzito, chumba knitenga, hali chakula changu mie si mchawi tena nataka kumlisha libwata, sijui nataka kumuua. Na mtoto pia sijui mwanga msaidiziii akawa anamfanyia ukatili mpaka mtoto akajua na udogo wake yule si baba yangu. Nikawazaaaa nakuwazaa kwani lazima kuolewaa. Hapa ndo ishakufaaa. Watu wananiambia pambana na ndoa yako, muombe Mungu. Mmmmmhhhh! Yatakwishaaa.
Wifi hatuongei mda kabl hata mambo ya kuloga na kuweka dawa, siku akaja mi nimejikalia kimyaa kama mfungwa, akaniambia wifi na maongezi na wewe, nikashangaaa. Akaniambia wifi kukweli wewe hujawahi kutukosea chochote basi tu warombo jeuriii sisi ndo tulivo sasa haya mambo yamefika pabaya. Mwenzio anatka kukua. Nikastuka Kuniuaaaa? Nimemkosea nini? Bwana mwenzio kashikwa akili na yule mwanamke alietoka kwa mwarabu, mimi nauhakika yeye ndo alie weka dawa ile. Sasa anamwambia wewe na baba yako mnataka kwenda mahakamani mgawane mali. Wewe mwanasheria utampukuta kila kituuu. Bora wakuue tu wawe na amani na hizi mali.
Hapa navokwambia waha kuchota unyayo,kitako wako kwa mganga wanapika makombeee huko na kupiga ramli za kufa mtu. Wameleta mtaaamu kutoa nyasa huko kwa kazi hio. Yule mwanamke mshirikina huyooo sijapata kuonaa. Anajua waganga mpaka wa Dubai. We chukua mwanao ondoka, na usiende kwenu nenda kusiko julikana Mungu atakusaidia tu bila hivo watakuumiza. Nakupa hii million 1 itakusaidia pa kuanzia. Usichukue chochote we toka na malapa kama unaenda dukani afu tokomeaaa kimojaaaa. Wakija kushtuka ushafika mbali sanaaa.
Huyu mpe mwaka tu niamini hana mia. Mwenyewe nimeacha biashara nae, hana usimamizi, management hana, wanamuibiaaa, wanamchota alikata mtaji kachukua mkopo million mia 4 bank. Huyu niamini mimi mwaka mwingi ataanza kutembeza vyombo tena. Pesa yote ialiwa kwa waganga na wataalamu. Mi naondoka kaa kama nusu saaa afu fanya nilivo kwambia. Mwenyewe haya mambo nimepewa na binamu yangu alie dukani kwenu nijiandae na msibaaa. Wapuuzi kweli.
Nilikufa ganziii. Nikaka dakika 10, lisaa niliona refu, nikambeba mwanangu stand ya bus, nikapanda shabiby mpaka Dodoma. Nimekaa Dodoma siku 2 napigiwa simu mama kafariki huku ghaflaaa. Nikarudiii. Kafariki vipi kakutwa katapika na hajakubwa, waswhili wakwa wanasema alikabwa na jini makata. Lile likitmwa halirudi bila roho. Nikaja kweli walitaka kuniuaaa, walivonikosa nyumbani kwangu wakaja kwetu wakamkumba mama maskini. Roho iliniumaa sanaaa. Akaja msibani mzazi mwenzangu, nikamfukuza mbele za watu, nikamchana live umetuma jini liniueee limemuua mama. Nakwambia mbele za watu ukiniuaaa nakwambia nitakulaa ukooo wako woooteeeeenitazikwa nao. Niguse na mwanangu uone. Watu wakamuondo msibani. Bado sikuridhikaaa, niktakaa maiti tumpelekee dukani kwake aile nyama, yeye si ndo kamuaaa. Niliumia sanaaaaa, sanaaaaa.
Baba akasema haya mambo hayana ushahidi kama kweli kafanya hivo yeye anamuachia Mungu, sisi wakristo tumtegemee Mungu atatulipia. Tusiwe watu wa visasi na kuhukumu tumuachie Mungu. Niliumia sanaaa sanaaaa. Baada ya msiba ikawa sasa business is closed, kuniua hawezi maana nishamchana mbele za watu, afu akawa hajui nimepoajee onajeee operation yao, akawa anahisi sasa mimi ndo nammaliza yeye, yeye si kapiga one kik one goal afu he missed sasa manake mi nawazidi nguvu si ndio. Wakawa wanajinyea nyea kuchinjambuzi kila baada ya masaa 6 kufanya makafara ya kujilinda.
Mi nikaondoka nyumbani na kwenda kupanga mbali kabisaaa, nikakata mawasiliano, kwenye kiduka chao sipitiiii. Hawajui niko wapi wala nafanya nini. Ndo nikakutana sasa na yule shostiii. Mwanangu akaanza kuumwa ndo nikakutana na waziri. Ila maneno mengi sanaa yalisemwaa, Monica malayaaa kaachika, Monica maisha yamemshindaaa, kaachwa anateseka maisha yamemla kibogaaa.
Watu hao hao baada ya yule bwana kufilisika kamili sasa mpaka karudi kwao rombo analima viaru na kulewa mbege na virobaaa ndo wanasema Monica ana akili sanaaa, yule hakuwa mwanaume, ule mkosiii mkosiii omba ukupitie kandooo. Hahahaaaaaa! Jamaniiii. Yule bwana yuko hai, huko kwao Rombo analima vibarua na kujenga jenga kulewa mbege na viroba mda wote. Yaani sio mtu wa kumtambulisha mwanangu alie zoea kumuita Waziri wa nchi baba, japo anajua waziri ni baba mleziii, ila moyoni atakuwa anahsi labda baba yake mzazi alikuwa Dr hivi, a Pilot au Enginerrr ila sio mnywa viroba asilaniii. Nawaza nikisema nimwambie nita muathiri kisaikolojia mjue. Ndugu msomaji ingekuwa wewe ungemwambia mwanao ambae umeinvest so much money into his future huu upuuzi. Anaweza kupata depression come on shule yenyewe IST unaanzaje kuwa na baba mnywa viroba? And my son is all i have and i am not risking his peace of mind for a looser who tried to kill me.
Baba tumepigiana kelele sanaa kwamba mwambie mwambie sitakiiii. Na sahivi kazi hana wote nawalisha mimi, na wadogo zangu na waume zao na wake zao nawalisha mimi, nimepiga mkwara ole wake mtu atakae mwambiaaa mwanangu mambo ya kisengery nimeapa nachinja mbuzi 9 kufuta undugu wangu nae vizazi 9. And the boy is not making it any easier for them. Ana maswaliiii who was my father? What didi he do for a living. Sasa mkiwa waongo muwe na consistency. Mjomba akae anamwambia alikuwa Pilot. Mamdogo anamwambia alikuwa Professor wa chuo. Mamdogo mwingine anamwambia alikuwa sucessful business tycoon. Akaja kunibananisha mama niambie wewe how come my dad didi everything, uncle swears he was a pilot, anty says he was professor, and another aunty says he was a tycoon. Nikamwambia yes my boy, he was a pilot, he taught part time chuo cha ma pilot South Africa because he was the best at what he does. And on the side he was major business tycoon. YOUR FATHER WAS A MAN OF MANY TALENTS.
Weee asipige when i grow up i will be like my father A MAN OF MANY TALENTS. Nikamchenchia semaaa nafuta hii kauliii kwa damuuuu ya Yesu ilimwagika Calvary. Akagomaa why? Hawa watoto shule tunapasuka misamba wenyewe kuwapeleka ila ndo zina wapa over confidence huwezi kuwaburuta navotakaaa. I kabidi tu nitumie siasa kwamba your Dad died early, sasa careful what you wish for, na wewe utakufa mapema shauri yako.
Mara kwenye sala za usiku aseme i pray for my real Daddy where he is, is happy and thinks about us. Jamaniii ana majaribuuu huyu mtoto. Chaaaaaaaaaaaaaa! Baba ananiambia mwambie ukweliii ataelewaaa na atakuwa upande wakooo. Sasa jamani ukweli gani manake ndugu wasomaji tuangaliage na ukweli wa kuwaambia watoto wetu.
Mkitaka kujua ana majaribu siku waziri kaja nyumbani mchana na mishe mishe zake tu, na yeye akatoka shule na wenzie mi spoilled brats wenzieee. Wakamkutaaa. Sasa si mtu wa jamii aafahamikaaa kwa suraaa. Wenzie wakawa exited sanaaa na waziri tu wa siasa akawapiga siasaaa za hapa na pale. Wenzie wakauliza so he is your pops man, how cool! He is so cool! Sijui kwanini na kwa vipiii asijibu YES HE IS MY FATHER BUT HE IS NOT MY REAL FATHER. Ilikuwa aibuuuu kubwaa. Waziri akawa diplomatic tu, wenzie wakaondoka bila kuaga.
Waziri akanipigia simu kwa masikitiko makubwa mnoo mnooo kwanini mtoto aseme vile after everything he did for us. After all the money anazolipa ada, kufinance destinations vaccations kila likizo hakai nchini, anampeleka mpaka vaccations na wanae wa kuwazaa, he still considers him not his real father? What has his real fathe done for him so far. Najitetea kwamba sio mimi mwenyewe mtoto bangi zakeeee. Waziri anasisitiza malezi yangu sio mazuriii. Mimi ndo namlsiha hayo maneno. Akatishia kujitoa kabisaaa ijulikae moja yeye sio father kamili kama vipi. Nilijielezea nilijitetea. Akatoa msimamo if he repeats that statement one more time ataondoka kwenyemasiha yetu jumla, nifanye nifanyavo to put him in his place. Mtoto huyu anataka kunipanda kichwani.
Nilirudi nyumbani nikamuita chumbani, nikachukua mkanda wa suruali yangu PURE LATHER. Nikafunga mlango. Niliml mikwajuuuu sio ya nchi hiii. Nilipambana nae man to man. mamaeee. Namuuliza baba ako unamjua wewe msengery mkubwa kama baba yako mzazi. Ashawi kulipa ada? Ashawahi kukunulia hata panadol? K mamayo zako, anajua unavaa nini, unakula nini, umeamkia wapi? au umelalia wapi? Weweaaejua unakula nini, unavaa designers, unaenda vaccations zaidi ya waziri ni nani? Hanisiiii mkubwaa wewe usie na shukraniii shubhamiiit, mshenzi wahid wewe ndo wa kumwambia waziri He is not your real father? Nilimpigaaa mpaka nikasema sasa namuua huyu mtoto. Nalo limedidnda HE IS NOT MY REAL FATHER na mikanda yote nilio mkoga. Hasira zinapanda zaidiii, dada anagonga mpaka analiaaa, dada utamuaaa mtoto ashajifunzaaa basiii harudiii tenaaaa. Yaani nkasikia kitu kimenikabaa rohoniii, mpaka nikaanza kuomba Mungu nisilinyonge tuuu hili toto halina idea na linachokisemaaa. Nikafungua mlango nikalitoa nje nikajifungia na kuanza kuliaaa na kumuomba Mungu msamaha na nguvu ya kukabiliana na hili jaribuuu. Nilijifungia mpaka kesho yake.
Nikaliamshaliende shule, kavimba alama za mikanda mwili mzimaa, jicho imevilia damu, dada anasema mwache alale tu dada hayupo vizuri nikamuuliza unataka kazi hutaki? Aende shule. Shule wakawaita ustawi wa jamiiii, wakampigia wazirii, wanataka kunifungulia kesi ya domestic violence, wainyanganye custody, ilikuwa balaa. Waziri akawapa wapa helaaa ustawiiiwakalimaliza chini ya carpet. Akanishangaakwanini nimempigaaa vile? Nikamwambia kiukweli mimi huyu mtoto kashanishindaaa. Akasema hamna tena kumpigaaa kama kuna ishu mimi nitazungumza nae.
Siku hio hio sikumkawizaa nikamtaarifu ukishikwa na nyege au pepo au ukiwashwa tu kusema wazirisio baba yako real au fake utajua mwenyewe naaapaaa, kwa jina la mama yangu alielala kaburini Neema, nakufukuza humu ndani, wewe si mwanangu, sitohusika na lolote juu yako kama utaenda huko kaburini kuishi na baba yako utajua mwenyewe, kama utamfata rombo mnywe viroba wote mkabebe zege wote utajua mwenyewe, kweli kabisaa i rest my case. Consider your self warned. Nikaingia chumbani. Alijua kuningo vuzi zote kwa kuchaa. Alinitibuaaa.
Uhusiao wetu ukawa wa tia maji tia maji hivo hiv ila alijirekebisha kidogo akajua na mimi Mom Mafia. Nikaanza tu kuhanaika na maombi ya kumtenganisha na ukoo wao na maroho ya ukoo wao maana nishaona mtoto wa simba ni simba. Like father like son. Afu na huyu Ben 10 nae ndo anataka aingie kwenye picha hapo azidi kutibua tibuaa mavuziii si balaaa ndo litazidi.
Maombi yalisadia akaja kuniomba msamaha mwenyewe dogo akamuomba na waziri kwamba alikosea and he was ungratefulll. Despite his real father hayupo he is more than a father to him. Huyu mtoto kama jitu zima vileee linaweza fanya kitu ukabakia unatoa macho tu. Tukaanza kwenda sawa kidogo sasa.